Iphone bila jailbreak ni kukosa mengi

Mkuu naomba orodhesha mambo unayokosa uki jailbrake iphone yako
Almost hakuna la maana zaidi ya wao Apple kukukosesha mambo ya maana kwasababu za kibiashara zaidi

Apps nyingi za muhimu ambazo zina-involve security hazi-run kwenye jailbroken device, mfano online banking apps, bado warranty ndo imekufa hivo, sasa some devices huwezi kurestore completely, na kwa nini nipoteze muda kukomaa na vitu ambavyo haviko stable, still unakua wa mwisho kupata updates from apple, inakulazimu kujaribu kurestore then u-update, then usubiri hadi developers wajailbreak kila update mpya ikitoka. Why all that trouble
 
Nishafanya hii procedure ila haimalizi kuisntall, inatoa error (#-1)

Mkuu uliiwasha kwenye dfu mode, ume download IPSW linalofaa kwa simu yako ambalo ni juu au sawa na ios iliyokuwa kwenye simu yako before.
Maana sometimes hiyo error husababishwa na kutumia IPSW ya zaman
 
Binafsi sijawahi kushindwa kuinstall apps yoyote sababu simu yangu ipo jailbroken

Ndio maana nikasema inategemeana na matumizi ya mtu pia, kwa watundu wa simu na wanaopenda kucheza na simu kama mimi habari ya kurestore ni issue ndogo sana

Swala warrant kibongo bongo ni kama nadharia tu
Shida ni hiyo moja ya kusubiri developer wafanikiwe kujailbrake

Halafu nimegundua jailbrake ni kama addiction flani hivi ukiizoea huwezi kuiacha
Nimeanza na 3g hadi sasa nina 5s mwendo ni jailbrake tu na sijawahi kujuta mkuu

Ilibidi nikomae na ios 7.2.1 sababu developer walisitisha jailbrake kwa ios 8 lakini naona ios8.3 tayari wameisha fanya yao
 

Mfano app gan haikubari kwenye jailbreaked iphone? Sijawahi kukutana na apps yoyote ikakataa installation.
Kuresore iphone mbona kitu kidogo sana na very easy. Update za OTA ndizo hutopata ili via itunes unapata mbona kawaida tu sema uki update ndio basi tena the device inarud kuwa not jailbreaked.
Device iko stable kama kawa sijaona ina crash tatizo.
Ukirestore device hakuna anayeweza jua kama uliwahi jailbreak hiyo simu
 

Hizo features zinazoongezeka baada ya jailbreaking zipo weak sana kunishawishi kujailbreak simu, ipad au macbook yangu.

I'm comfotable with the features zinazokuja na simu.
 
Hizo features zinazoongezeka baada ya jailbreaking zipo weak sana kunishawishi kujailbreak simu, ipad au macbook yangu.

I'm comfotable with the features zinazokuja na simu.

Upo sahihi mkuu kwamba wapo watu wanatumia kitochi na wapo comfortable na futures zake kwa asilimia mia

Ukweli utabaki alivyosema Jay Freeman (Saurik) " jailbroken is better than unjailbroken idevice

Ukijailbrake idevice yako hutakosa kitu ila utaongeza vitu
Na usipo jailbrake utakosa vitu
 
Hiyo ni kweli mimi nimejaribu ku-Jailbreack kwa kutumia Pangu inakwama ikiwa imefikia percent 20 inasimama sijui tena nifanyeje@Paul S.S
 
Haya mambo ni ya kimaskini maskini sana (figuratively)! Hivi ununue iPhone $600-700 afu uanze jailbreaking uli iweje? Tz kwa ujanja ujanja duh!

Kushusha hadhi ya apple, we ukitaka hizo kitu nunua tecno, huwawei & the like.

Yaani umeongea ukweli mtupu, mi nashangaa haya mambo sijui ya kuroot au Jailbreak..ni vijitabia vya kimaskini tuu..
 

Naona faida inayopata ni Whatsapp plus tu; nyingine umeshindwa kuorodhesha.
 
faita ni nyingiv kama unavyoona ukiroot simu kwenye android kumodify system kwa kuweka theme na apps zingine mfano huwezi kuweka whatsapp kwenye tablet (ipad) njia rahisi ni kujail break pia kupata apps ambazo ni expersive au kubypass restricted things mfano mobile network hotspot pia kusaidi hata kama umesahau apple id na unataka kutoa unaweza kama uli jailbreak simu yako au device yako
 
Naona faida inayopata ni Whatsapp plus tu; nyingine umeshindwa kuorodhesha.
Mbona nimeorodhesha faida nyingi au wewe unashindwa kusoma, au itakuwa hukusoma thread yote maana kuna sehemu nimeorodhesha mambo mengi
!. Unaweza geuza part ya memory yako ukaitumia kama Flash
2. Easy ku unlock carrier lock yako bila kutumia IME
3. Unaweza funga individual application kama hutaki kufunga whole device
4. Unaweza tengeneza user account zaidi ya moja kitu ambach iphone haina windows na android tayari kipo
5. Ios 7 kurudi chini unaweza weka feature ya messege delivery report.
6. Unaweza weka selection kati ya 2g na 3g ukawa una switch to either of the two ili ku control battery drainage ya simu yako maana kuanzia ios 8 iohone haina hii selection
7. unaweza weka patches za ku fix USSD code kwa wale wanaopata tatizo la carrier unlock kwa simu wengine uwa wakisha unlock wanakumbana na hili tatizo simu inakuwa hai support USSD codes
8. Kwa wapenda games kuna patches ambazo zitamfanya mchezaji awe na ela ya kununua chochote kwenye game lolote wakati anacheza badala ya kulipia kutoka kwenye bank account yako
9. Unaweza set browser yoyote kuwa default browser sio lazima iwe safari kama inavyokuwa. unaweza set bolt, opera, google chrome etc
10. Kwa wanaopenda customization ikiwemo ringtones, themes na kadhalika wanaweza fanya hili pia.

Ni mengi tu unayoweza kufanya inategemea na mtu mwenyewe nini anataka ongeza kwenye simu yake hapo hiyo whatsapp plus sijaitaja maana mwenyewe siitumii, naitumia official whatsapp ya iphone ila nime add web enabler so naweza pia tumia whatsapp web kitu ambazo ios officially hakijafika mpaka sasa symbian, windows, blackberry na android washaanza tumia.
 
Yaani umeongea ukweli mtupu, mi nashangaa haya mambo sijui ya kuroot au Jailbreak..ni vijitabia vya kimaskini tuu..

Inaelekea mnaongea bila hata kujua nini hasa maana ya kujailbreak na kwanini watu wanajailbreak simu.
Unakuta ios inakoaa features flani ambazo wewe unahitaji, laiti zingekuwa zauzwa ungenunua lakini hata haziuzwi huna optional zaidi ya kujail break.
Sasa hapo umaskini uko wapi?
Fanya vyovyote huwezi pata msg deliverly report kwenye ios bila kujailbreak. Mfano huo tu una uhusiano gani na umaskini?
 

Sisi wengine ni washamba wa simu.nini maana ya jailbreak, na hatua zipi unazifuata ktk jailbreak?
 
Sisi wengine ni washamba wa simu.nini maana ya jailbreak, na hatua zipi unazifuata ktk jailbreak?

Kujailbreak ni kuondoa restriction kwenye ios ili kuondoa limitation za kufanya baadhi ya mambo ambazo zimewekwa kwenye device husika na watengenezaji.
Kila version ya ios ina njia yake ya kuijalbreak mkuu ila sikushauri kujailbreak simu yake unless unajua unajailbreak ili kufanya nini
 
Yaani umeongea ukweli mtupu, mi nashangaa haya mambo sijui ya kuroot au Jailbreak..ni vijitabia vya kimaskini tuu..

Hujui ulisemalo
Labda kama umasiki umepata tafsiri mpya
 
Naona faida inayopata ni Whatsapp plus tu; nyingine umeshindwa kuorodhesha.

Mkuu unaweza kudowload/upload chochote kwenye safari browser ya simu yako?

Unaweza ku attach na kusend any kind of file kwa email?

Unaweza kumtumia mtu asiyetumia bidhaa za Apple file kwa bluetooth?

Unaweza kudownload video za youtube

Unaweza ku enable/disable wifi, data, bluetooth, in a single click badala ya settings etc etc etc

Unaweza kudownload chochote kwenye safari na kukiingiza kwenye app husika? Mfano mp3 zikaingia library vitabu ibook, video kwenye video nk bila itune?

Umaweza kuhamisha au kuingiza chochote kwenye simu yako kwa pc bila itune?

Unaweza kubadili font, theme,colour, icon nk?

Unaweza kudownload file la ukubwa wa mb100 bila wifi?

Unaweza kuifanya iphone yako kuwa kama usb flash ukatumza chochote?

Unaweza ku lock app uitakayo kwa passcode?

Kuna whatsap plus, viber plus, na Fb plus inayokupa features kibao ikiwemo huitaji kuinstall fb massenger

Kuna security apps nzuri zaidi za kupata simu yako iwapo itaibiwa au kupotea kuliko zilizopo App store

Kuna vitu kama delivery report kwa sms, kupiga simu kwa video bila wifi nk

Kuna apps mbadala nyingi sana ambazo Apple wamezikataa kwenge store yao utazipata cydia kwasababu ya ukirimba wao

Mambo ni mengi sana utapata iwapo utajailbrake idevice yako kulingana na mahitaji na interest zako

Haya mambo haya husiano na umasikini bali ni sera za Apple tu
 
Mkuu kuna tweak ya CCtoggle sijui kwanini Apple hawaiweki tukachagua vitu tunataka hadi niende setting etc etc etc

Au kutulazimisha faili la ukubwa kuanzia mb100 lazima udownload kwa wifi

Kuinyima safari browser uwezo wa kudownload au ku upload chochote

Au kuamua ku switch 2g au 3g
Au kilimit aina fulani tu ya mafaili ndio unaweza kuattach kutuma email

Huwezi kutuma video, music vitabu nk kwa whatsap
Wala email
Labda kama vipo camera roll
 
pia unaweza kutumia simu ambayo iko network locked bila ya kuunlock alimradi uwe umejail break so inafaida nyingi
 

Hata mimi nashangaa kwanini wasi adapt vitu vizuri vilivyoko cydia sielewi and i am sure wanaona
 
Nunua simu inayotoa hiyo delivery report, tatizo watu kabla ya kununua simu huwa hamuangalii mnahitaji nini kwenye simu ndio mwishowe mnaishia kujailbreak na kuroot!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ