Iringa Mjini kitimoto inatafunwa ni balaa

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,627
Nyama ya nguruwe aka Kitimoto inauzika na kuliwa Iringa mjini sijawahi kuona. Karibu na ofisi ya CCM Mkoa kuna mabanda mengi sana zaidi ya 100 yanauza na kukaanga nyama ya kitimoto kila siku kuanzia asubuhi mpaka usiku wa manane, na nyama inaisha aisee.

Unakuta bar moja imezungukwa na majiko mpaka 8 ya kitimoto, unakula lager, unatafuna mdudu kiroho safi kabisa , ukitaka na ugali au ndizi ni wewe tu.

Moshi, Arusha hawawafikii waHehe kwa kutafuna kitimoto aisee, siyo mbwa tena kama zamani.

Wanaikaanga vyema sana, makachumbari kama yote.

Na hali ya hewa ya Iringa ni kama imechujwa hivyo bia zinatembea tu.

Heko Iringa, watoto wa Mkwawa.
 
Bila picha itakua ni chai ya tangawizi
 
Hata wafuasi wa Chadema wapo hapo CCM mkoa wanakandamiza mbuzi Katoliki!
 
Bila shaka vibanda vya ccm hapo.!
 
Nyanda za juu kusini iringa niombe mbeya wanakula mbuzi katoliki sana aisee
 
Juzi nilikuwa morogoro maeneo ya kilakala aisee nguruwe analika sana !!!
Tuleni nguruwe kwa wingi jamani KASA anaua
Yakheee vipi.....Usiipe sifa mbaya nyama yetu ya KASA Yakheee.....
 
Wameelimishwa badala ya kula Mbwa wawe wanakula poko
 
Moshi Asubuhi na mapema majiko yamewashwa tyari Ni mwendo wa kuagiza tu.
 
Kulikuwa na bar inaitwa luxury kwa upande wa CCM mkoa hivi bado ipo? Kwa upande wa nyuma highland cinema ndio Kuna mabanda ya kitimoto hatari hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…