Israeli imetoa onyo kali kwa nchi za ulaya

Israeli imetoa onyo kali kwa nchi za ulaya

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
13,709
Reaction score
25,487
Oya
Myahudi kachafukwa kinoma.
Hataki discussion na mtu yeyote yule.
=================
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas amependekeza awamu nyengine ya vikwazo dhidi ya mawaziri wawili wa Israel, walowezi wanaozua vurugu na viongozi 10 wa kundi la Hamas.

Waziri wa usalama wa Taifa wa Israel Itamar Ben-Gvir na Waziri wa fedha Bezalel Smotrich ndio walioangukiwa na vikwazo hivyo.

Israel kupitia waziri wake wa mambo ya nje Gideon Saar tayari imeshatoa onyo kwa Ulaya dhidi ya kuichukulia nchi hiyo hatua akisema hilo litaathiri matakwa ya Ulaya. Amesema hatua yoyote dhidi ya Israel itakuwa na majibu makali.

Wakati huo Shirika la habari la Palestina WAFA limeripoti kuwa mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza yamewaua watu 17 akiwemo mwanamke mja mzito.
 

Attachments

  • Screenshot_20250917_205815_Instagram.jpg
    Screenshot_20250917_205815_Instagram.jpg
    217.8 KB · Views: 12
Mzani unamuinamia, "narrative" inabadilika kwa kasi sana
 
Kwamba atawafanya wazungu wa ulaya kama waarabu hapo majirani zake anavyo wachakaza ?
 
Netanya kasema Israel itatengeneza silaha za kutosha bila utegemezi kauli za wenye chuki wamezichoka, mimi naunga mkono hoja, Iran yaliwakuta sema Iran anatumia third party and they pay well
 
Back
Top Bottom