Ipi inawatofautisha hawa Wapambe wa Marais ?

Ipi inawatofautisha hawa Wapambe wa Marais ?

Kennedy

Platinum Member
Joined
Dec 28, 2011
Posts
61,643
Reaction score
74,512
Salam Wakuu !

Marais karibu Dunia nzima wana ADC wao kila wanapokwenda nadhani ni kutokana na umuhimu kwa Cheo cha Rais.

Naomba ikiwa mtu anajua kwa undani hii tofauti mfano ni Rais wetu hapa Tanzania muda wote awapo na MPAMBE(ADC) wake huwa amevaa Kijeshi .


Mfano mwingine ni baadhi ya Nchi ambazo Wapambe wa Marais ni mara chache sana kuwaona wakiwa wamevaa kijeshi.

Napenda nitaje baadhi ya nchi chache tu kama mfano US,Ufaransa,Canada na Urusi hawa huwa mara nyingi wamevaa suti nadhifu tena wakati mwingine za kufanana mpaka kushindwa kumjua Mpambe wa Rais ni yupi?

Rais Obama alipokuja hapa Tanzania Mpambe wake alikuwa amevaa Kijeshi kama anavyovaa Mpambe wa Rais wetu hapa.

Lakini Mpambe huyo huyo akiwa ama kwao US ama pia baadhi ya Nchi kama ziarani mfano China,Urusi na Mataifa kadha wa kadhaa huwa havai kijeshi kama alivyokuja Tanzania.

Huyu Mpambe wa Rais wetu wa Tanzania mara nyingi yupo kwenye sare za Kijeshi hakuna muda tumemuona akiwa kwenye suti na aina nyingine ya mavazi awapo sambamba na Rais.

Hii ni nini tofauti yake?
 
Mfano rais wa US anabadili walinzi kutegemea na sehemu anazoenda.

Nje ya US inahusisha zaid ya Secret Service. Kuna agencies nyingi zinaingia hapo kama CIA, FBI, US marines

Ila within US secret service na FBI ndo wana play role kubwa

KWa viongozi wa africa sijajua chochote
 
Mfano rais wa US anabadili walinzi kutegemea na sehemu anazoenda.

Nje ya US inahusisha zaid ya Secret Service. Kuna agencies nyingi zinaingia hapo kama CIA, FBI, US marines

Ila within US secret service na FBI ndo wana play role kubwa

KWa viongozi wa africa sijajua chochote
Sawa Sawa
 
Mfano rais wa US anabadili walinzi kutegemea na sehemu anazoenda.

Nje ya US inahusisha zaid ya Secret Service. Kuna agencies nyingi zinaingia hapo kama CIA, FBI, US marines

Ila within US secret service na FBI ndo wana play role kubwa

KWa viongozi wa africa sijajua chochote
Mm si mweledi sana ila hili jibu kama kasa au tango pori. Anyways ngoja tuwasubiri wajuvi waje.
 
Back
Top Bottom