chamilo nicolous
JF-Expert Member
- Mar 10, 2016
- 2,112
- 1,492
Serikali imepokea mkopo wa Tsh. Trilioni 1.3 kutoka IMF ili kupambamana athari za Covid19 iliyoondoshwa kwa maombi mwaka jana wa 2020.
inasemekana, fedha hizo zitatumika kujenga madarasa, kuboresha huduma za afya nk.
Serikali imekopa matrilioni ya Shilingi kujenga barabara vijijini kutoka Benki ya Dunia, imekopa matrilioni ya shilingi kujenga reli, imekopa matrilioni ya shilingi kujenga bwala la kuzalisa umeme, imekopa matrilioni ya shilingi kujenga miundombinu ya mrafi wa mabasi ya mwendokasi.
Serikali imetumia matrilioni ya shilingi kununua ndege (fedha taslimu).
Unaweza kujiuliza; Kwanini serikali inakopa fedha nyingi kwa ajili ya huduma muhimu za kijamii, halafu inatumia fedha nyingi kununua ndege? Yaani unakopa kwa ajili ya afya, elimu na chakula halafu kile kipato chako unachovuna kwenye mshahara au faida ya biashara unatumia kununua saa kali ya Rolex au suti kali ya Giorgio Armani?
Unaweza kudhani serikali yako ni ya watu wajinga sana. Hapana, si wajinga. Wana akili nyingi tu, lakini si kwa ajili ya wengine, ni akili zao kwa ajili yao wenyewe.
Mikopo yote inalipwa kwa fedha za walipa kodi wa Tanzania, ambao watateswa kwa kuongezewa tozo, kodi kwenye bidhaa kama mafuta nk, na makato na malipo makubwa kwenye huduma za kijamii; afya, elimu, nk. Hayo hayawaumizi wakubwa wa serikali. Kwahiyo, waziri fulani kutia saini mkataba wa mkopo wa matrilioni ya Shilingi sio shida kwake. Taabu hazitamuhusu. Na kesho atatia saini manunuzi ya ndege au magari 400 ya kifahari kwa ajili ya 'viongozi'.
Zaidi, manunuzi ya ndege na vitu vingine kwa gharama kubwa, ni 'madili ya watu'. Kuna 10%, kuna 'cha juu', kuna 'commission'... Kuna...ujinga mwingi sana.
Natamani nije nichukue Form, nigombee Urais, nikomboe Nchii, je mtaniona??
inasemekana, fedha hizo zitatumika kujenga madarasa, kuboresha huduma za afya nk.
Serikali imekopa matrilioni ya Shilingi kujenga barabara vijijini kutoka Benki ya Dunia, imekopa matrilioni ya shilingi kujenga reli, imekopa matrilioni ya shilingi kujenga bwala la kuzalisa umeme, imekopa matrilioni ya shilingi kujenga miundombinu ya mrafi wa mabasi ya mwendokasi.
Serikali imetumia matrilioni ya shilingi kununua ndege (fedha taslimu).
Unaweza kujiuliza; Kwanini serikali inakopa fedha nyingi kwa ajili ya huduma muhimu za kijamii, halafu inatumia fedha nyingi kununua ndege? Yaani unakopa kwa ajili ya afya, elimu na chakula halafu kile kipato chako unachovuna kwenye mshahara au faida ya biashara unatumia kununua saa kali ya Rolex au suti kali ya Giorgio Armani?
Unaweza kudhani serikali yako ni ya watu wajinga sana. Hapana, si wajinga. Wana akili nyingi tu, lakini si kwa ajili ya wengine, ni akili zao kwa ajili yao wenyewe.
Mikopo yote inalipwa kwa fedha za walipa kodi wa Tanzania, ambao watateswa kwa kuongezewa tozo, kodi kwenye bidhaa kama mafuta nk, na makato na malipo makubwa kwenye huduma za kijamii; afya, elimu, nk. Hayo hayawaumizi wakubwa wa serikali. Kwahiyo, waziri fulani kutia saini mkataba wa mkopo wa matrilioni ya Shilingi sio shida kwake. Taabu hazitamuhusu. Na kesho atatia saini manunuzi ya ndege au magari 400 ya kifahari kwa ajili ya 'viongozi'.
Zaidi, manunuzi ya ndege na vitu vingine kwa gharama kubwa, ni 'madili ya watu'. Kuna 10%, kuna 'cha juu', kuna 'commission'... Kuna...ujinga mwingi sana.
Natamani nije nichukue Form, nigombee Urais, nikomboe Nchii, je mtaniona??
.