Ipi flat screen bora kati ya matoleo haya?

Ipi flat screen bora kati ya matoleo haya?

Hicence, Boss, Lg mwanza zinapatikana kikubwa mfuko wako tu mkuu.
Kama kwa bei zipi. Nahisi unaweza kuta zipo juu hata kwa zaidi ya 100k au 150k ukilinganisha na bei za huko dar. Nipe chimbbo na bei zao zikoje nikazame mwisho wa mwezi huu. Au niagize kitoka dar
 
Agiza kutokea tunduma utapata kwa bei rahisi izo Brand kubwa mfano inch 43 Samsung utapata kwa 450K.
Tupeane majina ya brands, specification zake na bei zake. Na machimbo wapi zinapatikana ili tuweke na sisi ndani.
Napendelea
Sony 32"
Lg 32"
Tcl 32"
Hicence 32"
Boss 32"
Wenye kujua bei zake zikiwa mpya na pia naomba kujuzwa na bei zake kwa smart tv pia.
Maana huko instagram wauzaji wengine naona wamejaa utapeli. Licha ya kwamba navutiwa na huyu jamaa anaitwa LAMPARD ELECTONICS.

Naishi MWANZA vipi huku mwanza maduka ya electronics kama hizo sijui yapo na bei zimekaaje maana kitu kije kitoke dar kifike mwanza unaweza uziwa kwa bei iliongezeka zaid
 
Kitu Sony Bravia nakikubali sana. Rangi nzuri na Speaker nzuri wala hauhitaji kuunganisha na Sabufa.
Sauti ya Home Theatre ina ladha yake mkuu, yaani ukiunga hiyo Sony Bravia na 5.1 au 7.1 soround system hutachoka kuangalia either movie au kutazama music, hasa kama ngoma ni smart na unaingia huko Netflix, YouTube nk mzee
 
Kama kwa bei zipi. Nahisi unaweza kuta zipo juu hata kwa zaidi ya 100k au 150k ukilinganisha na bei za huko dar. Nipe chimbbo na bei zao zikoje nikazame mwisho wa mwezi huu. Au niagize kitoka dar

Za 100k hazipo, zinaanzia 400k na kuendelea
 
Habarini, naomba kujuzwa katika hizi flat screen za wananchi wa kipato cha kawaida, ni ipi bora kuliko zingine?

-Star-X tv
-Aborder tv
-Sundar tv

Hapa siongelei zile za kibosile kama Sony, LG na Samsung.
Mkuu kuna wachina wastaarabu kama TCL, Hisense, Xiaomi etc ukinunua Tv zao
1. Operating system inakuwa Android tv ambayo ipo optimized na TV.
2. Bei zao za kawaida Around 400k unapata smart ya 32 inches.
3. Specs nyengine pia zinakuwa decent kama kutumia vioo vya Ips, speaker nzuri etc.
 
Mkuu kuna wachina wastaarabu kama TCL, Hisense, Xiaomi etc ukinunua Tv zao
1. Operating system inakuwa Android tv ambayo ipo optimized na TV.
2. Bei zao za kawaida Around 400k unapata smart ya 32 inches.
3. Specs nyengine pia zinakuwa decent kama kutumia vioo vya Ips, speaker nzuri etc.
Vp mkuu kwa hizo ulizotaja ni bei gani kwa inch24 na 32??
 
Sorry nje ya mada. Tv yangu nikiangalia kupitia king'amuzi picha haiwi screen nzima inakuwa imejikata, space inabaki juu na chini lakini nikisema niangalie labda series au movie kutoka kwenye flash inaonekana vizuri screen nzima. Kwa mwenye kujua tatizo litakuwa nini.
Kuna kitu kinaitwa Aspect ratio ambazo ni maarufu ni
-16:9 ambayo ni likely itaweka huo weusi unaouna juu na chini ikiwa tv yako ni ndefu
-4:3 ambayo inapendeza kwa tv ndefu kama za chogo.

Hivyo unaweza ukacheza na hizo aspect ratio ipo option ya kustrech screen ili ienee kote.

Kwa remote ya Dstv angalia hii video inakupa maelekezo decoder za zamani na mpya

 
Agiza kutokea tunduma utapata kwa bei rahisi izo Brand kubwa mfano inch 43 Samsung utapata kwa 450K.
Mkuu mm naishi mwanza. Iyo biashara ya kupitia tunduma imekaaje. Nieleze kidogo nipate ufahamu, maana sipo vizuri kwenye huu uwanda wa kuagiza vitu kwa cost benefit analysis
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom