Ishi na watu kwa akili

Ishi na watu kwa akili

Mfano uko hospitalini unatakiwa ufanyiwe oparesheni ya jicho na kuna kiasi fulani cha fedha kinahitajika, unaeleza tatizo lako usaidiwe; matokeo yake wanakuambia Mungu atakusaidia utapona. Sasa ataponaje bila kupata matibabu?
Uwezo wa Mungu ni mkubwa, unaweza pata msaada kutoka sehemu usiyotegemea kabisa ukatatua tatizo. Kumbe huyo aliyetoa msaada ameongozwa na Mungu aje akusaidie.
 
Equation x hiyo nikama kutafuta thamani ya X ambayo bado ijapatikana
Binadamu wanachangamoto kweli, unamweleza shida zako ukifikiri atakusaidia ata kwa mchango kidogo; matokeo yake wanakushauri Mungu atakusaidia.

Sasa mtu ana njaa, hitaji lake kwa sasa ni chakula; sasa hapo Mungu atamsaidiaje, badala ya wewe kumuwezesha kula? Urafiki ni kutatua kero iliyopo, na si kuhamisha majukumu kwa muumba.

Hii kuhamisha majukumu ni dalili ya uchoyo.
 
Uwezo wa Mungu ni mkubwa, unaweza pata msaada kutoka sehemu usiyotegemea kabisa ukatatua tatizo. Kumbe huyo aliyetoa msaada ameongozwa na Mungu aje akusaidie.
Aliyeshiba ndio hupata nguvu ya kuomba, hujala siku 2 hiyo nguvu ya kuomba utaipata wapi?
 
Anvyokuambia Mungu atakusaidia anamaanisha kuwa Mungu atakupatia chakula kwa kumtumia mtu yoyote, hata ambaye hukumuambia shda yako............maana yy hana uwezo wa kukusaidia lkn Mungu anaweza
 
Nakubaliana na wewe 👆, kwa hiyo usimueleze mtu matatizo yako ambaye hawezi kukusaidia
Watu tunajuana hali zetu za kiuchumi, kuna mwngne unaona tu hana uwezo wa kukusaidia hata ukimuomba......lkn hii haimaanish usmuombe maana huez jua anaweza kukusaidia hata kmawazo tu.

Kuna weny uwezo lkn n wachoyo hata ukiwaomba msaada hawakusaidiii
 
Haukuweza kujisemea sasa ndiyo maana amesaidia kukumbushia.Hata kama ungeweza kujisemea sio vibaya akakumbushia maana ni jambo jema.Jifunze kuwa na shukrani
Shukrani kwa kupata maneno matupu haisaidii mkuu
 
Back
Top Bottom