Ileje ni moja ya Wilaya duni nchini ikiwa ni miaka 48 tangu kuundwa na ikiwa chini ya CCM

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,811
218,468
Wilaya ya Ileje ni miongoni mwa Wilaya zilizounda Mkoa wa Mbeya (naambiwa sasa imehamishiwa Mkoa wa Songwe ) ni miongoni mwa wilaya zinazounda Mkoa huo, historia inaonyesha kwamba kabla ya kuwa Wilaya. Ileje ilikuwa sehemu ya Wilaya ya Rungwe.

Mpaka sasa imetimia miaka 48 tangu Ileje iliporasimishwa na kuwa Wilaya. Bali umasikini unaoiandama Wilaya hii unatisha. Kibaya zaidi Hali ya Umasikini wa kutupwa wa Ileje inafichwa na viongozi wa serikali na ccm ili kuepusha Aibu, shule ni duni, huduma za afya ni duni, huduma za kijamii ni duni, hali ya uchumi wa mtu mmoja mmoja inasikitisha, kwa ufupi ni kwamba Ileje inanuka umasikini wa kutia aibu.

Lakini cha kushangaza ni kwamba , Wilaya, Halmashauri na Jimbo hilo vimeongozwa na ccm kuanzia enzi za Uhuru hadi leo, ukiacha madiwani wawili watatu kutoka NCCR, TLP na CHADEMA.

Iko haja sasa ya wananchi kushikamana kwa pamoja kuikomboa Ileje kwa Udi na Uvumba ili kunusuru maisha ya Watu .

FB_IMG_1691319688775.jpg
FB_IMG_1691319695756.jpg
FB_IMG_1691319705190.jpg
 
Wilaya ya Ileje ni miongoni mwa Wilaya zilizounda Mkoa wa Mbeya (naambiwa sasa imehamishiwa Mkoa wa Songwe ) ni miongoni mwa wilaya zinazounda Mkoa huo, historia inaonyesha kwamba kabla ya kuwa Wilaya. Ileje ilikuwa sehemu ya Wilaya ya Rungwe.

Mpaka sasa imetimia miaka 48 tangu Ileje iliporasimishwa na kuwa Wilaya. Bali umasikini unaoiandama Wilaya hii unatisha. Kibaya zaidi Hali ya Umasikini wa kutupwa wa Ileje inafichwa na viongozi wa serikali na ccm ili kuepusha Aibu, shule ni duni, huduma za afya ni duni, huduma za kijamii ni duni, hali ya uchumi wa mtu mmoja mmoja inasikitisha, kwa ufupi ni kwamba Ileje inanuka umasikini wa kutia aibu.

Lakini cha kushangaza ni kwamba , Wilaya, Halmashauri na Jimbo hilo vimeongozwa na ccm kuanzia enzi za Uhuru hadi leo, ukiacha madiwani wawili watatu kutoka NCCR, TLP na CHADEMA.

Iko haja sasa ya wananchi kushikamana kwa pamoja kuikomboa Ileje kwa Udi na Uvumba ili kunusuru maisha ya Watu .

View attachment 2709997View attachment 2709998View attachment 2709999
What is your point?
 
Barabara ya Lami ipo ni almost 48 km kutoka Mpemba kimsingi hiyo wilaya inategemea zaidi kilimo hususani mazao ya chakula kama Mahindi, karanga nk
 
Labda niseme ukweli, changamoto zipo kwenye wilaya hii,lakini umeexagrate sana kwamba ileje maisha ni magumu kiasi hicho si kweli,ileje chakula si shida na wamalawi wanaishi kwasababu ya wilaya hii,tarafa ya Bundali kuna ndizi,kahawa,viazi,mahindi hakuna njaa.........yes uongozi wa mbunge wa Steven kibona aliyekuwa anaelekea kuikomboa wilaya bahati mbaya alifariki,Akaje Cheyo aliyekuwa waziri wa ardhi huyu kweli alikuwa mzigo,baadaye kibona na sasa hivi Msongwe ambaye ameikomboa wilaya hasa kwenye miundombinu.

Kwa makazi wilaya ya ileje watu wote tangu enzi na enzi ni nyumba za matofali,njaa haijawahi kutokea ileje kama baadhi ya maeneo kwasababu mvua ipo ya kutosha sana.

Changamoto kubwa ilikuwa ni barabara kutoka Mpemba to Isongole saizi ni lami,lakini tayari mkandarasi anaingia kazini Kwa barabara ya Isongole -Malangali Ndembo -Kasumulu Kyela,mazao yamekuwa yakioza Kwa kukosa soko kwasababu ya miundombinu hasa wakati wa mvua.....Ila ujio wa Kasekesnya Msongwi amepunguza changamoto nyingi na hiyo shule uliyoweka Picha ni eneo ambalo sina uhakika kama kuna zaidi ya wakazi mia tano,ni eneo ambalo liko porini sana njia ya kuelekea Kyela,na unaweza kuta mwalimu mmoja shule nzima.

Pia,mgodi wa kiwira uko wilaya hii lakini wanufaika walikuwa Rungwe na Kyela kupata kodi na ileje kijiografia haikutakiwa kuwa Songwe lakini ni Siasa baada ya kuwapora tonge Kyela na Rungwe kupata gawio la mgodi ambao uko kwenye wilaya ya ileje.....ileje ilikuwa haipati kitu japo mgodi upo ileje.

Kuna mengi umeandika hapo hayana uhalisia na wilaya hii yenye kila kitu
 
Back
Top Bottom