Ninapenda kuongea na mashabiki wa CCM. Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi sana hasa ni nini CCM INACHOTAFUTA? Nimefahamu na kugundua kuwa CCM inachotafuta ni ulaji tu na sio kweli kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli. Kama kweli CCM ni chama cha watu wote na kinawajali wanyonge wasingeweza kufanya yafuatayo
- Kutumia kila aina ya mbinu kuhakikisha Dr. Slaa haonekani katika vyombo vya habari,wala kusikika, Hivyo kuwanyima haki wananchi kuwasikiliza wagombea na kuamua wampe nani kura. Kama CCM wanaamini sera zao ni nzuri kwa nini wanazuia sera za mwingine ambaye wanasema sio nzuri kujulikana kwa wananchi? Katika hilo mtanzania huitaji ushabiki inahitaji akili kidogo tu kufikiri na kujua yupi bora
- CCM wamekataa midahalo, Kama CCM mna amini wagombea wenu ni safi na makini kuanzia raisi mpaka wabunge kwa nini muogope kuulizwa maswali na wananchi, ambao mnasema mnawapenda na kuwajali? na pia kwa nini mnaogopa kuwekwa pamoja na wapinzani wenu ambao mnawaita wadhaifu , hawana uwezo wa kuongoza !Katika hilo haitaji ushabiki, unahitaji akili ndogo tu kufikiri na kujua yupi bora.
- CCM kwa nini mnakumbatia ushirikina(refer statement za sheikh yahya) kama kweli mnawajali wananchi, kwa nini kutafuta kura kwa ushirikina. Kama mna amini sera na mambo yenu wananchi wanayakubali. katika hilo huitaji ushabiki, inahitaji akili ndogo sana kufikiri yupi bora.
- Ufisadi ndo hamtaki kabisa kuongelewa, kama ufisadi wa CCM si kweli kwa nini mnatumia nguvu kuhakikisha watu hawaongelei ufisadi? Mwana CCM huitaji ushabiki katika hilo, INAHITAJI AKILI NDOGO SANA NA UZALENDO WA KWELI KUAMUA NANI NI KIONGOZI ANAYETAKIWA KUONGOZA TAIFA LETU.