IPTL kushusha bei ya umeme kutoka sh 450 hadi sh 80 kwa Uniti

Tujikumbushe!

View attachment 196306

Mshauri wa Biashara wa Kimataifa wa Kujitegemea wa Kampuni ya VIP, James Rugemarila (katikati) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya IPTL akizungumza na waandishi wa habari leo Ofisini kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam kuhusiana na Kampuni ya VIP kumaliza mgogoro uliokuwepo kati ya VIP na IPTL uliodumu kwa muda mrefu. (Kushoto kwake) ni Mkurugenzi Mteule wa VIP, Benedictor Rugemarila. (Wa kwanza kushoto) ni Mshauri wa Masuala ya Usalama wa kampuni hiyo, Kamala Stephen aliyehudhuria mkutano huo wa waandishi wa habari.

Kampuni ya VIP imemaliza mgogoro wa muda mrefu uliokuwa baina yake na Kampuni ya IPTL katika Mahakama Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam tangu Februari 25,2002.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, Mshauri wa Biashara wa Kimataifa wa Kujitegemeawa wa VIP, James Rugemarila ambaye pia ni Mkurugenzi wa IPTL, alisema kuwa mgogoro huo ulidumu kwa muda mrefu na kuwagharimu fedha nyingi.
Aliongeza kuwa mgogoro huo ulikuwa na tafsiri mbalimbali na
kwa kuwa ulikuwa mahakamani walishindwa kutoa taarifa kwa jamii kuhofia kuingilia uhuru wa mahakama.
Rugemarila alisema kwa kuwa umeisha wameamua kuweka kila kitu wazi ili jamii ielewe na taarifa hizi zitatangazwa kwenye magazeti ya Jambo Leo, The African, Daily
News, Guardian, blogus, Channel Ten, ITV nk.
Akizungumzia zaidi kuhusu Kampuni ya Pan Africa Power Sulutions Tanzani LMT, iliyonunua hisa za VIP kwenye IPTL na kupewa kibali na VIP kuhalalisha ununuzi wa shea za Mechmar katika IPTL, alisema itawakomboa wananchi kwa kupata nishati hiyo kwa bei nafuu.
Aliongeza kuwa katika muda mfupi baada ya kampuni hiyo kuanza kazi itazalisha megawati 500 kwa bei kati ya uscents 6 na uscent 8 kwa kila unit ukilinganisha na bei za sasa zinazotozwa na makampuni ya kuzalisha umeme zilizo kati ya uscent 33 na 55 uscen kwa unit moja.

“Hii ni kampuni ya Kitanzania, ambayo ni bahati mbaya tu huyu Mkurugenzi wa PAP, Dr. Harbinder Singh Sethi amefiwa na jamaa yake ndiyo maana hayupo tutamleta mtamuona atakuja Jumatatu mtawasiliana naye, inaonesha Watanzania tunaweza,” alisema Rugemarila

Asante kwa taarifa!!
 
Kutokana na hukumu ya Mahakama Kuu, Kampuni ya PAP ilijadiliana na wadai halali wa mikopo ya IPTL na kuingia Mkataba wa kuwalipa wadai wote wa IPTL isipokuwa SCB-HK ambaye hakuwasilisha madai yake.
SCB-HK iliyokuwa ikiidai IPTL fedha ilizotumia kununua deni lililotokana na kufilisiwa kwa MECHMAR kule Malaysia (siyo Tanzania) haijawahi kujadiliana na IPTL kuhusu malipo ya mkopo wake kama upo. Mvutano huu unaendelea ICSID kati ya TANESCO na SCB –HK, ukiitaka TANESCO ilipe gharama za kununua umeme ikijumuisha deni la IPTL. Madai ya SCB –HK dhidi ya TANESCO yanatokana na madai ya kuwepo kwa deed of Assignment ya MECHMAR kuhusiana na Mkopo wa IPTL ambapo Mtambo wa IPTL uliwekwa kama dhamana ya mkopo. Hata hivyo deed of assignment hiyo haikuwahi kusajiliwa hapa nchini kama inavyotakiwa katika kifungu Na. 172 cha sheria za makampuni Cap. 212 zinavyoelekeza Kwa kutokusajili assignment deed hiyo, SCB –HK ilikosa sifa ya kufungua madai yake hapa nchini badala yake ilifungua madai haya ICSID nchini Uingereza kama ilivyoelezwa kwenye kifungu Na. 2.8.2 cha taarifa hii, kitu kinachoonyesha kudharau Mahakama zetu

TANESCO pia ilitoa hoja kwamba Mahakama ya Usuluhishi haina mamlaka ya kusikiliza mgogoro huo kwa vile SCB-HK haikuomba ruhusa ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuwasilisha shauri hilo kwenye Mahakama ya Usuluhishi kwa kuwa haikuandikisha mkopo huo hapa nchini kama inavyotakiwa katika kifungu Na. 172 cha Sheria ya Makampuni Cap 212. Pamoja na TANESCO kuweka pingamizi hili, wakili wake Mkono & Co Advocates hakuitetea hoja hii wakati wa kesi katika ICSID;
Wakati kesi ikiendelea ICSID Mahakama Kuu ya Tanzania iliiondoa kampuni ya IPTL katika ufilisi, TANESCO walimuomba wakili kuwasilisha taarifa ICSID ya IPTL kuondolewa katika ufilisi ili SCB –HK iondoe kesi hiyo mahakamani na kuwasilisha madai yake kwa IPTL, kampuni ambayo sasa ni hai (Solvent) kulingana na uamuzi wa Mahakama Kuu. Mawakili wa TANESCO Mkono & Co Advocates, hawakuwasilisha ombi hilo ICSID na kuifanya ICSID iendelee na kesi hiyo hadi ilipotoa uamuzi tarehe 12 Februari, 2014
ICSID katika uamuzi wake ilielekeza SCB – HK na TANESCO wakubaliane kuhusu namna ya kukokotoa tariff ndani ya muda wa miezi mitatu na kuwasilisha makubaliano yao ICSID. Mawakili wa TANESCO hawakuonesha dalili yoyote ya kutoridhishwa na uamuzi huo, badala yake walisisitiza kuishauri Serikali na TANESCO itekeleze maelekezo hayo ya ICSID huku wakijua kuwa SCB – HK na TANESCO hawana uhusiano wowote wa kimkataba.

Kafulila Hatuwezi kuwalipa SCB-HK kama unavyotaka wewe, Tanzania haijawahi kuingia mkataba na SCB-HK

View attachment 195834

tumemquote hapo alipokuwa akiongea na mwandishi wa Raia mwema.

Hata mimi nilianza kuhisi hapa maana makala nyingi hata za Zitto zinaitaja sana SCB-HK, hawa jamaa wanapigania maslahi ya SCB-HK kumbe. Lakini ishakula kwao maana IPTL imembwaga SCB-HK mahakama kuu.
 
[h=2]Maswa awazodoa Zitto na Kafulila[/h]
Eliakim-Maswi.jpg

, ameingia katika vita ya maneno na wabunge kwa kuwaporomoshea matusi huku akisema anataka kukabiliana nao nje ya Bunge.
Aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu mkakati na mwelekeo wa sekta ndogo ya umeme.
Maswi alitangaza ‘vita' hiyo na wabunge alipokuwa akijibu maswali ya waandishi baada ya kumaliza kueleza mkakati wa sekta hiyo.
Waandishi walimtaka aeleze mkakati wa wizara yake wa jinsi inavyokabiliana na

mikataba mibovu na matumizi mabaya ya fedha, mambo ambayo yanaweza kuigharimu wizara na kuifanya ifikie malengo yake.
Akitoa maelezo, Maswi alisema wizara hiyo haijawahi kupitisha mikataba mibovu tangu awe katibu mkuu wake.
Maswi alisisitiza kuwa hakuna ukweli wowote kuhusiana na madai ya matumizi mabovu ya fedha na kwamba hata ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) iliipa wizara hiyo hati safi.
Hata hivyo, wakati akiendelea kutoa ufafanuzi wa masuala hayo, ghafla alitaja majina ya baadhi ya wabunge kama vile Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) na mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) akidai kuwa ni wezi.
"Tatizo la nchi hii kuna watu wanaongea tu… sasa wanatudhalilisha. Mimi nataka mtu anayejiona ni mwanaume aje hapa aseme siyo tunatishana tishana tu hapa. Ukiwa bungeni ndiyo unajifanya ni mwanaume. Hawa Kafulila na Zitto ni wezi na washenzi.
"Wakati mtu mwenyewe ni mshenzi tu. Hakuna hapa… kama mwanaume aseme huku nje na mimi niwaambie waandishi mkija mje na ushahidi.
"Mimi simtetei mtu najiamini sili rushwa. Mimi sichukui rushwa na sintochukua, niliwaambia mkitaka nifuatieni… unaweza kuja nyumbani kwangu nikakuonyesha vitu vyangu na kukuambia nilivipataje.
"Lakini mshenzi mmoja ananyanyuka huko… hoo Maswi mwizi, sijui nini, mshenzi tu. Mimi nasema kama akiwa ni mwanaume aseme nje huku.
"Kwa nini usemee bungeni? Kwa sababu pale kuna immunity (kinga), kama wewe ni mwanaume useme kama mimi hapa halafu utanitambua kwamba mimi nani, nitakushughulikia tu.
"Hata na mimi juzi nilivyomsikia Werema (Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick) anasema tumbili nikasema kweli katumbili kale, hatuwezi kuchezeana," alisema na kuongeza:
"Naomba ukitoka hapa ukamwambie Kafulila kwa sababu najua ni mtu wake, ni mshenzi na mwambie nimesema ni mshenzi. Kafulila na mwenzake Zitto wamechukua hela, mnafikiri sijui, najua na ni kwa sababu ya njaa, njaa zao tu, na nimemwambia kama yeye ni mwanaume aseme open hapa."
Maswi alisema kwa sababu hiyo ndiyo maana Zitto hajawahi kuchangia hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini tangu yeye awe katibu mkuu wa wizara hiyo.
"Hawezi kuchangia kwa sababu namjua, mwizi mtupu… tangu niingie hajawahi kuchangia labda juzijuzi kwa sababu alikuwa na matatizo….naye Kafulila hivyohivyo tu. We know (tunajua) kwa sababu mimi siyo mwanasiasa siwezi kusema ovyo.
"Mimi nina ethics (miiko). Mimi nimelelewa na kama hujalelewa nyumbani kwenu utalelewa na dunia, kwa hiyo (anamtaja mwandishi) kamwambie kwanza mimi namsubiri sana yaani nina usongo naye," alisisitiza Maswi.
Katibu Mkuu huyo alisema aliwahi kumpigia simu Kafulila na kumwambia kama yeye ni mwanaume ayazungumze masuala hayo nje ya Bunge.
 
Kwelo ccm inajua jinsi ya kitega mitego yake ili ipate kura zetu! Hii yote ni njia za kutafuta point za kusimamia pindi muda wa kampeni utakapokuwa umewadia kwa kigezo kuwa waonewe huruma ya kubaki madarakani ili wakamilishe ndoto zao! Kuwa macho sana nao.
 
Watu hamfanyi kazi kwa bidii, ustaadi na uadilifu, msimamie rasilimali mlizopewa na huyo Mungu, mnaomba miujiza ya Mungu kuwezesha umeme ushuke bei, yaani Mungu awezeshe umeme ushuke bei kwa watu wanaolala nyumbani kuanzia asubuhi mpaka jioni, kwa watu wasiosimamia rasilimali vizuri, kwa watu wasiochukua tahadhari bali wanamwomba Mungu ugonjwa wa Ebola usiingie nchini mwao, wanamwomba Mungu alete mvua badala ya kujenga mabwawa ya kuvuna maji, Eeee Mungu una kazi sana. Haya omba Mungu akujengee nyumba na akusomeshee watoto wako.

kwani vibaya mkuu?
 
Kwelo ccm inajua jinsi ya kitega mitego yake ili ipate kura zetu! Hii yote ni njia za kutafuta point za kusimamia pindi muda wa kampeni utakapokuwa umewadia kwa kigezo kuwa waonewe huruma ya kubaki madarakani ili wakamilishe ndoto zao! Kuwa macho sana nao.

ndivyo ilivyo siyo?hatari sana.
 
Kwelo ccm inajua jinsi ya kitega mitego yake ili ipate kura zetu! Hii yote ni njia za kutafuta point za kusimamia pindi muda wa kampeni utakapokuwa umewadia kwa kigezo kuwa waonewe huruma ya kubaki madarakani ili wakamilishe ndoto zao! Kuwa macho sana nao.

Toa ujinga wako humu, CCM wametajwa wapi kwenye topic? kama huna hoja bora upate mawazo ya wengine tu alafu upite. Akili za kizwazwa tu! IPTL ndio wanaosema watashusha bei ya umeme siyo CCM,
 
kwani vibaya mkuu?

ndio, ni vibaya Mkuu, kwa sababu tayari waliotangulia wakati dunia inaumbwa walimwomba Mungu akawasikia na kutuweka kwenye nchi yenye rasilimali nyingi, kwa hiyo tunachopaswa kufanya ni kumwomba Mungu atujalie afya ili tuweze kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo, lakini sio kuendelea kumsumbua Mungu atuletea maendeleo ilihali tunashinda vijiweni na kuwafuata wanasiasa kwa maslahi yao binafsi.
 
ndio, ni vibaya Mkuu, kwa sababu tayari waliotangulia wakati dunia inaumbwa walimwomba Mungu akawasikia na kutuweka kwenye nchi yenye rasilimali nyingi, kwa hiyo tunachopaswa kufanya ni kumwomba Mungu atujalie afya ili tuweze kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo, lakini sio kuendelea kumsumbua Mungu atuletea maendeleo ilihali tunashinda vijiweni na kuwafuata wanasiasa kwa maslahi yao binafsi.

Vijana wafanye kazi, nyinyi ndio engine ya hii nchi. Tafuteni fursa zifanyieni kazi siyo unapiga hatua mbili harafu unarudi nyuma hatua tatu, unaingiza laki moja unataka kunywa pombe za laki mbili. Msipofanya kazi vijana mtaendelea kutumika na wanasiasa uchwara kama Kafulila na itakuwa ngumu kuleta mabadiriko ya kweli katika hii nchi.
 
sasa hawaogopi hasara?na walikuwa wapi siku zote mpaka wasubiri uchaguzi?
 
Hizo mbwembwe za uchaguzi 2015,afadhali mturudishie fedha zetu mlizotuibia kupitia tegeta escrow account na richmond.
 
Hizo mbwembwe za uchaguzi 2015,afadhali mturudishie fedha zetu mlizotuibia kupitia tegeta escrow account na richmond.

IPTL ni chama kipya cha siasa kumbe asante mkuu nilikuwa sijui! mkuu Tegeta escrow account ndio kitu gani naomba mawazo yako mkuu. Richmond nawaelewa sindio ile kampuni hewa ambayo hata mmliki wake alikuwa hafahamiki, lakini walikuwa wakichota mihela na baadae wale wenzao kina Dowans wakashinda kesi na kutudai mihela!
Mkuu rudi unifundishe kuhusu escrow account, nini chanzo chake na vinamahusiano gani na IPTL.
 
Hizo mbwembwe za uchaguzi 2015,afadhali mturudishie fedha zetu mlizotuibia kupitia tegeta escrow account na richmond.
Kwa faida ya JF tufahamishe uhusiano wa IPTL na ESCROW ni upi?
 
Kura yenu hapo inahitajika... Kweli ukiwa maskini utachezeshwa hadi ngoma za wanyama........
 
Hivi ni kweli unaendelea kuamini kelele za kafulila? naomba nikukumbushe yafuatayo;
Kafulila alisema Seth ambaye ni mwenyekiti mtendaji wa PAP/IPTL ni fisadi na kwamba serikali ya Kenya imempiga marufuku kuwekeza nchini humo. Jibu lake likawa hili;

KAMPUNI ya kufua umeme ya Pan African Power Solution inayoimiliki kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) imezidi kung’aa katika nchi za jumuia ya Afrika Mashariki katika kusambaza nishati ya umeme.
Hatua hiyo inasababishwa na serikali ya Kenya kuipatia barua kampuni hiyo ya kufanya nao kazi ya usambazaji umeme katika mradi unaohusisha nchi mbili za jumuia hiyo, ambazo ni Tanzania na Kenya.
Barua ya Kenya iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Petroli, Injinia Joseph .K. Njoroge ya tarehe 19, Agosti 2014 kwenda kwa Mwenyekiti Mtendaji wa PAP, Harbinder Sing Sethi.

Katika mwendelezo wa porojo zake akaja na la Prof. Tibaijuka, akimta Mkurugenzi wa PCCB Dr. Hosea amkamate na kumshitaki Prof. Tibaijuka kwa kuhongwa pesa za akaunti ya Escrow. Ukweli ni huu;

PAP wamekanusha kuwa pesa alizopewa Prof. Tibaijuka hawahusiki nazo bali ni za mwanahisa wa zamani wa iptl bwana James Rugemalira ambaye wakati anatoa pesa hizo hakuwa mwanahisa kwani alishauza hisa zake 30% kwa PAP. Mchakato ambao ulifanyika kwakuzingatia sheria na nyaraka zipo Brela.

Leaving other people to speculate and going on giving
misleading information about the money is not proper. Facts
are available that clearly shows that the money in escrow
account do not belong to the public. It is privately-owned
money.
 
Hizo mbwembwe za uchaguzi 2015,afadhali mturudishie fedha zetu mlizotuibia kupitia tegeta escrow account na richmond.

Leaving other people to speculate and going on giving
misleading information about the money is not proper. Facts
are available that clearly shows that the money in escrow
account do not belong to the public. It is privately-owned
money.
 
Back
Top Bottom