Inakuwaje ugomvi wenu wa mahusiano utatuliwe na wengine...????

ninapofikiri hapo huwa naona bora matatizo yangu nife nayo.
mhhh usifanye hivyo..... A Problem Shared is Half a Problem........ lakini inabidi tuangalie ni nani tunaongea nae na ni kweli matatizo ya wapenzi inabidi wenyewe ndio wayasolve sababu wanajua kuhusu matatizo yao kuliko mtu mwingine yoyote
 
Habari zenu wapenzi wangu wote wa MMU??
Hili jambo nimelifikiria kwa muda mrefu, na kila siku nazidi kulifikiria ila nakosa jibu. Watu wengi wanapokuwa kwenye mahusiano eg wapenzi, inapotokea wamegombana wanatafuta mtu mwingine awasuluhishe na mara nyingi huwa anafanikiwa. Swali ninalojiuliza, inakuwaje mwanamke/mwanamme haupo tayari kumsikiliza mwenzio na kumuelewa ila upo tayari kumsikiliza mtu wa pembeni? Hivi inaleta picha gani baada ya nyie kupatana baada ya kusuluhishwa na ndugu au rafiki?
Binafsi nafikiri kama mpenzi wangu hatonisikiliza mimi, sitokuwa tayari amsikilize mwingine kwa niaba yangu na kama sipo tayari kumsikiliza yeye na kutatua tatizo basi sitoweza kumsikiliza ndugu wala jamaa yake. Wewe je unaonaje?

Kweli matatizo ya kwenye ndoa inabidi yatatuliwe na wanandoa wenyewe. Lakini wakati mwingine na kulingana na tatizo lenyewe ina make sense kutafuta msaada wa mawazo toka third parties. Kwa mfano utafanyaje kama partner wako anataka ku argue saa zote badala ya kukaa chini na kujadili hilo tatizo? Would just just keep it in the relationship and stress about it or talk to other people close to you?

Kuongelea matatizo yako na mtu mwingine ni behaviour inayokubalika kama utamshirikisha friend or family member, au confidant ambaye anaweza kukupa unbiased perspective. Ndio maana watu wengine wanakuja hapa JF kutafuta ushauri juu ya matatizo kwenye ndoa. Otherwise, they should have kept it in the relationship and not seek third party opinion. Nakubali uhusiono na mwanandoa wako should be your first priority lakini wanandoa wanatofautiana sana. Kuna wanadamu humu duniani wanadhani whatever they say is right.

Tena kwa wanawake hili ni muhimu sana, b'se there are men out there who don't really care what women have to say especially if its about them. Inawezekana hapa tunaongea from urban perspective, lakini huko vijijini ndoa nyingi zinadumu kutokana na busara za wanandugu. Pia wapo wanawake wengi huwa wanapigwa sana na wanaume zao na huwa hawasemi kutokana na hii kasumba ya wanting to keep it in the relationship. Victims wa domestic violence au wale waliowahi kufanya kazi na hawa victims wataelewa nina maana gani. Na kumbuka domestic violence is not limited to physical violence.
 
Kuongelea matatizo yako na mtu mwingine ni behaviour inayokubalika kama utamshirikisha friend or family member, au confidant ambaye anaweza kukupa unbiased perspective. .
sijajua umemaanisha kuongelea kimtindo upi. Kuna wengine huongelea matatizo baada ya kuwa washayatatua (napendelea zaidi hili), wengine huongelea matatizo kwa wakati ule ambao wapo kwenye matatizo kwa nia wasaidiwe au waonewe huruma.
 
Habari zenu wapenzi wangu wote wa MMU??
Hili jambo nimelifikiria kwa muda mrefu, na kila siku nazidi kulifikiria ila nakosa jibu. Watu wengi wanapokuwa kwenye mahusiano eg wapenzi, inapotokea wamegombana wanatafuta mtu mwingine awasuluhishe na mara nyingi huwa anafanikiwa. Swali ninalojiuliza, inakuwaje mwanamke/mwanamme haupo tayari kumsikiliza mwenzio na kumuelewa ila upo tayari kumsikiliza mtu wa pembeni? Hivi inaleta picha gani baada ya nyie kupatana baada ya kusuluhishwa na ndugu au rafiki?
Binafsi nafikiri kama mpenzi wangu hatonisikiliza mimi, sitokuwa tayari amsikilize mwingine kwa niaba yangu na kama sipo tayari kumsikiliza yeye na kutatua tatizo basi sitoweza kumsikiliza ndugu wala jamaa yake. Wewe je unaonaje?

Mie tabia hii inanikera sana kusema kweli ila namshukuru Mungu katika mahusiano niliyowahi kuwa nayo hakujawahi kutokea tatizo la kumshirikisha 3rd party ili kutafuta usuluhishi wa tatizo lilikuwepo.

Kwanza naona ni kuwapa faida watu wengine wayajue matatizo yenu na si ajabu kuyatangaza kwa watu wengine na wao kuwa wanawachora tu kila wawaonapo.

Mna matatizo yenu kaeni chini hata kwa masaa, siku hata wiki ili kutafuta suluhisho kama kweli wote mna nia ya kumaliza tatizo lilikuwepo basi ni lazima tu mtafanikiwa ila kama mmoja ana ajenda zake za siri basi itakuwa ngumu sana kupata suluhisho.
 
sijajua umemaanisha kuongelea kimtindo upi. Kuna wengine huongelea matatizo baada ya kuwa washayatatua (napendelea zaidi hili), wengine huongelea matatizo kwa wakati ule ambao wapo kwenye matatizo kwa nia wasaidiwe au waonewe huruma.

Kwa hiyo kati ya hayo mawili ni lipi unazungunzia? Kuongelea tatizo baada ya kulitatua au kuongelea tatizo kabla ya kulitatua? Kama ni kuongelea tatizo baada ya kulitatua, then I can't see the point of doing that. Sidhani kama wataweza kuongelea tatizo ambalo tayari wameshalitatua, b'se hakuna tatizo hapo tena. Kama ndipo ulipobase argument yako, then tuko pamoja. Lakini kama ni kuongelea tatizo kwa wakati ule ambao upo kwenye tatizo kwa nia ya kutaka usaidiwe au uonewe huruma, then kutokana na nilivyosema kwenye post yangu ya mwanzo that is perfectly fine.
 
Fikiria hapo mnaenda kuanika madhaifu yenu kwa watu halafu baada ya hapo mnapatana, mnaanza kuambatana. Wale wasuluhishi wenu wanawatazama tu, na gumzo juu, wale usiwaone vile yule mwanaume yulo hivi na hivi yule mwanamke ndo usiseme...dah na ukishasema hayafutiki. Tumalizane humu ndani bana mzee!
 
Mie tabia hii inanikera sana kusema kweli ila namshukuru Mungu katika mahusiano niliyowahi kuwa nayo hakujawahi kutokea tatizo la kumshirikisha 3rd party ili kutafuta usuluhishi wa tatizo lilikuwepo.

Kwanza naona ni kuwapa faida watu wengine wayajue matatizo yenu na si ajabu kuyatangaza kwa watu wengine na wao kuwa wanawachora tu kila wawaonapo.

Mna matatizo yenu kaeni chini hata kwa masaa, siku hata wiki ili kutafuta suluhisho kama kweli wote mna nia ya kumaliza tatizo lilikuwepo basi ni lazima tu mtafanikiwa ila kama mmoja ana ajenda zake za siri basi itakuwa ngumu sana kupata suluhisho.

Mkuu nakubaliana na wewe lakini itakuwaje mkishindwa kupata suluhisho? Kwa kawaida kama kuna tatizo liwe or lisiwe lla kindoa tunashauriwa kukaa kukaa chini na kujaribu kulitafutia ufumbuzi. Lakini vipi mkishindwa kupata ufumbuzi? Mtaendelea kuishi na hilo tatizo au mtatafuta msaada toka sehemu nyingine? Kuna watu wengi tuu wamekuja hapa JF wakitaka ushauri wa matatizo ya ndoa. Na ukisoma posts za watu wengi wamekuwa wakiwashauri hawa watu wajaribu kuwashirikisha sijui wazazi wa pande zote mbili, kiongozi wa dini, waende counselling, nk. Nafikiri whether or not kuwashikisha third parties kwenye kutatua matatizo ya kindoa inategemea na wanandoa wenyewe, aina ya tatizo, nature na content ya ndoa yao, na connection na third parties wenyewe. Nakubali sio vizuri kutangaza kwa watu wengine matatizo yako, but I will never advise any person to keep a problem to themselves especially pale wanaposhindwa kuyatatua wao wenyewe.
 
Kwa hiyo kati ya hayo mawili ni lipi unazungunzia? Kuongelea tatizo baada ya kulitatua au kuongelea tatizo kabla ya kulitatua? Kama ni kuongelea tatizo baada ya kulitatua, then I can't see the point of doing that. Sidhani kama wataweza kuongelea tatizo ambalo tayari wameshalitatua, b'se hakuna tatizo hapo tena. Kama ndipo ulipobase argument yako, then tuko pamoja. Lakini kama ni kuongelea tatizo kwa wakati ule ambao upo kwenye tatizo kwa nia ya kutaka usaidiwe au uonewe huruma, then kutokana na nilivyosema kwenye post yangu ya mwanzo that is perfectly fine.
mkuu namaanisha kuongelea tatizo ili uonewe huruma na utatuliwe, mfano mmegombana mnatafuta mtu awasuluhishe, hiyo sikubali nayo na hata wadau hapo chini wamechangia vizuri tu ubaya wa kuwaambia watu matatizo yako. Binafsi nahisi ni bora kama unapenda watu wayajue matatizo yako, waambie wakati ushayatatua. Hapo itaonyesha pia ni vipi upo imara. Kama mdau mmoja alivyocomment hapo chini kuwa wengine hufurahi kuona wenzao wapo kwenye matatizo, wengine wana matatizo zaidi yako na wengine hawapendi kusikiliza matatizo ya watu. Matatizo yetu tutafte namna ya kuyatatua wenyewe.
 
Fikiria hapo mnaenda kuanika madhaifu yenu kwa watu halafu baada ya hapo mnapatana, mnaanza kuambatana. Wale wasuluhishi wenu wanawatazama tu, na gumzo juu, wale usiwaone vile yule mwanaume yulo hivi na hivi yule mwanamke ndo usiseme...dah na ukishasema hayafutiki. Tumalizane humu ndani bana mzee!

LD tatizo unafikiri tatizo linaweza tuu kutatuliwa na wahusika. Mbona kungekuwa na raha sana duniani. Unfortunately, it does not work like that. Sawa tuyamalise matito yetu humo humo ndani. Utafanyeje kama mkishindwa kumalizana? Utaendelea kuishi na tatizo kwa sababu unataka watu wengine wasijue tatizo lako?
 
mkuu namaanisha kuongelea tatizo ili uonewe huruma na utatuliwe, mfano mmegombana mnatafuta mtu awasuluhishe, hiyo sikubali nayo na hata wadau hapo chini wamechangia vizuri tu ubaya wa kuwaambia watu matatizo yako. Binafsi nahisi ni bora kama unapenda watu wayajue matatizo yako, waambie wakati ushayatatua. Hapo itaonyesha pia ni vipi upo imara. Kama mdau mmoja alivyocomment hapo chini kuwa wengine hufurahi kuona wenzao wapo kwenye matatizo, wengine wana matatizo zaidi yako na wengine hawapendi kusikiliza matatizo ya watu. Matatizo yetu tutafte namna ya kuyatatua wenyewe.

In short kuna makundi mawaili ya watu. Kundi la kwanza ni la wanandoa ambao hawatasema chochose about their unhappiness kwenye ndoa zao. They go with the flow hoping something will change and they will solve their problems by themselves. Kama hili likishindikana ni heri waachane kabisa kuliko kushirikisha third parties. Kundi la pili ni la wanandoa ambao watatumia kila njia kujaribu kutatua matatizo yao. They will try everything in their disposal to make the marriage work before making a final decision to end the marriage.

Tofauti ya haya makundi ni kuwa, kundi la kwanza sio problem solvers. Either they solve the problem by themselves lakini wakishindwa, that is the end of it. Heri kuendelea kuishi na tatizo au kuvunja ndoa badala ya kutafuta assiatance nje ya ndoa. Kundi la pili ni problem solvers who feel they owe it to the marriage to try to find solutions to the problems before they throw in the towel. They will try every means available to solve the problem.

Mkuu na wengine wengi waliochangia mpo kwenye kundi la kwanza. Mnaamini kwenye ile theorectical assumptions kuwa matatizo yote kwenye ndoa yanaweza kutatuliwa na wanandoa wenyewe bila kuhusisha third parties. Mimi niko kwenye kundi la pili. Naamini kuwa, japokuwa matatizo ya kwenye ndoa inabidi yatatuliwe na wanandoa wenyewe, this theoretical assumption can be refutable in practice. Siyo matatizo yote ya kindoa yanayoweza kutatuliwa na wanandoa wenyewe. Kuna matatizo mengine wanandoa watahitaji third party intervention ili yatatuliwe. Kwa maneno mengine kwa vile ndoa, wanandoa na matatizo ya ndoa yanatofautiana from one marriage to another, how to address those problems may also vary.

The fact kuwa unaimiliki au unaijua ndoa yako ndani na nje haina maana kuwa utaweza kusolve matatizo yote kwenye hiyo ndoa. Kumbuka family is an institution kama institutions nyingine kama kampuni. Inakumbwa na matatizo ambayo mengine yaweza kutatuliwa humo humo ndani. Lakini kuna matatizo mengine mengine yatahitaji problem solving skills ikiwa na pamoja na kutafuta msaada nje ya institution ili tatizo litatuliwe ipasavyo. Kumbuka hata unapofunga na kusali ili Mungu ayatatue matatizo kwenye ndoa yako, you are also seeking a third party assistance.
 
EMT kiukweli ndivyo watu wanavyoishi wanatafuta wasuluhishi wanarudi tena kukaa chumba kimoja! Inauma ujue yani umeshindwa kunielewa mimi ukumuelewa huyo third part! Wakati unaniambia unanipenda? Kha mioyo ya binadamu mibaya sana.
 
umeshindwa kunielewa mimi ukumuelewa huyo third part! .
yaani wewe ndio umeelewa topic vizuri kabisaaa. Tumeishi wote miaka mingi ila usinielewe wala kusikiliza ninayokwambia aje 3rd party akwambie yale yale umsikilize na ukubali.
 
EMT kiukweli ndivyo watu wanavyoishi wanatafuta wasuluhishi wanarudi tena kukaa chumba kimoja! Inauma ujue yani umeshindwa kunielewa mimi ukumuelewa huyo third part! Wakati unaniambia unanipenda? Kha mioyo ya binadamu mibaya sana.

LD ni kweli unayoyasema. Kila mwanandoa anengependa kutatua matatizo yake bila kumshirikisha third party. In fact, kila mwanadamu angependa kutatua matatizo yake mwenye kulinda privacy. Bahati mbaya hili haliwezekani kwa matatizo yote. Ndio maana unamkuta kwa mfano mwanasheia ameshitakiwa, badala ya kujitetea mwenyewe, anamweka mwanasehria mwingine amtetea. Wakati mwingine unakuta emotions are so high to the extent kuwa hata mwenzako hataki kusikia kabisa sauti yako. Utafanya nini? Utaendelea kuishi na mtu asiyeongea na wewe, uta break up, au utatumia your problem solving skills?
 
Ni vyema wanandoa/wapenzi kumaliza mambo yao wenyewe..kama watu wawili walikutana na kuwa pamoja, hata wakati wa migogoro wawe pamoja kuyamaliza.

Laa ikitokea kumshirikisha mtu basi kuwe na mipaka ya kitakachoongelewa..Naamini wengi wanashirikisha watu kwa kupanic, stress na mawazo ambapo hukuta ameshasema yanayomtatiza hata kama aliapa asingefungua mdomo..ikiwa anayeshirikishwa ana roho nzuri pia experience ya jambo kama hilo anaweza kutoa shauri nzuri kama vile kujishusha,kusamehe na kutoa moyo kuwa hizo changamoto zinatokea hata kwa watu wengine..

Mind you, ujue nini unaongea na unaongea na nani!!..mwisho wa siku ni kujitahidi kupambana na kutatua matatizo binafsi kwa wapenzi wenyewe maana ni sehemu ya maisha!!
 
...hii itatusaidia kujibu.

Joharis- Window.gif


...wanadamu hakuna mkamilifu.
"Atakaye ushauri, amekubali kukosolewa!"
 
Ni vyema wanandoa/wapenzi kumaliza mambo yao wenyewe..kama watu wawili walikutana na kuwa pamoja, hata wakati wa migogoro wawe pamoja kuyamaliza.

Laa ikitokea kumshirikisha mtu basi kuwe na mipaka ya kitakachoongelewa..Naamini wengi wanashirikisha watu kwa kupanic, stress na mawazo ambapo hukuta ameshasema yanayomtatiza hata kama aliapa asingefungua mdomo..ikiwa anayeshirikishwa ana roho nzuri pia experience ya jambo kama hilo anaweza kutoa shauri nzuri kama vile kujishusha,kusamehe na kutoa moyo kuwa hizo changamoto zinatokea hata kwa watu wengine..

Mind you, ujue nini unaongea na unaongea na nani!!..mwisho wa siku ni kujitahidi kupambana na kutatua matatizo binafsi kwa wapenzi wenyewe maana ni sehemu ya maisha!!

...Penye Red, ....very very important point BJ. Ubarikiwe.
 
Mie naona kama unavyoona.Halafu hii tabia ya baadhi ya wanaume kusambaza taarifa za ndani ya nyumba zao au mapungufu ya wake zao kwa ndugu zao ndio inayosababisha ndugu waanze kumchukia mkeo, mpenzio. Ukiingia kwenye mahusiano ikiwamo ndoa, jua fika umekuwa mkumbwa na umeanza familia ambayo ni baba, mama (na watoto kama mtabarikiwa). Aibu yako ni aibu ya familia na aibu ya familia ni yako.
FA hii umenipa elimu mpya....nilikuwa najua na mpaka sasa naamini wanawake ndio wenye tabia ya kutoa mambo ya ndani nje kumbe wanaume pia!!Nadhan mtoa mada umeuliza swali na kujijibu! Kutokubali kujishusha kwa mmoja wa wapenz huchaangia kuhusisha mtu wa nje! Kila Mmoja akipanda hata mkeshe hamtafikia muafaka.... Ila kuna mazingira mengine ambayo huchangia pia, mfano mmekwaruzana na shem, unamwangukia kuomba msamaha shem hataki kabisaaa kukusamehe, nawe wampenda lazima utatoka 'ukajishtaki' kwa mtu mwingine ili aje akuombee msamaha (ilaa kama kosa linatishia kuachwa)
 
Back
Top Bottom