Ikulu mbona hamjibu tuhuma hii?

Ikulu mbona hamjibu tuhuma hii?

Walimtumia Shamsi Vuai Nahodha kuanza kulainisha nati ... Kamwe JK hawezi kufanyakosa la kiufundi la kumjibu Lowassa maana atafunguka zaidi ...

Kabisa mkuu. Hawezi kujibu tuhuma hizi,mengi yatafumuka.
 
Hawawezi kuthubutu kuujibu kwani utamweka rehani Bosi wake JK, kumbuka Tundu Lissu aliongea nini wakati wa issue ya escrow ikijadiliwa bungeni juu ya mkataba wa IPTL, JK ana scandal nyingi kuhusiana na mikataba ya umeme kwa vile yeye wakati mikataba hiyo inasainiwa katika vipindi tofauti alikuwa Waziri wa Nishati na Madini kisha Waziri wa Fedha na Escrow amekuja kuitetea akiwa rais. Jamaa anajua sana kuwabambikia mizigo wenzake kumbe yeye ndiye mhusika mkuu. Nakumbuka wakati vyombo vya habari vikianza kudodosa issue ya Richmond kuna wakati JK alikuwa akitoa ufafanuzi sana juu ya kinachoendelea hadi gazeti moja liliandika kichwa cha habari kifutacho nanukuu ' HIVI KIKWETE AMEKUWA MSEMAJI WA RICHMOND'? Mwanzoni mwa issue ya Richmond jamaa alikuwa anaitetea ile mbaya.

Usisahau kuwa familia yake ndiyo mmiliki halali wa PAP
 
juu wapi? nadhani jamaa bado wanajadili kama hiyo juu ilimaanisha hapo, maana hata mimi hiyo kauli haipo wazi sana, juu ya meza, kiti au juu ya paa, sikuielewa.

Hahahahahahahahahaha JF bwana inao gt,....
 
thubutu wakanusheeee hawajitaki kustaafu kwema, maana salva, mkulu wanastaafu oct 25, salva inabidi aanza kujikomba kwa anayekuja aone kama ataambulia chochote au kilimo kinamsubili.
Salva atajikomba kwa nani? Maana kama ni Magufuli alimchafua sana. Kama ni Lowassa walishafarakana
 
hahaaa,haaa hawawezi kumjibu huyo vasco ana kawaida ya kusema kelele za mpangaji hazimnyimi mwenye nyumba usingizi.
 
Swali ni kwa nin ikulu hawajakanusha??

Hv ana ushahidi kuwa aliamrishwa na mamlaka ya juu?Sio tu anabwabwaja ooh, Mwanyika atoka kuongea, ooh mara akarudi na kuniambia ameagzwa iwe ıv au vile.Umbea tu, kwani yeye hakuwa na namba ya mkuu wa Kaya?
 
Tukijibu sasa yatafumuka mengi tukapunguza kula.... kwa jinsi wananchi walivyoamka goal la mkono tumeona ngumu.
 
Usisahau kuwa familia yake ndiyo mmiliki halali wa PAP

Hakika katika kuishi kwangu sijawahi kushuhudia Rais msanii kama Jk, anastaafu akiwa ni bilionea wa kutupa kutokana na mikataba hiyo michafu ya magabacholi huku akiwa amewaachia watu wengine hata rafiki zake wa karibu vidonda vya kudumu mioyoni mwao, inafaa akatubie dhambi hii.
 
Imekuwa kawaida ya wasemaji wa ikulu kujibu haraka haraka tuhuma zinazotolewa juu ya watumishi wa ikulu hasa rais kikwete.

Majuzi tumemsikia EL akidai kuwa mamlaka ya juu yake (rais) indiyo iliidhinisha mkataba wa richmond kusainiwa licha ya kutiliwa shaka na wataalam. Swali ni kitu gani kinamzuia salva na wenzake kuliongelea hili (kukanusha) kama ilivyo kawaida yao?

Tafakari!
etc
hakusema ikulu wala rais, mamlaka iliyo juu yake inaweza kuwa ni makamu wa rais, rais wa zanzibar,
 
Hakika katika kuishi kwangu sijawahi kushuhudia Rais msanii kama Jk, anastaafu akiwa ni bilionea wa kutupa kutokana na mikataba hiyo michafu ya magabacholi huku akiwa amewaachia watu wengine hata rafiki zake wa karibu vidonda vya kudumu mioyoni mwao, inafaa akatubie dhambi hii.

Haki haipotei ila inaweza kucheleweshwa tu.
 
Unatuaminisha kuwa EL sio mwizi wala hakushiriki wizi?
 
etc
hakusema ikulu wala rais, mamlaka iliyo juu yake inaweza kuwa ni makamu wa rais, rais wa zanzibar,
mkuu umetoka chooni?lini waziri Mkuu wa JMT mamlaka ya juu yake ikawa serikali ya zmz
 
Back
Top Bottom