Intel duo core na intel pentium!!

Richbest

Senior Member
May 23, 2011
101
24
Habari wapendwa! Naomba mnisaidie tofauti na faida/hasara za kila moja hapo juu!
 
Pentium ni ya zamani sana na juzi Intel wametangaza kui-phase out.
Dual core ilikuwa improved version ya Pentium ila nayo ikawa upgraded na nafasi yake imechukuliwa na Core2duo.
Ila ni bora uende na processor za kisasa zaidi yaani Intel Core i3, Core i5 na kama uchumi unaruhusu Core i7
 
Hili nilishawahi kulielezea hapo zamani:

NYONGEZA: Pentium zilikuwa ni Processor 1 inafanya kazi kwenye Computer kama CPU. Baadaye wakaja na CoreDUAL ambazo ndani zilikuwa ni Processor Pacha. Baadaye wakaja na Core2Dual ambazo zinakuwa ni Processor pacha mbili. Ila hizi zote zinakuwa zinafanya kazi pamoja kila kukitokea kazi ya kufanya. Sasa hivi wamekuja na hizo mkuu kaandika hapo zenye Alama ya i3, i5 au i7. Hizi nazo zina procssor nyingi ndani ila zinafanya kazi kidogo tofauti na hizo Core Dual. Maelezo yake ndiyo haya hapa chini:>>>>

Hizi Processor zinafanya kazi kwa maelezo mazuri ni kama yale maroli yenye matairi mengi na kama halina mzigo mkubwa au halina kabisa, linanyenyua baadhi ya matairi juu na yanakuwa hayakanyagi chini/kutumika. Mzigo ukiwa mkubwa basi yanashushwa ili kusaidia yale mengine na wakati huohuo kuugawanya mzigo kwenye matairi mengi ili gari lisiharibu barabara kwa uzito.

Hizo processor nazo huwa ndani ziko nyingi na kama kuna kazi kidogo, bazi zinafanya kazi chache tu au moja na nyingine zinapumzika na hivyo ku-Save energy. Kama kazi zikiongezeka, basi inaongeza na processor zaidi kufanya kazi. Ila zote zimefungiwa ndani ya CPU moja na zinafanya kazi moja, mbili.... zote.

https://www.jamiiforums.com/tech-gadgets-and-science-forum/161436-vijana-wa-ma-kompyuta.html
 
Habari wapendwa! Naomba mnisaidie tofauti na faida/hasara za kila moja hapo juu!
Duo ni family processor yenye Core(cpu) mbili kwenye chip moja.inaweza kuwa ni Intel au AMD au chip maker yeyote Kwa hiyo

Dual Core= Ndani ya proccessor chip moja kuna CPU mbili
Intel Petium= Ni kampuni mojawapo inayotengeza chip za prccessor. Pentium nimoja ya product famlly zao za mwazo amabzo archtecture yake ni kiyume cha Duo. CPU moja ndani ya proccessor moja.

Ebu Soma maelezo ya mtalaaam huyu wakati unasubiri majibu ya wataalam wengine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom