International Friendly - Namibia vs Tanzania

International Friendly - Namibia vs Tanzania

engmtolera

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
5,149
Reaction score
1,441
kwa wapenda soka mnaweza angalia mechi kupitia hii link hapa.
mechi itaanza saa mbili kamili usiku kwa saa za Tanzania,unaweza kufuatilia hii link ili kuelewa zaidi
tvall-soccer.com/livestream/match/369600/Namibia-vs-Tanzania
stars.jpg


Leo Tanzania inacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia, hizi ni mechi zipo ktk ratiba ya FIFA, timu hii imekwenda Namibia na Salum Madadi ambaye ni kaimu mkurugenzi wa ufundi wa TFF ameteuliwa pia kuwa kaimu kocha wa Taifa Stars. Alishawahi kuifundisha Taifa Stars na pia kuwa kocha mkuu wa Simba miaka ya nyuma.na ana leseni ya juu ya CAF.
Na timu hii imefanikiwa kufanya mazoezi siku moja tu.
Tunaelewa ktk soka kuna matokeo matatu yanaweza kutokea, kufungwa, kushinda ama kutoa sare
Niwatakie kila lenye jema Taifa star's

======================

FT

Namibia 1 - 1 Tanzania


 
Leo Tanzania inacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia, hizi ni mechi zipo ktk ratiba ya FIFA, lakini cha kushangaza ni kwamva timu hii ya taifa ya Tanzania imekwenda Namibia bila hata kuwa na kocha wa kueleweka.
Tunaelewa ktk soka kuna matokeo matatu yanaweza kutokea, kufungwa, kushinda ama kutoa sare
Niwatakie kila lenye jema Taifa star's
Kocha wa kueleweka ndio nini? Unafuatilia mpira wa Tanzania kweli ama ni mtumwa wa EPL? Humjui Salum Madadi!
 
Kocha wa kueleweka ndio nini? Unafuatilia mpira wa Tanzania kweli ama ni mtumwa wa EPL? Humjui Salum Madadi!

Salum madadi ndio kocha wa taifa kwa sasa? Ameajiliwa kama kocha ama ni mfanyakazi wa TFF?
 
Mbona hili suala la kawaida kbs duniani...au hujui suala la carataker manager o coach.
 
Mkuu Jamal Malinzi, hivi ilikuaje hadi TFF ikateua wachezaji wa timu ya Taifa, ikaomba mechi kwa mujibu wa kalenda ya FIFA pasipo kuwa na kocha au maandalizi yoyote?

Kuna ulazima gani wa kucheza mechi hizi ikiwa hakuna kocha wa kuwapima wachezaji anaowataka?

Au ndio kusema kaka Madadi ndiye mrithi wa Poulsen kwa sasa?
 
Last edited by a moderator:
Kocha wa kueleweka ndio nini? Unafuatilia mpira wa Tanzania kweli ama ni mtumwa wa EPL? Humjui Salum Madadi!

Nafuatilia soka la Tanzania na ndio maana naelewa kuwa leo timu yetu inamechi ya kirafiki,tena kwa jili ya maandalizi ya kwenda MOROCCO na ndio maana nikawa na wasiwasi,kwani timu imefanya mazoezi siku moja na kocha kaachishwa kazi juzi tu na kumbuka mechi hii tukipoteza tunashuka ktk ubora wa viwango vya soka,hii si mechi ya kujaribu ni mechi muhimu sana kwetu.
pamoja na hayo,bado nina imani na timu ya Taifa na naendelea kuiombea ifanye vizuri,ingawaje nipo tayari kupokea matokeo ya aina yeyote yale
 
Mkuu Jamal Malinzi, hivi ilikuaje hadi TFF ikateua wachezaji wa timu ya Taifa, ikaomba mechi kwa mujibu wa kalenda ya FIFA pasipo kuwa na kocha au maandalizi yoyote?

Kuna ulazima gani wa kucheza mechi hizi ikiwa hakuna kocha wa kuwapima wachezaji anaowataka?

Au ndio kusema kaka Madadi ndiye mrithi wa Poulsen kwa sasa?
Mkataba wetu na wadhamini unatutaka tucheze mechi zote za kimataifa kwenye kalenda ya FIFA, tunawajibika kuuheshimu na kuzingatia mahitaji yake.

Muda wa maandalizi haukuwepo, sio tu kwa Tanzania, bali kwa nchi zote za Afrika ambazo vilabu vyao vinacheza ubingwa wa Afrika. Ndio maana Kiiza na Okwi wame-scramble kwenda Zambia kuchezea Uganda bila hata kuingia kambini, the same for South Africa wanaocheza na brazil leo. CAF wamefanya return leg ziwe za siku saba badala ya 14 kwa sababu ya World Cup, hiyo ndiyo hali halisi tuliyomo.

Mahitaji ya kisheria yalituzuia kumtumia Mwl Kim kuteua timu katikati ya mazungumzo ya kukatiza mkataba, kulikuwa na legal implications kwa mujibu wa ushauri wa kisheria tuliopewa wakati huo.

Timu iliteuliwa na mwalimu mwenye leseni ya Ukocha ya CAF leseni A (ndiyo ya juu).
 
Muda wa maandalizi haukuwepo,sio tu kwa Tanzania,bali kwa nchi zote za Afrika ambazo vilabu vyao vinacheza ubingwa wa Afrika.
Ndio maana Kiiza na Okwi wame scramble kwenda Zambia kuchezea Uganda bila hata kuingia kambini,the same for south africa wanaocheza na brazil leo.

Mkuu hapa kwenye maandalizi kidogo nashindwa kukuelewa una maana gani...

TFF ilishatambua uwepo wa mechi hii muda mrefu kidogo kama miezi miwili iliyopita...

Kwa mujibu wa mtandao wa TFF, taarifa ya mechi hii ilitolewa tarehe 14 mwezi Januari...

Taifa Stars Kuikabili Namibia FIFA Date Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia

Pia kwa mujibu wa taarifa hiyo programu ya maandilizi ya mechi hii tayari mlishaiacha mikononi mwa Poulsen...

Sasa kwa nini msingelisubiri hadi mechi hii ipite kwanza ndipo msitishe mkataba na Kim kwa maslahi ya nafasi ya nchi katika viwango vya FIFA?

CAF wamefanya return leg ziwe za siku saba badala ya 14 kwa sababu ya world cup,hiyo ndiyo hali halisi tuliyomo.

Ushiriki wa Yanga katika michuano ya klabu bingwa ulishajulikana tangu awali ikiwemo ratiba ya mechi ya kwanza na ya pili...

Kwa nini basi kikosi kisingeliteuliwa tangu awali kwa kuwa tayari inajulikana wachezaji wa Yanga hawatoweza kupata nafasi?

Mkuu mimi nadhani kutakuwa na sababu nyingine lakini sio hii, huenda mlifanya haraka kidogo kusitisha kibarua cha Kim na mkasahau kuwa kuna mechi hii muhimu...
 
watu8

Mazungumzo na Kim, labda wewe unisaidie, yalianza lini? Na kwa mujibu wa kalenda ya vodacom premier league na ligi daraja la kwanza, hiyo timu ingekuwa assembled lini?
 
Last edited by a moderator:
Mazungumzo na Kim,labda wewe unisaidie,yalianza lini? Na kwa mujibu wa kalenda ya vodacom premier league na ligi daraja la kwanza,hiyo timu ingekuwa assembled lini?

Mkuu ukiifuatilia link hii hapa chini inaonesha kuwa TFF ilishamuelekeza Kim afanye maandalizi ya mechi ya leo...

allAfrica.com: Tanzania: Stars Face Namibia On Fifa Date

Wambura said they have already informed Taifa Stars coach Kim Poulsen about the issue so that he can now start preparing his programmes.

Ndio maana nauliza kwa nini basi msingelisubiria hadi mechi hii ambayo ni muhimu kwa viwango vya FIFA ipite kwanza, ndiposa mfanye mchakato wa kuvunja mkataba na Bw. Poulsen.
 
Rainford Kalaba yuko ndani ya kikosi cha Zambia dhidi ya Uganda,Emma Okwi,Hamis Kiiza yuko ndani ya kikosi cha Uganda dhidi ya zambia leo.Kwanini Tanzania haina Ulimwengu na Samatta dhidi ya Namibia?
 
Rainford Kalaba yuko ndani ya kikosi cha Zambia dhidi ya Uganda,Emma Okwi,Hamis Kiiza yuko ndani ya kikosi cha Uganda dhidi ya zambia leo.Kwanini Tanzania haina Ulimwengu na Samatta dhidi ya Namibia?

Wanaogopa kuvunjika, watz hatutambui umuhimu wa mechi za kirafiki ndio maana wameamua club kwanza taifa baadae.
 
Mtu anachaguliwa kuwa Rais TFF anabadili mambo atakavyo kama mwanasiasa afanyavyo.Kocha stahiki wa Stars mbadala wa Kim ni yule aliyekuwa akimsaidia kwa karibu miaka 4 sasa Mr... (Nimesahau jina) ndiye amechukua ujuzi na anawajua wachezaji wetu vizuri sa huyu Madadi wa nini?
 
Wanaogopa kuvunjika, watz hatutambui umuhimu wa mechi za kirafiki ndio maana wameamua club kwanza taifa baadae.

Lakini kumbuka timu ya Taifa haiwezi kuwa bora kama vilabu husika vinaendesha soka kiujanja ujanja,timu ya Taifa ikiwa nzuri inavutia kucheza na timu kubwa na hii inawapa nafasi wachezaji wetu kwenda kucheza nje ya Tanzania
 
kwa wapenda soka mnaweza angalia mechi kupitia hii link hapa
Namibia vs Tanzania.Live.Stream.Free - Imgur
Namibia vs Tanzania.Live.Stream.Free - Imgur
mechi itaanza saa mbili kamili usiku kwa saa za Tanzania,unaweza kufuatilia hii link ili kuelewa zaidi
Namibia vs Tanzania - International Friendly 2014-03-05 Live Streaming - Online Football TV
stars.jpg

Leo Tanzania inacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia, hizi ni mechi zipo ktk ratiba ya FIFA, timu hii imekwenda Namibia na Salum Madadi ambaye ni kaimu mkurugenzi wa ufundi wa TFF ameteuliwa pia kuwa kaimu kocha wa Taifa Stars. Alishawahi kuifundisha Taifa Stars na pia kuwa kocha mkuu wa Simba miaka ya nyuma.na ana leseni ya juu ya CAF.
Na timu hii imefanikiwa kufanya mazoezi siku moja tu.
Tunaelewa ktk soka kuna matokeo matatu yanaweza kutokea, kufungwa, kushinda ama kutoa sare
Niwatakie kila lenye jema Taifa star's

mungu ibariki Tanzania
mungu ibariki Taifa Stars
 
mungu ibariki Tanzania
mungu ibariki Taifa Stars

pamoja na magumu tunayopitia,tuendelee kuisapoti timu
mpaka sasa

Iraq 2 vs China 0,mechi ni mapunziko sasa hivi
Iraq pamoja na vita na mabomu ya kila lakini wanacheza soka la hali ya juu,hii inatokana na maandalizi mazuri ya timu bila kujari nchi ipo ktk mazingira gani
 
Back
Top Bottom