unalaumu au unasema mkuu ? kwani huoni nilivyo Copy na Paste? Mwisho wa maandishi huoni Address yako? Au kuna ubaya Copy and Paste Mkuu wewe si umetafsiri kwa kiswahili ili watu wapate kujuwa mimi nime Copy kwenye Blog yako kuwapa hapa watu Wafaidike kuna ubaya gani mkuu?Wakubwa naomba ushauri,inakuwaje post zangu zote nilizoandika kuhusu tech hazionekani na ghafla naona post zote zimeibuka tena ila muandishi ni mtu mwingiine(Mzizi Mkavu)?
Mkubwa awali ya yot ninachokifanya sio kutafsiri kama unavyofikiria(labda picha baadhi ndio za kukopy na kupaste),ila makala zote huwa ninaandika kuanzia mwanzo. Hivyo hakuna suala la kutafsiri hapo.
Pili,Kama ningeona umeonesha source,nisingeandika hapa.Nimepitia habari zote,hakuna hata moja iliyoonesha source.
haswaa,Kama ukiangalia kwa undani kwenye download hakuna kazi hata moja wa Mtanzania, Kama utatafakari utagundua kuwa hizi ni vitu viwili tofauti. Je ni watanzania wangapi wenye uwezo wa kununua hivyo vitabu? Pia kama umesoma Kuhusu Downloads! Kizuri gawana na wenzako! utagundua tumeandika kila kitu hapo.
Vilevile angalia Technology--News sehemu ambayo tunaweka habari za kitanzania tulizokopi na kupaste,zote tumeonesha Source chini kabisa
Nilichotaka kumaanisha kuwa,ni kitu cha busara kuthamini kazi za wanyonge kama sisi,JF na AfroIT sote tuna lengo moja la kuisaidia jamii,ila lazima tuheshimiane,ndio maana tangu AfroIT ianze sijawahi kukopi makala yoyote toka kwenye hili jukwaa na kuipeleka kule,hata za kwenye News. Hivyo kama mtu akikopi na kupaste toka AfroIT basi aoneshe Source,kwa kufanya hivi inaleta faraja na moyo kwa waandishi kuendelea kuandika makala za kiswahili ili ije siku tuwe na contents za kutosha za kiswahili.
Note:AfroIT inaruhusu matumizi ya contents ili hali umeonesha source;
All in all,tuishie hapa,nadhani umenipata mkuu MziziMkavu.
Admin naomba ifute hii topic kabla ya mamluki hawajaja.