Ipi flat screen bora kati ya matoleo haya?

Ipi flat screen bora kati ya matoleo haya?

Mimi nilinunua LG tena kwa bei kubwa. Ilikufa baada ya mwaka mmoja. Yaani waranty iliisha wiki hii yenyewe ikafa next Week. Iliniuma sana maana niliweka pesa nyingi pale.

Nikajiapia next time sitanunua TV ya bei ghali. Nitanunua ya bei ya kawaida ili hata ikifa nisipate hasara.

Baada ya hapo nikanunua Aborder. Nashukuru mpaka leo haijasumbua. Hata ikiharibika asubuhi tu jioni nanunua nyingine coz it is cheap.
Boss, asante kwa kuni-quote. Na mimi nilikua na LG 32" nikajiona nimetoooka nayo imekufa juzi juzi.

Tena ilikua 720p HD, sahivi nataka ninunue Hisanse 1080 FHD au 4K kabisa maana naona ni cheap.
 
Tv ni utuzaji wako tu. Ukiifunga ukutani na ikatulia vizuri bila kubuguziwa itakaa muda mrefu tu. Mimi nilikaa na star X 24’ miaka mitano hadi nilipoiuza na kununua 43.
Same to me
Yangu ina miaka mitano na wala haina dalili za kuchoka
 
Nina tv evvoli 43EV100 led tv

Sasa kuna baadhi movie kutoka kwenye flash hazitoi SAUTI.

--Je tatizo ni movie zenyewe "zilivyodounlodiwa" ama

--Shida ni tv yangu?
 
LG,SAMSUNG,SONY BRAVIA, HISENSE na TCL , nje ya hapo mkuu mimi sinunui yaani bora hata ninunue 24 inches ya brands hizo kuliko hayo majina inch 50
Mimi nimeuza 32 ya kichina nikanunua LG 27 ipo quality sana kweli nilikua natumai taka taka sasa hivi najichanga ninunue 43 LG
 
Kuna watu wamekariri brand tu ila electronics zipo nyingi sana na nzuri. Mimi natumia Evvoli ni bonge la tv, mwaka wa 10 huu iko kama original. So ni chaguo lako tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom