IAEA yathibitisha mpango wa Iran wa kuzalisha uranium Shirika la kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) limethibitisha mpango wa Iran wa kuzalisha uranium.
Mwakilishi wa nchi hiyo katika IAEA ameeleza kwamba mpango huo unalenga kuzalisha fueli ya aina mpya kwa ajili ya kinu cha nyuklia cha Tehran, na Iran imeripoti hatua zote husika kwa IAEA huku maofisa wa shirika hilo wametembelea kinu cha kuzalisha uranium mwezi huu.
Taarifa moja iliyotolewa na IAEA imesema Iran imeliarifu kuwa kazi yake ya utafiti wa nyuklia haitazuiliwa na kanuni yoyote.
Baada ya kupunguza ahadi kwenye makubaliano juu ya suala la nyuklia la Iran mwezi Januari mwaka jana, Iran ilitangaza kuwa utafiti wa nyuklia hautazuiliwa na utafanyika kwa mujibu wa mahitaji ya nchi hiyo.
Na habari nyingine zimesema hivi karibuni Kikosi cha wanajeshi wa baharini cha Iran kimefanya mazoezi ya kijeshi na kuonyesha meli mbili mpya za kivita.
Moja inayoitwa Makran yenye urefu wa mita 228 inaweza kubeba helikopta 5 na vifaa vya tani 82,000 na kuendeshwa kwa siku 1000 bila ya kutia nanga.
Na meli nyingine ya kivita ambayo ilionekana katika mazoezi hayo ni Zereh, yenye urefu wa mita 47, inaweza kurusha makombora kutoka kwenye meli yenye masafa ya kilomita 300.
Mwakilishi wa nchi hiyo katika IAEA ameeleza kwamba mpango huo unalenga kuzalisha fueli ya aina mpya kwa ajili ya kinu cha nyuklia cha Tehran, na Iran imeripoti hatua zote husika kwa IAEA huku maofisa wa shirika hilo wametembelea kinu cha kuzalisha uranium mwezi huu.
Taarifa moja iliyotolewa na IAEA imesema Iran imeliarifu kuwa kazi yake ya utafiti wa nyuklia haitazuiliwa na kanuni yoyote.
Baada ya kupunguza ahadi kwenye makubaliano juu ya suala la nyuklia la Iran mwezi Januari mwaka jana, Iran ilitangaza kuwa utafiti wa nyuklia hautazuiliwa na utafanyika kwa mujibu wa mahitaji ya nchi hiyo.
Na habari nyingine zimesema hivi karibuni Kikosi cha wanajeshi wa baharini cha Iran kimefanya mazoezi ya kijeshi na kuonyesha meli mbili mpya za kivita.
Moja inayoitwa Makran yenye urefu wa mita 228 inaweza kubeba helikopta 5 na vifaa vya tani 82,000 na kuendeshwa kwa siku 1000 bila ya kutia nanga.
Na meli nyingine ya kivita ambayo ilionekana katika mazoezi hayo ni Zereh, yenye urefu wa mita 47, inaweza kurusha makombora kutoka kwenye meli yenye masafa ya kilomita 300.