johnmashilatu
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 718
- 703
AGIZO la Jaji Mkuu Agustino Ramadhan la kupatiwa dhamana kwa raia wa Afrika Kusini, mwenye asili ya Kiasia Dawid Human (48), aliyehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela na faini ya sh milioni mbili, limefanikisha mfungwa huyo kuachiwa kwa dhamana.
Dawid, ni Mkuu wa Kitengo cha ulinzi cha kampuni ya Geita Gold Mines (GGM); alikutwa na hatia ya shambulio la aibu hivyo kupewa adhabu hiyo Desemba 10 mwaka huu, baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, kujiridhisha kwamba mfungwa huyo alitenda kosa.
Baada ya hukumu hiyo kutolewa, Dawid alikata rufaa na wakati huo huo Jaji Ramadha, aliagiza mfungwa huyo kupewa dhamana baada ya maombi ya dhamana yake kuwasilishwa kwa jaji huyo.
Kwa mujibu wa maelekezo ya Jaji Ramadhan, Dawid alipewe dhamana hiyo kwa sababu za kibinadamu hivyo kutakiwa kuwasilisha mahakamani hapo pasi ya kusafiria na mdhamini mmoja aliyesaini mkataba wa dhamana ya sh milioni tano.
Hata hivyo, Dawid alifanikiwa kutimiza masharti ya dhamana hiyo na hivi sasa yuko nje. Akizungumzia suala hilo kwa niaba ya Msajili Msaidizi wa Mahakama ya Rufaa, Janeth Masesa, ambaye pia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Nyamaga, alisema Dawid akamilisha masharti ya dhamana yake Desemba 21 mwaka huu.
Masesa, alisema raia huyo wa kigeni atakuwa nje kwa dhamana hadi hapo rufaa yake itakapoanza kusikilizwa. Hukumu ya Dawid ilitolewa na Jaji Aishiel Sumari wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo. Ilidaiwa kuwa Machi mwaka 2007 katika kijiji cha Mchauru, kilicho kwenye mgodi wa Geita, Dawid, alimshika matiti, sehemu za siri na makalio Adelina kwa nia ya kumnyanganya kitambulisho baada ya kufukuzwa kazi mgodini hapo.
Source: Tanzania daima
My take
Imani na Jaji mkuu huyo Brigedia jenerali, mwimba kwaya, Agustino Ramadhan ilinitoka siku nyingi hasa alipoongoza jopo la majaji wenzake na kukataa asiwepo mgombea binafsi.
mimi sio mwanasheria, lakini hizo sababu za kiutu kwanini zitolewe kwa mzungu pekee? au huyo mzungu ndio mtu zaidi ya mama aliyemdhalilisha?
Nafikiri jaji Agustino ramadhani ambaye pia nasikia ni mwenyekiti wa mahakama ya haki za binadamu ya afrika, anapaswa kuchagua moja. yeye ni Muumini na kule kile kifungu kinachosema, Huwezi......, chagua, kwaya au anzisha kampuni ya ulinzi huko unaweza kufanya vizuri vinginevyo idara ya mahakama chini yako inatia kizunguzungu
naambiwa kesho unaweza kuagwa (kustafu) mimi nasema umechelewa!, tutakukumbuka kw alipi ulilofanya wakati wa uongozi wako wa idara ya mahakama?, nakumbuka samwel Sitta aliwahi kukupa vidonge vyako kutokana na jinsi mahakama inavyofanya kazi zake.
Dawid, ni Mkuu wa Kitengo cha ulinzi cha kampuni ya Geita Gold Mines (GGM); alikutwa na hatia ya shambulio la aibu hivyo kupewa adhabu hiyo Desemba 10 mwaka huu, baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, kujiridhisha kwamba mfungwa huyo alitenda kosa.
Baada ya hukumu hiyo kutolewa, Dawid alikata rufaa na wakati huo huo Jaji Ramadha, aliagiza mfungwa huyo kupewa dhamana baada ya maombi ya dhamana yake kuwasilishwa kwa jaji huyo.
Kwa mujibu wa maelekezo ya Jaji Ramadhan, Dawid alipewe dhamana hiyo kwa sababu za kibinadamu hivyo kutakiwa kuwasilisha mahakamani hapo pasi ya kusafiria na mdhamini mmoja aliyesaini mkataba wa dhamana ya sh milioni tano.
Hata hivyo, Dawid alifanikiwa kutimiza masharti ya dhamana hiyo na hivi sasa yuko nje. Akizungumzia suala hilo kwa niaba ya Msajili Msaidizi wa Mahakama ya Rufaa, Janeth Masesa, ambaye pia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Nyamaga, alisema Dawid akamilisha masharti ya dhamana yake Desemba 21 mwaka huu.
Masesa, alisema raia huyo wa kigeni atakuwa nje kwa dhamana hadi hapo rufaa yake itakapoanza kusikilizwa. Hukumu ya Dawid ilitolewa na Jaji Aishiel Sumari wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo. Ilidaiwa kuwa Machi mwaka 2007 katika kijiji cha Mchauru, kilicho kwenye mgodi wa Geita, Dawid, alimshika matiti, sehemu za siri na makalio Adelina kwa nia ya kumnyanganya kitambulisho baada ya kufukuzwa kazi mgodini hapo.
Source: Tanzania daima
My take
Imani na Jaji mkuu huyo Brigedia jenerali, mwimba kwaya, Agustino Ramadhan ilinitoka siku nyingi hasa alipoongoza jopo la majaji wenzake na kukataa asiwepo mgombea binafsi.
mimi sio mwanasheria, lakini hizo sababu za kiutu kwanini zitolewe kwa mzungu pekee? au huyo mzungu ndio mtu zaidi ya mama aliyemdhalilisha?
Nafikiri jaji Agustino ramadhani ambaye pia nasikia ni mwenyekiti wa mahakama ya haki za binadamu ya afrika, anapaswa kuchagua moja. yeye ni Muumini na kule kile kifungu kinachosema, Huwezi......, chagua, kwaya au anzisha kampuni ya ulinzi huko unaweza kufanya vizuri vinginevyo idara ya mahakama chini yako inatia kizunguzungu
naambiwa kesho unaweza kuagwa (kustafu) mimi nasema umechelewa!, tutakukumbuka kw alipi ulilofanya wakati wa uongozi wako wa idara ya mahakama?, nakumbuka samwel Sitta aliwahi kukupa vidonge vyako kutokana na jinsi mahakama inavyofanya kazi zake.