Inaniuma sana: Juma Nature Kwanini usiache kama huwezi?

Inaniuma sana: Juma Nature Kwanini usiache kama huwezi?

Hii ni remix ya ngapi sasa? Maana hata huo ulioufanyia utofauti ni remix pia.
 
INANIUMA SANA ni wimbo wenye 'emotional value', ambayo pengine Nature ameamua kuichezea na kuipuuza. Ameifanyia Remix kwa mtindo wa 'kigodoro' kwa kumshirikisha Msaga Sumu, mtindo wa kisasa, mtindo ambao unaendana na nyakati zilizopo, Old wine in a new bottle..
Sijui majuzi nilikutwa na nini... kwanza, nianze kutamka bayana nilikuwa sina taarifa za Kibla kufanya remix ya Inaniuma Sana...dah, yaani nipo outdated ile mbaya! Lakini uzi huu umenikumbusha kwamba last week nilijisikia hamu sana ya kuisikiliza Inaniuma Sana, tena nakumbuka nilitaka kuitafuta online lakini sijui ilikuwaje nikasahau! Kwa hakika alichoifanyia Inaniuma Sana ni unforgivable! Ile haikuwa ngoma ya kuigusa unless kama unataka kuaibika! Hivi unaigusa vipi ngoma kama, according to me, Liberian Girl na kujidai unataka kuifanyia remix kama sio unatafuta kujidhalilisha?!
 
Kiroboto uswahili umemzidi. Mimi namwona kama ni Msanii asiyependa ama asiyetaka kuwa na watu wa kumshauri. akikurupuka na bangi zake harudi nyuma.
Hebu fikiria ngoma moja aliitoa si mda mrefu sana inaitwa 'Komaa'..niliipenda sana hii ngoma kwani Kiroboto alikua amekuja kama nilivyotamani aje...style ambayo ilinikumbusha ngoma za kitambo za kiroboto....sasa si akaja akatoa video...tobaaaaaaa...aliniudhiiii..video kama imepigwa kwa tecno.
 
Back
Top Bottom