Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,434
- 7,092
Naomba nitumie lugha kali kumkemea huyu Msanii mkongwe wa muziki wa B. Flava nchini, Juma Cassim Nature, maana naona wasanii wanazidi kutudharau na kutunyanyasa kwa sababu ya ubinafsi wao, shenzy kabisa!
Mwanamuziki/Msanii yeyote ni kama nabii, ni kama mteule au mpakwa mafuta kwa sababu moja kuu; Ana ufuasi mkubwa sana unaomfuatilia.
Sasa mtu wa aina hii, ni lazima ajue anabeba hisia, matarajio na mioyo ya watu wengi. Kwahiyo anapaswa kujua kwamba anabeba maumivu, furaha, hasira, na faraja za watu wengi sana. Hana budi kuheshimu hilo na kuwa makini kwa kila akifanyacho; hususani kwenye kile kilichompa wafuasi wengi..
Kufanya kazi nzuri, sio hiari, ni lazima. Kwa sababu hufanyi kwa ajili yako tu, bali kwa ajili ya wanaonunua kazi yako. Ni dharau ya hali ya juu kufanya kile unachojisikia kwa vile tu unapendwa!
To cut the story short, Juma Nature ame-release RMX ya wimbo wake wa kihistoria, wimbo uliobeba kumbukumbu za maisha ya miaka ya nyuma ya watanzania wengi, wimbo unaowakumbusha watu mambo flani flani kwenye maisha kila wausikiapo. Wimbo wenye heshima na unaokumbukwa zaidi kwa muda mrefu sasa. INANIUMA SANA!
INANIUMA SANA ni wimbo wenye 'emotional value', ambayo pengine Nature ameamua kuichezea na kuipuuza. Ameifanyia Remix kwa mtindo wa 'kigodoro' kwa kumshirikisha Msaga Sumu, mtindo wa kisasa, mtindo ambao unaendana na nyakati zilizopo, Old wine in a new bottle..
Si dhambi, lakini je kuna haja ya kufanya hivyo?
Alichokifanya ni 'Value Assassination' ya huu wimbo bila kujua. Ni nani aliyemshauri hata kuthubutu kufanya hivi? Ni nini kimemsukuma kufanya huu ujinga? Watu wengine sijui wakoje!!!
Anatafuta namna ya kurudi? Kwani kwenye muziki hakuna kustaafu? Hivi hakuna namna ya kumfanya msanii akapumzika kutumikia kufanya alichokifanya kwa muda mrefu ili asiharibu reputation yake? Ninachoamini, Utendaji huenda na umri, zama na shauku ya mtendaji. Vikipita hivyo, ni kuboronga tu ndio kunakofuatia..
Kwa hili, Nachelea kusema Nature umedharau sana watu wengi, zaidi umedharau 'thamani' ya kazi yako! Ni bora ukatangaza kustaafu, ili tukuenzi kwa heshima.
Nimechukia kweli kweli!
OLD: View attachment Juma_Nature-Inaniuma_Sana.mp3
NEW: View attachment Juma_Nature-Inaniuma_Sana_RMX_Ft_Msaga_Sumu.mp3
Mwanamuziki/Msanii yeyote ni kama nabii, ni kama mteule au mpakwa mafuta kwa sababu moja kuu; Ana ufuasi mkubwa sana unaomfuatilia.
Sasa mtu wa aina hii, ni lazima ajue anabeba hisia, matarajio na mioyo ya watu wengi. Kwahiyo anapaswa kujua kwamba anabeba maumivu, furaha, hasira, na faraja za watu wengi sana. Hana budi kuheshimu hilo na kuwa makini kwa kila akifanyacho; hususani kwenye kile kilichompa wafuasi wengi..
Kufanya kazi nzuri, sio hiari, ni lazima. Kwa sababu hufanyi kwa ajili yako tu, bali kwa ajili ya wanaonunua kazi yako. Ni dharau ya hali ya juu kufanya kile unachojisikia kwa vile tu unapendwa!
To cut the story short, Juma Nature ame-release RMX ya wimbo wake wa kihistoria, wimbo uliobeba kumbukumbu za maisha ya miaka ya nyuma ya watanzania wengi, wimbo unaowakumbusha watu mambo flani flani kwenye maisha kila wausikiapo. Wimbo wenye heshima na unaokumbukwa zaidi kwa muda mrefu sasa. INANIUMA SANA!
INANIUMA SANA ni wimbo wenye 'emotional value', ambayo pengine Nature ameamua kuichezea na kuipuuza. Ameifanyia Remix kwa mtindo wa 'kigodoro' kwa kumshirikisha Msaga Sumu, mtindo wa kisasa, mtindo ambao unaendana na nyakati zilizopo, Old wine in a new bottle..
Si dhambi, lakini je kuna haja ya kufanya hivyo?
Alichokifanya ni 'Value Assassination' ya huu wimbo bila kujua. Ni nani aliyemshauri hata kuthubutu kufanya hivi? Ni nini kimemsukuma kufanya huu ujinga? Watu wengine sijui wakoje!!!
Anatafuta namna ya kurudi? Kwani kwenye muziki hakuna kustaafu? Hivi hakuna namna ya kumfanya msanii akapumzika kutumikia kufanya alichokifanya kwa muda mrefu ili asiharibu reputation yake? Ninachoamini, Utendaji huenda na umri, zama na shauku ya mtendaji. Vikipita hivyo, ni kuboronga tu ndio kunakofuatia..
Kwa hili, Nachelea kusema Nature umedharau sana watu wengi, zaidi umedharau 'thamani' ya kazi yako! Ni bora ukatangaza kustaafu, ili tukuenzi kwa heshima.
Nimechukia kweli kweli!
OLD: View attachment Juma_Nature-Inaniuma_Sana.mp3
NEW: View attachment Juma_Nature-Inaniuma_Sana_RMX_Ft_Msaga_Sumu.mp3