MAXI SHIMBA ON LINE
YESU SI MUNGU:
KWA SABABU HANA SIFA ZA MUNGU
Mwenyezi Mungu Anazo sifa zifuatazo ambazo Yesu hanazo hata sifa moja wapo. Mwenyezi Mungu ndiye muumba wetu ambaye ni mmoja. Anajulikana na anatambulikana kwa sifa zake. Biblia inatuelezea sifa hizo. Hapa chini nitaeleza baadhi ya sifa za Mwenyezi Mungu zinazotajwa katika Biblia. Vilevile nitaeleza kwamba Bwana Yesu Kristo hana hata sifa moja sawa na Biblia.
1. MUNGU HAJARIBIWI
Biblia inasema kwamba: Mtu ajaribiwapo, asiseme, ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala mwenyewe hamjaribu mtu, (Yakobo 1:13).
Tuone hali ya Bwana Yesu Kristo kwamba yeye anayo sifa hii au ni kinyume chake.
Biblia inasema kwamba: Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi, (Mathayo 4:1). Mungu hajaribiwi lakini Yesu alijaribiwa na Iblisi, kwahiyo hawezi kuwa mungu, kwa sababu ya kukosa sifa hii ya Mungu
2. MUNGU HAFI
Mwenyezi Mungu ni hai ambaye anadumu milele na hatakufa. Akili inakubali kwamba Mungu ni yule ambaye anao uzima wa milele kama Biblia inavyosema kwamba: Mimi naweka amri, ya kwamba katika mamlaka yote, ya ufalme wangu watu watetemeke na kuanguka mbele za Mungu wa Danieli; maana yeye ndiye Mungu aliye hai, adumuye milele, na ufalme wake ni ufalme usioharibika, mamlaka yake itadumu hata mwisho. (Danieli 6:26).
Sasa tuone kwamba je, Bwana Yesu anayo sifa hii ya Mungu ya kuwa hai milele bila kifo.
Biblia inaeleza kwamba Bwana Yesu hana sifa hii:
Naye Yesu akisha kupaza sauti tena kwa nguvu akaitoa roho yake. (Mathayo 27:50). Hivyo mtu ambaye alifariki hawezi kuwa Mungu.
Wakristo wanaamini kwamba Bwana Yesu alifariki kifo cha laana lakini sisi Waislamu tunaamini kwamba Yesu hakufa kifo cha laana bali Mwenyezi Mungu alimsaidia
3. MUNGU ANAJUA KILA KITU
Ni sifa ya Mwenyezi Mungu kujua kila kitu cha dhahiri na cha siri. Kitu chochote hakiwezi kufichika
kwake.
Kama Biblia inavyosema kwamba: Basi usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukampe kila
mtu kwa kadri ya njia zake; wewe ujuaye moyo wake;(maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya
wanadamu wote. (1Wafalme 8:39).
Sasa tuone kiwango cha Bwana Yesu cha kujua mambo.
Biblia inasema kwamba: Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa. Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. Mtini ukanyauka mara. (Mathayo 21:18-19).
Mtu ambaye hajui kwamba msimu huu mti fulani haupatikani matunda ilhali hata watoto wadogo wanajua misimu ya matunda mbalimbali, hawezi kuwa Mungu.
Tena aya hii inaonesha tabia ya Bwana Yesu kwamba mwenyewe alikosea kujua msimu wa matunda ya mtini na kisha akaulaani mti bure.
Pia Bw. Yesu anakiri mwenyewe kwamba hajui chochote kuhusu habari za saa ile (Mathayo 24:36).
4. MUNGU HACHOKI
Mwenyezi Mungu hana kasoro ya udhaifu wowote.
Sifa zote njema zinamhusu yeye. Biblia inasema kwamba: Je, wewe hukujua? hukusikia? Yeye Mungu
wa milele, Bwana muumba miisho ya dunia, hasinzii wala hachoki, akili zake hazichunguziki. (Isaya 40:28).
Sasa tuone hali ya Yesu. Je, yeye anayo sifa hii ya Mungu? Kama hana, basi hawezi kuwa Mungu.
Biblia inasema: Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, Basi Yesu kwa sababu amechoka kwa safari yake,
akaketi vivi hivi kisimani. Nayo yapata saa sita. (Yohana 4:6).
Mwenye kuchoka hawezi kuwa Mungu.
5. MUNGU HAUWAWI
Mwenyezi Mungu ndiye mwenye mamlaka na nguvu zote na anao uwezo kamili, hawezi kushindwa mbele ya yeyote:
Watakushusha hata shimoni; nawe utakufa kifo chao waliouawa kati ya bahari. Je, utazidi kusema
mbele yake huyo akuuaye, Mimi ni Mungu?
Lakini u mwanadamu, wala si Mungu, mkononi mwake akutiaye jeraha. (Ezekieli 28:8-9).
Mwanadamu anauawa na bwana Yesu anayo sifa hii sawa na Biblia. Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimuuwa mkimtundika katika mti. (Matendo 5:30).
Mtu ambaye anatundikwa na anauawa hawezi kuwa Mungu. Bali ataitwa mtu dhaifu.
Sisi Waislamu hatuamini kabisa kwamba Bwana Yesu aliuawa au alitundikwa.
6. MUNGU HASINZII WALA HALALI
Mwenyezi Mungu ni mwenye uwezo wa aina zote ambaye hahitaji kupumzika wala kusinzia. Biblia inasema kwamba:
Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, yeye aliye mlinzi wa Israeli. (Zaburi 121:4).
Mungu hahitaji kusinzia wala kulala lakini Bwana Yesu alikuwa akilala sana. Kwahiyo hawezi kuwa Mungu. Biblia inasema kwamba: Ilitokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji. Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto, wakamwamsha, wakamwambia, mwalimu, si kitu kwako kama tunaangamia? (Marko 4:37-38; Mathayo 8:23-25).