India kutumika electronic visa

mzenjiboy

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
907
385
India wamebuni utaratibu mpya wa kuomba visa ya nchi hiyo. Itakuwa kwa njia ya mtandao badala ya mtu kwenda ubalozini pale nchini mwake. Utaratibu huu umebuniwa ili kuwarahishia watalii pamoja na wageni wengine wanaokwenda nchi hiyo.

Baada ya kutuma maombi yako kwa njia ya mtandao huchukua kama siku nne ili kupata jawabu, ikiwa umekubaliwa basi unasafiri na visa yako utaikuta kiwanja cha ndege huko India.

Ni nchi 43 ndizo zitazofaidika na utaratibu huu mpya lakini katika orodha ya nchi hizo 43 TANZANIA haimo lakini majirani wa TZ, Kenya wao wamo.
 
Sasa umuhimu wa uzi wako u wapi kama hatuna faida na mfumo huo???
 
Yule jamaa aliyetupiga mabilion ni mhindi,nawachukia hawa wadosi kupita maelezo.....pambavu zao.
 
Watu 8 inaonesha TZ inaanza kutengwa kutokana na kashfa zisokwisha.
 
ID hatuna, payment system magumashi, address zenye mitaa na namba za nyumba pia hatuna. Online bado hatuna mipango nazo.
 
Back
Top Bottom