Maryam Malya
Senior Member
- Nov 29, 2021
- 115
- 258
Moja ya sifa ya Kiongozi bora ni kuibua viongozi wengine na kupelekea kutimiza ndoto zao na hii imekua moja ya sifa kubwa na zakipekee za Rais Samia Suluhu Hassan.
Kwenye teuzi za hivi karibuni Rais Samia ameweka imani kwa maingizo mapya kwenye Baraza la Mawaziri kwa kumleta Hamis Mwinjuma (Mwana FA), kuwa Naibu Waziri Utamaduni Sanaa na Michezo na kuifanya Wizara hiyo kwa mara ya kwanza kuongozwa na Msanii.
Kwenye teuzi za nyuma Rais Samia alionesha upendo kwa kutuletea maingizo mapya kwenye Baraza la Mawaziri alitupa Naibu Waziri Ridhiwani Kikwete na Waziri Mohammed Mchengerwa wote hawa ni viongozi vijana ambao jicho la upendo la Rais Samia liliwaamini kushika nafasi kubwa za maamuzi.
Hongera sana Rais Samia uliowapa Imani na upendo wako watakulipa kwenye Utendaji.