Ikiwa Siku ya sensa hakutakuwa na mapumziko, basi sensa inaweza kuchukua zaidi ya wiki kukamilika

Nobunaga

JF-Expert Member
Mar 22, 2019
1,169
4,986
Kwa mujibu wa Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi, Mama Anna Makinda ametoa tangazo kwamba siku ya sensa, tarehe 23/08/2022 ambayo itakuwa Jumanne, haitakuwa siku ya mapumziko. Haya ni maajabu.
IMG-20220813-WA0030.jpg


Kwa mujibu wa historia ya sensa za miongo miwili iliyopita, inaonesha ili kuwapata watu wote majumbani basi sensa zilifanyika siku za mapumziko yaani Jumamosi na Jumapili.
Mwaka 2002 sensa ilianza kufanyika usiku wa tarehe 24 kuamkia 25 Agosti ambayo ilikuwa ni Jumamosi kuamkia Jumapili. Mwaka 2012 sensa ilifanyika tarehe 26 Agosti ambayo ilikuwa Jumapili.
Cha kushangaza sensa ya mwaka huu 2022, tarehe iliyopangwa ni 23 Agosti ambayo itaangukia siku ya Jumanne, siku ambayo ni ya kazi, na wanasema hakutakuwa na mapumziko.

Hapa bila hata ya kutumia akili za rocket science hawatapata data zote kwa siku hiyo maana wengi watakuwa makazini, na hata wale watakaowakuta majumbani watakuwa na data nusunusu maana wengi watakuwa watoto na wafanyakazi wa majumbani ambao wanajua majina tuu, huenda hata wasijue nyumba wanayoishi ni ya wazazi wao ama ni ya kupanga.

Kwa jinsi nilivyosikia hii sensa inahitaji data nyingi mpaka viwanja na nyumba anazomiliki mtu, namba za NIDA, taarifa za walemavu, taarifa za vifo vya wazazi, taarifa za vifo vitokanavyo na uzazi, nk basi tutegemee hii sensa kuchukua zaidi ya wiki sababu ya kutopatikana kwa watu watakaotoa data zote kwa siku moja.
 
Kwa mujibu wa Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi, Mama Anna Makinda ametoa tangazo kwamba siku ya sensa, tarehe 23/08/2022 ambayo itakuwa Jumanne, haitakuwa siku ya mapumziko. Haya ni maajabu.
View attachment 2322941

NAONA BAADHI YA WATU KUGOMEA HILI ZOEZI NA HATA DATA HAWATAZIPATA ZA KUTOSHA

Mathalani nyumbani ninapokaa wote tunatoka asubuhi na kurudi night kali, hizo data watazipata wapi?
 
NAONA BAADHI YA WATU KUGOMEA HILI ZOEZI NA HATA DATA HAWATAZIPATA ZA KUTOSHA

Mathalani nyumbani ninapokaa wote tunatoka asubuhi na kurudi night kali, hizo data watazipata wapi?
Hii sensa haitakamilika kwa siku 1 abadani.
 
Kwa mujibu wa Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi, Mama Anna Makinda ametoa tangazo kwamba siku ya sensa, tarehe 23/08/2022 ambayo itakuwa Jumanne, haitakuwa siku ya mapumziko. Haya ni maajabu.
View attachment 2322941
Wamekuja kwangu Jana ( wanadai wapo field ) hakika maswali ni mengi sana kama ulivyoainisha hapo juu.

Maswali mengine kwa kweli yanafedhehesha ila ndio vile inabidi utoe ushirikano.

Maswali ya URAIA na malazi au ukaaji nayo yanahitaji uvumilivu kidogo.
 
NAONA BAADHI YA WATU KUGOMEA HILI ZOEZI NA HATA DATA HAWATAZIPATA ZA KUTOSHA

Mathalani nyumbani ninapokaa wote tunatoka asubuhi na kurudi night kali, hizo data watazipata wapi?
Kama utalala hapo atakae kuwepo yeyote lazima atoe taarifa zako kama ni SIRI utapigiwa simu.
 
Mpaka hapo hakutapatikana taarifa Sawa Sawa....

Ingepaswa kuwa siku ya mapumziko.. Na watu washauriwe kukaa majumbani ili kutoa takwimu sahihi...



Sent from my TECNO LA7 using JamiiForums mobile app
Ndicho kilichokuwa kinatakiwa. Huwezi kusema watu waache taarifa zao nyumbani as if ni kitu simple. Hizi ni taaeifa nyeti, huwezi kumuambia dingi amuachie dada wa kazi taarifa zake nyeti kama za nyumba anazomilki, viwanja na mashamba nk.

Kuna baadhi ya taarifa ni private hata mke na mume wanafichana, halafu eti uje useme waziache kwa watakaokuwepo?
 
Kwa mujibu wa Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi, Mama Anna Makinda ametoa tangazo kwamba siku ya sensa, tarehe 23/08/2022 ambayo itakuwa Jumanne, haitakuwa siku ya mapumziko. Haya ni maajabu.
View attachment 2322941

Kwa mujibu wa historia ya sensa za miongo miwili iliyopita, inaonesha ili kuwapata watu wote majumbani basi sensa zilifanyika siku za mapumziko yaani Jumamosi na Jumapili.
Mwaka 2002 sensa ilianza kufanyika usiku wa tarehe 24 kuamkia 25 Agosti ambayo ilikuwa ni Jumamosi kuamkia Jumapili. Mwaka 2012 sensa ilifanyika tarehe 26 Agosti ambayo ilikuwa Jumapili.
Cha kushangaza sensa ya mwaka huu 2022, tarehe iliyopangwa ni 23 Agosti ambayo itaangukia siku ya Jumanne, siku ambayo ni ya kazi, na wanasema hakutakuwa na mapumziko.

Hapa bila hata ya kutumia akili za rocket science hawatapata data zote kwa siku hiyo maana wengi watakuwa makazini, na hata wale watakaowakuta majumbani watakuwa na data nusunusu maana wengi watakuwa watoto na wafanyakazi wa majumbani ambao wanajua majina tuu, huenda hata wasijue nyumba wanayoishi ni ya wazazi wao ama ni ya kupanga.

Kwa jinsi nilivyosikia hii sensa inahitaji data nyingi mpaka viwanja na nyumba anazomiliki mtu, namba za NIDA, taarifa za walemavu, taarifa za vifo vya wazazi, taarifa za vifo vitokanavyo na uzazi, nk basi tutegemee hii sensa kuchukua zaidi ya wiki sababu ya kutopatikana kwa watu watakaotoa data zote kwa siku moja.
Atatoa taarifa kwa nani na kama kuna swali watamuuliza nani na yeye hayupo?Wamechemka.
 
Wamekuja kwangu Jana ( wanadai wapo field ) hakika maswali ni mengi sana kama ulivyoainisha hapo juu.

Maswali mengine kwa kweli yanafedhehesha ila ndio vile inabidi utoe ushirikano.

Maswali ya URAIA na malazi au ukaaji nayo yanahitaji uvumilivu kidogo.
Hivi ilikuwaje mpaka wakapanga tarehe ya sensa ikawa siku ya kazi? Kuna nini hasa hiyo tarehe? Wangeweka iwe weekend kungekuwa na shida gani.
 
Basi nawashauri hao maafisa waweke mabando ya kutosha coz sioni namna gani nitakaa home kusubiria kazi bila malipo. Sitaacha details zozote, wakiona kuna umuhimu watapiga simu.
 
Back
Top Bottom