MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Mafanikio ya CCM kwenye uchaguzi wa 2015 na hakika miaka ya mbeleni baada ya hapo ita tegemea sana na safu ya wagombea itakayo wakilisha kwa wananchi hapo 2015. Kwa vile JK kikatiba hata ruhusiwa kugombea 2015 hakuna sababu ya CCM kusumbuliwa na utaratibu wao wa kumpitisha raisi anaye toka chama chao kugombea muhula wa pili bila kupingwa.
Nikisema safu ya wagombea namaanisha wote wabunge pamoja na mgombea uraisi. Nitajaribu kuelezea jinsi wagombea ubunge na uraisi watakavyo kiua au kukifufua CCM.
1. Wagombea ubunge:
Kwanza hapa wanabidi wafuate demokrasi na kuhakikisha alieshinda kura za maoni ndiyo mgombea. Lazima mgombea ubunge aonekane kuwa chaguo la watu laa sivyo wapiga kura wataona walio pitishwa ni wagombea wenye kutetea maslahi ya wachache ndani ya chama na si wananchi.
Wahakikisha wana pata wagombea ubunge wenye mvuto kwa jamii na rekodi nzuri katika utumishi. Hii ita saidia kukipa mvuto tena chama na kurudisha imani ya wananchi kwake. Kuna wanaCCM wengi tu wanaopendwa na kuheshimiwa na jamii pamoja ya kwamba CCM kiujumla wake si maarufu kwa sasa.
Wahamasishe vijana wengi zaidi wagombee ubunge kupitia chama chao. Na hapa namaanisha vijana ambao hawaji na mzigo wowote i.e. not the Laus and the like. Kwa kawaida vijana wana clean record na jamii ipo tayari zaidi kuwapa nafasi. Lakini muhimu zaidi itaonyesha kwamba chama kipo tayari kuanza upya na kufungua ukurasa mpya.
2. Mgombea urais:
Sihitaji kusisitiza umuhimu wa mgombea raisi kwa chama chochote. Mgombea uraisi ndiyo kama "kapteni" wa safu ya wagombea ofisi za umma wa chama chochote. Mgombea uraisi kwa mvuto wake ana weza hata kusaidia wagombea wa nafasi mbali mbali toka chama chake washinde. Mgombea uraisi ndiye sura wa chama katika chaguzi na ndiyo kiashiria ya nini tutegemee kutoka kwa chama hicho.
Hapa CCM isilambe matapishi yake. Hapa namaanisha kuto kung'an'gania kumuweka mtu ambae alisha poteza mvuto kwa jamii. Nadhani hapa wote mnajua namaanisha nini. Mgombea uraisi siyo lazima atoke kwenye kundi la wale "usual suspects". Washtueni wananchi kwa kumuweka hata mtu ambae hawaja fikiria kabisa ange gombea kama ilivyo kuwa kwa Chadema na Dr. Slaa.
Wakati wa kuchagua mgombea msiangalie tu CCM mnamtaka nani bali angalieni wananchi wanamtaka nani. Kwani mgombea uraisi ni wa chama ila akisha kuwa raisi ana kuwa raisi wa wananchi wote. Kwa hiyo msiangalie tu maslahi ya chama.
Hakika msi chague mtu yoyote ambae ana connections na failures za awamu itakayo kuwa ina maaliza muda wake. Hii itaonekana kama muendelezo wa yale yale kama vile John McCain wa Marekani alivyo onekana angekua muendelezo wa yale yale ya George Bush. Kuweni makini sana. Kwa safari hii nawa shauri mvunje utamaduni na kuto kumchagua mtu yoyote aliye kuwa waziri katika awamu hii ya nne.
Chagueni mtu ambae hana madeni makubwa ya fadhila! Hii itampunguzia uwezo wa kuchagua watu kwenye nafasi za uteuzi kwa kuzingatia merit za hao watu. Kila mwanasiasa ana madeni kwa vile hamna anaeingia ofisini bila kuwa na nguvu za watu nyuma yake ila wekeni mtu mwenye deni dogo iwezekanavyo.
Mwisho:
Haya ni maoni yangu tu. Hakika maamuzi ya mwisho ni ya CCM yenyewe na hatma ya chama ipo katika uongozi wa sasa. Sitegemei kwamba nita sikilizwa mwananchi wa kawaida kama mimi. Ila mwishoni hakika hamtaweza kusema hamkuambiwa.
Nikisema safu ya wagombea namaanisha wote wabunge pamoja na mgombea uraisi. Nitajaribu kuelezea jinsi wagombea ubunge na uraisi watakavyo kiua au kukifufua CCM.
1. Wagombea ubunge:
Kwanza hapa wanabidi wafuate demokrasi na kuhakikisha alieshinda kura za maoni ndiyo mgombea. Lazima mgombea ubunge aonekane kuwa chaguo la watu laa sivyo wapiga kura wataona walio pitishwa ni wagombea wenye kutetea maslahi ya wachache ndani ya chama na si wananchi.
Wahakikisha wana pata wagombea ubunge wenye mvuto kwa jamii na rekodi nzuri katika utumishi. Hii ita saidia kukipa mvuto tena chama na kurudisha imani ya wananchi kwake. Kuna wanaCCM wengi tu wanaopendwa na kuheshimiwa na jamii pamoja ya kwamba CCM kiujumla wake si maarufu kwa sasa.
Wahamasishe vijana wengi zaidi wagombee ubunge kupitia chama chao. Na hapa namaanisha vijana ambao hawaji na mzigo wowote i.e. not the Laus and the like. Kwa kawaida vijana wana clean record na jamii ipo tayari zaidi kuwapa nafasi. Lakini muhimu zaidi itaonyesha kwamba chama kipo tayari kuanza upya na kufungua ukurasa mpya.
2. Mgombea urais:
Sihitaji kusisitiza umuhimu wa mgombea raisi kwa chama chochote. Mgombea uraisi ndiyo kama "kapteni" wa safu ya wagombea ofisi za umma wa chama chochote. Mgombea uraisi kwa mvuto wake ana weza hata kusaidia wagombea wa nafasi mbali mbali toka chama chake washinde. Mgombea uraisi ndiye sura wa chama katika chaguzi na ndiyo kiashiria ya nini tutegemee kutoka kwa chama hicho.
Hapa CCM isilambe matapishi yake. Hapa namaanisha kuto kung'an'gania kumuweka mtu ambae alisha poteza mvuto kwa jamii. Nadhani hapa wote mnajua namaanisha nini. Mgombea uraisi siyo lazima atoke kwenye kundi la wale "usual suspects". Washtueni wananchi kwa kumuweka hata mtu ambae hawaja fikiria kabisa ange gombea kama ilivyo kuwa kwa Chadema na Dr. Slaa.
Wakati wa kuchagua mgombea msiangalie tu CCM mnamtaka nani bali angalieni wananchi wanamtaka nani. Kwani mgombea uraisi ni wa chama ila akisha kuwa raisi ana kuwa raisi wa wananchi wote. Kwa hiyo msiangalie tu maslahi ya chama.
Hakika msi chague mtu yoyote ambae ana connections na failures za awamu itakayo kuwa ina maaliza muda wake. Hii itaonekana kama muendelezo wa yale yale kama vile John McCain wa Marekani alivyo onekana angekua muendelezo wa yale yale ya George Bush. Kuweni makini sana. Kwa safari hii nawa shauri mvunje utamaduni na kuto kumchagua mtu yoyote aliye kuwa waziri katika awamu hii ya nne.
Chagueni mtu ambae hana madeni makubwa ya fadhila! Hii itampunguzia uwezo wa kuchagua watu kwenye nafasi za uteuzi kwa kuzingatia merit za hao watu. Kila mwanasiasa ana madeni kwa vile hamna anaeingia ofisini bila kuwa na nguvu za watu nyuma yake ila wekeni mtu mwenye deni dogo iwezekanavyo.
Mwisho:
Haya ni maoni yangu tu. Hakika maamuzi ya mwisho ni ya CCM yenyewe na hatma ya chama ipo katika uongozi wa sasa. Sitegemei kwamba nita sikilizwa mwananchi wa kawaida kama mimi. Ila mwishoni hakika hamtaweza kusema hamkuambiwa.