Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,661
- 46,349
Waarabu hasa Wapalestina wamekuwa wakipambana kutotaka kulitambua kabisa taifa la Kiyahudi la Israel. Iran mpaka leo wanasema wazi taifa la Israel halina uhalali wa kuwepo juu ya uso wa nchi. Karibu kila taifa la Mashiriki ya Kati ama limewahi kuingia katika mgogoro au kupigana vita kabisa na Israel.
Kwa nini Waarabu hawawataki Wa-Israeli Mashariki ya kati? Historia ya miaka karibu 3500 inaonyesha uwepo wa taifa la Israel.
Kwa nini Waarabu wa Palestina hawataki kabisa kusikia wazo la uwepo wa taifa la Israel katika eneo asili la Wa-Israeli?
Inasikitisha sana mpango wa mataifa mawili tangu 1937 ambao Israel iliukubali mwaka 1947 na kwa muda mrefu wakiuridhia huku Wapalestina na Waarabu wengine wakiukataa kabisa mpaka kupelekea kupoteza kila kitu leo hii na vita visivyokoma.
Kwangu naamini uwepo wa taifa la Israel ambalo ni stable, lenye demokrasia imara na maendeleo ya juu sana katika eneo gumu la Mashiriki ya Kati ni jambo la manufaa sana kwa ukanda huo na dunia kwa ujumla.
Kwa nini Waarabu hawawataki Wa-Israeli Mashariki ya kati? Historia ya miaka karibu 3500 inaonyesha uwepo wa taifa la Israel.
Kwa nini Waarabu wa Palestina hawataki kabisa kusikia wazo la uwepo wa taifa la Israel katika eneo asili la Wa-Israeli?
Inasikitisha sana mpango wa mataifa mawili tangu 1937 ambao Israel iliukubali mwaka 1947 na kwa muda mrefu wakiuridhia huku Wapalestina na Waarabu wengine wakiukataa kabisa mpaka kupelekea kupoteza kila kitu leo hii na vita visivyokoma.
Kwangu naamini uwepo wa taifa la Israel ambalo ni stable, lenye demokrasia imara na maendeleo ya juu sana katika eneo gumu la Mashiriki ya Kati ni jambo la manufaa sana kwa ukanda huo na dunia kwa ujumla.