Introducing ESE Dictionary – “Kamusi”


Mkuu Nyasiro kwanza nikushukuru sana kwa msaada wko mkubwa, mimi nimefanikiwa bila shida baada ya kuweka off windw firewall na antivirus kwa muda, nakushukuru sana, kwani kutumia ile ya tuki ni usumbufu sana mpaka kupata neno lako unalotaka kwenda mbele na kurudi nyuma unatumia muda mwingi sana,
Ckufikiri kuwa kuna watanzania wanaweza kufanya hicho kitu,nimeguswa sana nakuahidi ntakaporudi dar es salaam ntakuchangia bila shida,
Napenda kuuliza nilipokuwa natumia tu kwa mara ya kwanza ikaniambia kuwa kuna toleo jipya kama napenda ku-install, kwa kuwa haikuwepo kwenye maelezo yako nikaogopa kukubali, hii unaizungumziaje ?
 
Wakashina
Asante kwa kudownload na kutumia hii kamusi.

Kwa kawaida ukiona unakuwa notified kuwa kuna toleo jipya basi inakubidi kudownload wala usiwe na shaka kabisa. Lakini kuna tatizo la kiufundi limetokea ambapo unaambiwa kuna toleo jipya hata kama halipo. Hii inatokana na instruction zenye makosa ambazo zinaangalia kama kuna toleo jipya automatically unapokuwa connected. Tatizo hili nitalirekebisha muda si mrefu katika toleo lijalo.

Kwa sasa njia sahihi ya kujua kama kuna toleo jipya ni kupitia kwenye kipengele cha About ----> Update

Tafadhali kama unakumbana na shida yoyote nijilushe.
 

nimeingia tena imenipa hiyo option , nimesema yes imenipeleka kwenye hii page ESE Dictionary | Nyasiro Software ila sidhani kama ni updates kama inavyosema yenyewe, ila hili c tatizo sana Nyasiro nafikiri next time utalirekebisha tu, halisababishi usumbufu kiasi hicho, kwa sababu ni swala tu lakusema No basi unaendelea na shughuli zako kama kawaida, kama ntapata shida tofauti sitasita kukutaarifu kwa maboresho zaidi
AKHSANTE
 
Wakashina hata kwangu napata shida hiyo. Ntarekebisha kwenye toleo lijalo usijali kabisa.
 
Nyasiro
haina shida mkuu na wala haisumbui sana, we fanya tu taratibu ili tupate kitu cha uhakika
 
Last edited by a moderator:
Jamani kuna mtu ananifanyia uhuni kwenye site yangu. Hii ni mara ya pili inakuwa hacked!

CC Donn, C6

Sasa angalia watu wanashindwa kudownload my programs. Msaada jamani.
 
Last edited by a moderator:
Jamani kuna mtu ananifanyia uhuni kwenye site yangu. Hii ni mara ya pili inakuwa hacked!

CC Donn, C6

Sasa angalia watu wanashindwa kudownload my programs. Msaada jamani.

Dah, huyu jamaa.... Ngoja nilicheki mkuu, uko online?
 
Last edited by a moderator:
nimeshaipata..kwa marekebisho madogo madogo... ungeweza kutuwekea jinsi ya kutamka maneno (phonology) ili kuwajali wasioweza kusikia vizuri. nikupongeze kwa kazi nzuri uliyoifanya. Mungu akubariki
 
Nice work, nasubiria version ya Linux

Asante mkuu.

nimeshaipata..kwa marekebisho madogo madogo... ungeweza kutuwekea jinsi ya kutamka maneno (phonology) ili kuwajali wasioweza kusikia vizuri. nikupongeze kwa kazi nzuri uliyoifanya. Mungu akubariki

Unaposema niweke jinsi ya kutamka maneno(phonology) una maana gani?
Unamaanisha transcription(text-based) au pronunciation(audio)?

Matamshi(audio) yapo kwa lugha ya kingereza. Ila kiswahili sijaweka kwa sababu Windows TTS haitamki vyema maneno ya kiswahili.
 
kwa lugha ya kiingereza ndo maana nimeandika ili kuwajali wasioweza kusikia vizuri
 
kuwajali wasioweza kusikia vizuri.....audio haitoshi..unaweza kuona zile dictionary kama oxford nk...zina jinsi ya kutamka pia kuna audio
 

Nakutana na hali hii!
 

Attachments

  • Capture.PNG
    13.2 KB · Views: 75
kuna na matatizo ya kiufundi kwenye website ya Nyasiro. hivyo download link ikawa haipo hewani kwa muda. Tatizo linashughulikiwa.

Shukran! Nasubiri.

Sent from my GT-I9192 using Tapatalk
 
Last edited by a moderator:
Kuna shida imetokea na inafanyiwa kazi. Nadhani kabla ya mwezi wa 3 ntatoa update kwa hyo naomba kama kuna feature unapenda iwepo basi uiweke mapema ili tupate kitu bora zaidi.
 
kuwajali wasioweza kusikia vizuri.....audio haitoshi..unaweza kuona zile dictionary kama oxford nk...zina jinsi ya kutamka pia kuna audio

Mh! nimekupata lakini kwa kingereza itakuwa ngumu sana kwa sababu sauti za kingereza ni complicated sana. Kingereza kina irabu zaidi ya 5 (ukiweka ma dipthong na monothong) na kina konsonanti nyingi sana kuliko kiswahili. kwa hiyo sidhani kama ntaiweka hii kitu. Lakini kwa kiswahili inakuwa rahisi kidogo na ntaona kama ntaiweka hii feature.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…