mzenjiboy
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 907
- 385
India wamebuni utaratibu mpya wa kuomba visa ya nchi hiyo. Itakuwa kwa njia ya mtandao badala ya mtu kwenda ubalozini pale nchini mwake. Utaratibu huu umebuniwa ili kuwarahishia watalii pamoja na wageni wengine wanaokwenda nchi hiyo.
Baada ya kutuma maombi yako kwa njia ya mtandao huchukua kama siku nne ili kupata jawabu, ikiwa umekubaliwa basi unasafiri na visa yako utaikuta kiwanja cha ndege huko India.
Ni nchi 43 ndizo zitazofaidika na utaratibu huu mpya lakini katika orodha ya nchi hizo 43 TANZANIA haimo lakini majirani wa TZ, Kenya wao wamo.
Baada ya kutuma maombi yako kwa njia ya mtandao huchukua kama siku nne ili kupata jawabu, ikiwa umekubaliwa basi unasafiri na visa yako utaikuta kiwanja cha ndege huko India.
Ni nchi 43 ndizo zitazofaidika na utaratibu huu mpya lakini katika orodha ya nchi hizo 43 TANZANIA haimo lakini majirani wa TZ, Kenya wao wamo.