Inaniuma sana

mtengwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2011
Posts
1,603
Reaction score
871
Hayanihusu moja kwa moja ila inaniuma kwa kweli. Nina rafiki yangu ana girlfriend wake ambae dada huyo anampenda sana rafiki yangu na anafanya kila analoweza kumfurahisha jamaa. Rafiki yangu ni kicheche ana wasichana wasiohesabika anabadili kila leo japo anampenda huyu mdada kuliko wanawake wake wote. Huyu mdada she is wife material kabisa kimuonekano hata kitabia, natamani rafiki yangu amuoe lakini kwa upande wa pili tabia za jamaa naona either atakuja kumuumiza mdada akijua jamaa kicheche au atamuambukiza STD's. Naumia sana nikiwaza maisha ya mdada baadae. Sina la kufanya maana rafiki hashauriki. Wana MMU nimsaidiaje mdada
 
Ndio huyo mkuu! Unataka nn tena?!
Dada anampenda rafiki yangu, siwezi kumuoa maana najua upendo wake kwa rafiki yangu hauishi hata wakiachana vipi, unataka nimegewe?
 
Naona ushampenda mpenzi wa rafili yako, uje utupe maendeleo desemba.
 
pilipili usio ila yakuashia nn?

Mfano akipata ukimwi dada wa watu na ukichukulia namkubali sana shem wangu. Ananiulizaga kama rafiki yangu anamcheat, anauliza kama hayuko serious me namwambiaga yuko peke yake tho najua wako wengi.
 
Kwa kumsaidia kamtambulishe kwenu kisha umlipie mahari utakuwa umemsaidia sana!
 
Mfano akipata ukimwi dada wa watu na ukichukulia namkubali sana shem wangu. Ananiulizaga kama rafiki yangu anamcheat, anauliza kama hayuko serious me namwambiaga yuko peke yake tho najua wako wengi.

Tupo wengi wenye marafiki wa hivyo ila kwakuwa ni rafiki yako mpe ukweli wake..!!
Player hubadilika na kutulia zaidi ya shabiki kipofu
 
Si kwamba nataka kumuoa hapa ila I wish kupata such kind of woman.

Mkuu hizo ni dalili za kuchepuka na demu wa mshikaji wako! Hatua moja huanzisha nyingine....
 
Tupo wengi wenye marafiki wa hivyo ila kwakuwa ni rafiki yako mpe ukweli wake..!!
Player hubadilika na kutulia zaidi ya shabiki kipofu

Tunamwambia kila siku lakini habadiliki anaona sifa kua na wengi hadi wanamuita fundi kei..
 
Chamsingi onya hiyo rafiki ako aache umalaya pori!hapo utakua umemsaidia huyo shemejiyo kpenz,ambaye hana hatia.tafakari...chukua hatua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…