Jamani wapendwa wana JF wenzangu, Nimedata? within one month 3 cars within predent's office related to him straight have been involved in scandals of tyres and dirty fuel. Who is iresponsible to that? who has to be punished? How is president supposed to react to this for his security?
Ikulu yakanusha Rais kupata ajali
20th June 2010
Ikulu imekanusha na kufafanua juu ya taarifa iliyotolewa na gazeti moja la kila siku (sio Nipashe) lililoripoti kuwa Rais Jakaya Kikwete amenusurika katika ajali baada ya gari lake kupasuka tairi wakati msafara wake ukipita hifadhi ya Katavi.
Taarifa iliyotolewa na Mwandishi wa habari msaidizi wa Rais, Premi Kibanga, ilisema taarifa hizo si za kweli na kufafanua kuwa wakati msafara wa Rais ukipita katika hifadhi ya Katavi kutoka Namanyere kwenda Sumbawanga, jiwe lilinasa kwenye rim ya gari na kuanza kusababisha sauti isiyo ya kawaida hali iliyolazimu dereva wa gari ya Rais kusimama na kumhamisha Rais kwenye gari ya ziada ambayo siku zote huwa kwenye msafara kwa ajili ya dharura.
Alisema baada ya hatua hiyo msafara uliendelea na mafundi wa Ikulu walibaki nyuma kushughulikia hitilafu ambayo iligundulika kuwa kwenye tairi ya nyuma upande wa kushoto ili kutoa jiwe lililonasa kwenye rim na kusababisha mlio usio wa kawaida.
Kibanga alisema wakati shughuli hiyo ikiendelea walifika maofisa wa Polisi kutoka Mpanda ili kulinda gari la Rais na walikuta mafundi wakiwa katika shughuli ya kurudishia tairi ambayo ilitolewa kwa ajili ya kutoa jiwe kwenye rim na wala haikuwa pancha kama ilivyoelezwa kwenye taarifa hiyo.
"Napenda kusisitiza kuwa katika hali hiyo hakukuwa na hatari yoyote ya kuweza kuelezewa kuwa Rais amenusurika ajali. Hiyo ni dua mbaya kwa mtu yeyote usiyemtakia au kumtakia mema kwa hali yoyote ile na wala si ustaarabu na heshima kwa kiongozi wako mkuu wa nchi.
Sio kila tukio lolote la kupata pancha au kupata hitilafu ya gari linaweza kuelezewa katika hali kama ilivyoelezewa katika taarifa hiyo ya gazeti la Mtanzania hadi kuleta taharuki na kujengea watu na jamii nzima hofu isiyo na msingi," alisema. Alisisitiza umuhimu wa waandishi wote kupata taarifa za ufafanuzi na za udhibitisho kutoka kwa watu walio na mamlaka ya kufanya kazi hiyo na wala sio kutoka kwa mtu yeyote aliyeyoko serikalini ama Ikulu.
Alisema ni wajibu wa mwandishi wa habari yeyote aliye makini kupata ufafanuzi wa taarifa zozote alizonazo. "Nasikitika kwamba hakuna mwandishi yeyote aliyenitafuta ili nimpe ufafanuzi wa jambo hili, kwa sababu mimi ndiye niliyekupo kwenye msafara wa Rais.
Hili ndiyo jukumu kubwa na la msingi kwa mwandishi au chombo chochote cha habari ili kuondoa mkanganyiko wa maelezo ama taarifa ya matukio muhimu mahali popote."
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Ikulu yakanusha Rais kupata ajali
20th June 2010
Ikulu imekanusha na kufafanua juu ya taarifa iliyotolewa na gazeti moja la kila siku (sio Nipashe) lililoripoti kuwa Rais Jakaya Kikwete amenusurika katika ajali baada ya gari lake kupasuka tairi wakati msafara wake ukipita hifadhi ya Katavi.
Taarifa iliyotolewa na Mwandishi wa habari msaidizi wa Rais, Premi Kibanga, ilisema taarifa hizo si za kweli na kufafanua kuwa wakati msafara wa Rais ukipita katika hifadhi ya Katavi kutoka Namanyere kwenda Sumbawanga, jiwe lilinasa kwenye rim ya gari na kuanza kusababisha sauti isiyo ya kawaida hali iliyolazimu dereva wa gari ya Rais kusimama na kumhamisha Rais kwenye gari ya ziada ambayo siku zote huwa kwenye msafara kwa ajili ya dharura.
Alisema baada ya hatua hiyo msafara uliendelea na mafundi wa Ikulu walibaki nyuma kushughulikia hitilafu ambayo iligundulika kuwa kwenye tairi ya nyuma upande wa kushoto ili kutoa jiwe lililonasa kwenye rim na kusababisha mlio usio wa kawaida.
Kibanga alisema wakati shughuli hiyo ikiendelea walifika maofisa wa Polisi kutoka Mpanda ili kulinda gari la Rais na walikuta mafundi wakiwa katika shughuli ya kurudishia tairi ambayo ilitolewa kwa ajili ya kutoa jiwe kwenye rim na wala haikuwa pancha kama ilivyoelezwa kwenye taarifa hiyo.
"Napenda kusisitiza kuwa katika hali hiyo hakukuwa na hatari yoyote ya kuweza kuelezewa kuwa Rais amenusurika ajali. Hiyo ni dua mbaya kwa mtu yeyote usiyemtakia au kumtakia mema kwa hali yoyote ile na wala si ustaarabu na heshima kwa kiongozi wako mkuu wa nchi.
Sio kila tukio lolote la kupata pancha au kupata hitilafu ya gari linaweza kuelezewa katika hali kama ilivyoelezewa katika taarifa hiyo ya gazeti la Mtanzania hadi kuleta taharuki na kujengea watu na jamii nzima hofu isiyo na msingi," alisema. Alisisitiza umuhimu wa waandishi wote kupata taarifa za ufafanuzi na za udhibitisho kutoka kwa watu walio na mamlaka ya kufanya kazi hiyo na wala sio kutoka kwa mtu yeyote aliyeyoko serikalini ama Ikulu.
Alisema ni wajibu wa mwandishi wa habari yeyote aliye makini kupata ufafanuzi wa taarifa zozote alizonazo. "Nasikitika kwamba hakuna mwandishi yeyote aliyenitafuta ili nimpe ufafanuzi wa jambo hili, kwa sababu mimi ndiye niliyekupo kwenye msafara wa Rais.
Hili ndiyo jukumu kubwa na la msingi kwa mwandishi au chombo chochote cha habari ili kuondoa mkanganyiko wa maelezo ama taarifa ya matukio muhimu mahali popote."
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI