Inakuwaje CCM ndiyo wanauchoka uenyekiti wa Mbowe?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
21,443
40,537
Hili jambo huwa silielewi kabisa. Kweli Mbowe kama binadamu ana madhaifu yake, lakini inakuwaje ni CCM ndiyo wanataka kuweka ukomo wa uenyekiti wa Mbowe CHADEMA?

Yaani ni kama Wamarekani waseme ni kwa nini wajerumani wanaendelea kumchagua Angela Merkel kuwa Kansela wao. CCM kuhusu Mwenyekiti wa Taifa hakuna mahali kwenye katiba yao pamewekwa ukomo wa muda, bali wanabadilishana kwa kutegemea "Tamaduni" ya chama hicho na wala si kwa uchaguzi kwa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho hakuna kugombea nafasi ya mwenyekiti Taifa.

Sasa chama ambacho huwa hakifanyi kabisa uchaguzi wa Mwenyekiti Taifa, kinakuwaje na nguvu ya kimaadili kuwaambia CHADEMA wabadilishe Mwenyekiti wao Taifa? Kwani kwenye Katiba ya CHADEMA kuna kipengele kinakataza mtu kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Taifa zaidi ya mara moja?
 
Nimekuwa nafuatia threads nyingi kwenye mitandao ya kijamii.

Moja kati ya threads hizo ni hii ya kumtaka Mh.Freeman Mbowe aachie Uenyekiti Na wanaoongoza Na suala hilo ni CCM.

Ni dhahiri kuwa Uongozi wa Mh.Mbowe ni mwiba Kwa CCM.

Nawaomba wanachama wa Chadema Na Viongozi wake huu ni wakati wa Kushikamana maadui wa Chadema wanajukikana, Wasaliti wa Vyama vya Upinzani wanajulikana Na tunawaona .
 
Democracy

Cdm kubadilisha katiba ili mwenyekiti awe wa milele sio democracy

Kupitisha mgombea urais kwa kura za ndioooooooo sio democracy.

Kupingana na mwenyekiti unafukuzwa sio democracy.

Kuwa na wafuasi ambao hawawezi kufikiri nje ya fikra za mwenyekiti hiyo sio democracy.

Kukataza/kuzuia mikutano ya kisiasa sio democracy.

Kuhisi peke yako ndio mwenye akili sio democracy.

Kutosimamia sheria sio democracy.

Kutumia cheti cha MTU ni kuvunja sheria.

Kujihisi wewe ni mtoto wa mfalme wakati sio kweli hiyo sio democracy.

Kujifanya hupangiwi sio democracy.

Ukiwa njaa huwezi kupractice democracy(kila wakati utawaza tumbo lako )
 
Na siku upinzani wakirubunika kumtoa mbowe basi kuna uwezekano ccm wakapenyeza pandikizi lao!
Tundu lissu anafaa ila abaki kuwa mwanasheria wa chama!

Huwa wanataka wapate mtu watakayemyumbisha kirahisi yawe kama haya ya cuf na nccr kipindi hicho!
 
Kwa hili namuunga mkono magufuli kutokana na smsimamo wake kuwa ukiona adui yako anakupromote ujue umechemka na ukiona anakupinga ujue umepatia hivyo kazia hapo hapo.Lakini huu ni mtazamo tu inaweza kuwa vinnginevyo
 
Ni kweli huu utetezi wa wanacdm wengi kuhusu Mbowe kukaa muda mrefu madarakani. Lakini tujiulize je ni kweli bila Mbowe cdm itayumba? Hivi inge/ikitokea Mbowe akafariki ndio mwisho wa cdm? Hivi hatuona kuwa kitendo cha Mbowe kumleta Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea urais ni ndio imechangia leo hii cdm kuongea kitu na watawala kuwapuuza? Huwezi kufananisha cdm ya kabla ya Lowassa na cdm baada ya kuwasili Lowassa. Inahitaji ushabiki wa kisiasa kuendelea kumpigia debe Mbowe kuwa mwenyekiti. Ni kweli amefanya mazuri mengi sana kukifikisha chama hapo kilipo, lakini kiukweli sasa ni wakati wa yeye kukaa pembeni na wala sio kwa matakwa ya ccm bali kutokana na uhalisia tu.
 
Mbowe siku akiachia uenyekiti kabla ya maccm kutoka madarakani basi tusahau mkoloni mweusi kuondoka madarakani
 
Nimekuwa nafuatia threads nyingi kwenye mitandao ya kijamii.Moja kati ya threads hizo ni hii ya kumtaka Mh.Freeman Mbowe aachie Uenyekiti Na wanaoongoza Na suala hilo ni CCM .Ni dhahiri kuwa Uongozi wa Mh.Mbowe ni mwiba Kwa CCM.Nawaomba wanachama wa Chadema Na Viongozi wake huu ni wakati wa Kushikamana maadui wa Chadema wanajukikana, Wasaliti wa Vyama vya Upinzani wanajulikana Na tunawaona .
Hapana Mbowe ni dikteta na mwenyekiti wa kudumu wa Chadema,tunachopinga ni kuwa yale anayoyahubiri ni tofauti na anayoyatenda,kuanzia kwa Ole Sosopi akamleta Msigwa,ok huko hatuwaingilii ni Ufipa ,lakini kwa EALA ambalo ni la kitaifa lazima tuwanyoroshe kwa kutaka kuleta ufipa kwenye bunge.Kwa sasa Mbowe ni sawa na Wenger wa Arsenal
 
Hili jambo huwa silielewi kabisa. Kweli Mbowe kama binadamu ana madhaifu yake, lakini inakuwaje ni CCM ndiyo wanataka kuweka ukomo wa uenyekiti wa Mbowe CHADEMA?

Yaani ni kama Wamarekani waseme ni kwa nini wajerumani wanaendelea kuchagaua Angela Merkel kuwa Kansela wao. CCM kuhusu Mwenyekiti wa Taifa hakuna mahali kwenye katiba yao pamewekwa ukomo wa muda, bali wanabadilishana kwa kutegemea "Tamaduni" ya chama hicho na wala si kwa uchaguzi kwa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho hakuna kugombea nafasi ya mwenyekiti Taifa.

Sasa chama ambacho huwa hakifanyi kabisa uchaguzi wa Mwenyekiti Taifa, kinakuwaje na nguvu ya kimaadili kuwaambia CHADEMA wabadilishe Mwenyekiti wao Taifa? Kwani kwenye Katiba ya CHADEMA kuna kipengele kinakataza mtu kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Taifa zaidi ya mara moja?
Ungewauliza kwanza Chadema na Mbowe wenu ambao kila siku hakuchi bila kuisema CCM utadhani wao ni wanachama wa CCM
 
Hili jambo huwa silielewi kabisa. Kweli Mbowe kama binadamu ana madhaifu yake, lakini inakuwaje ni CCM ndiyo wanataka kuweka ukomo wa uenyekiti wa Mbowe CHADEMA?

Yaani ni kama Wamarekani waseme ni kwa nini wajerumani wanaendelea kuchagaua Angela Merkel kuwa Kansela wao. CCM kuhusu Mwenyekiti wa Taifa hakuna mahali kwenye katiba yao pamewekwa ukomo wa muda, bali wanabadilishana kwa kutegemea "Tamaduni" ya chama hicho na wala si kwa uchaguzi kwa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho hakuna kugombea nafasi ya mwenyekiti Taifa.

Sasa chama ambacho huwa hakifanyi kabisa uchaguzi wa Mwenyekiti Taifa, kinakuwaje na nguvu ya kimaadili kuwaambia CHADEMA wabadilishe Mwenyekiti wao Taifa? Kwani kwenye Katiba ya CHADEMA kuna kipengele kinakataza mtu kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Taifa zaidi ya mara moja?
Maccm woooooote wanamgwaya saaaaana Mbowe
 
Back
Top Bottom