Ili tuwe na uhamiaji wenye tija, tufanye haya

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
8,388
4,052
Ili tuwe na wahamiaji wenye awe tija mfanyabiashara au wafanyakazi vitu vifuatavyo vinatakiwa kuzingatiwa na mamlaka zinazohusika, uhamiaji, Wizara ya kazi , TIC, fedha/TRA , na Biashara na madini.

Moja wahamiaji wote awe muwekezaji au mfanyakazi awe ana ishi kwenye makazi ya watu sio magodown au sehemu zao za Biashara

Pili office zao au shughuli zao za biashara zisiwe kwenye makazi yao au watu , Bali yawe kwenye sehemu ambayo zinatambulika Kama ni office bldg or business premises.

Tatu wapewe tax number ambayo itakuwa linked na Biashara anayofanya au mshahara anaopata hivyo inakuwa rahisi kufuatilia ulipaji kodi na tija yake kwa nchi.

Kuna wengine wanakuja Lakini hawalipi kodi kwenye mishahara Yao au Biashara zao.

Na wanapokaa kwenye magodown inakuwa rahisi wao kujificha au kujifanya ni Mgeni na si mfanyakazi

Na pia kutumia sehemu hizo kufanya Biashara zingine ambazo si halali au tofauti na Vibali vyao vya kuishi nchini.

Na kwa wanaochukua au kupata TIC certificate wawe na proper organization chart inayoonyesha who is who au key personnel.

Na ilikibidi ufuatliaji ufanyike kwenye hili kwani wengine hawatekelezi hili la organization structure au kufukuza local staff Baada ya kupata tic certificate na kushindwa kwendana na ahadi zao au walicho sema
 
Back
Top Bottom