Nini maana ya #HapaKaziTu ?
Ukisema HapaKaziTu kuna watu watakuuliza unasema hivo mbona hauna ajira? Kazi na ajira ni vitu viwili tofauti ingawa kwa kiasi Fulani vinaweza kufanana kwakuwa kila aliyeajiriwa anafanya kazi lakini si kila afanyae kazi ameajiriwa.
Dhana ya HapaKaziTu inaambatana na uwajibikaji kwenye kila jambo. Ili kuleta maendeleo ya kasi Watanzania tunapaswa kuwa na Rais mwenye uwezo MKUBWA wa kufanya kazi kwa bidii, kujituma kwa moyo wote na uzalendo wa hali ya juu.
Wananchi nao wanapaswa kufanya kazi kwa bidii kwa kuiga mfano wa kiongozi wao. Tunaposema kazi tunakusudia kazi yoyote aifanyayo mtu kama kulima, kujenga, kuongoza watu n.k na wala siyo kuajiriwa tu.
China na Japan zilipata maendeleo makubwa walipoamua kufanya kazi kwa bidii kwenye kilimo, viwanda, uvuvi na hata kwenye utumishi wa umma.
Ili tupate MABADILIKO ya kweli tunahitaji vitu viwili;
1. kiongozi mchapakazi atakayefanya kazi kubwa ya kupambana na MAFISADI wote nchi nzima
2. Raia wanaojituma kweli kweli
Hii ndiyo maana ya kaulimbiu ya #HapaKaziTu , kila mtu atafanya kazi kwa bidii popote alipo kuanzia wanafunzi shuleni, waliojiajiri kwenye miradi yao hadi watumishi wa umma ofisini.
Hakuna asiyehitaji MABADILIKO, lakini mabadiliko ya kweli yatakuja kwa kufanya kazi kwa bidii na kukomesha UFISADI.
Tumchague Dr. John Magufuli tupate MABADILIKO ya kweli kwa kufanya kazi na kujituma
#HapaKaziTu
Ukisema HapaKaziTu kuna watu watakuuliza unasema hivo mbona hauna ajira? Kazi na ajira ni vitu viwili tofauti ingawa kwa kiasi Fulani vinaweza kufanana kwakuwa kila aliyeajiriwa anafanya kazi lakini si kila afanyae kazi ameajiriwa.
Dhana ya HapaKaziTu inaambatana na uwajibikaji kwenye kila jambo. Ili kuleta maendeleo ya kasi Watanzania tunapaswa kuwa na Rais mwenye uwezo MKUBWA wa kufanya kazi kwa bidii, kujituma kwa moyo wote na uzalendo wa hali ya juu.
Wananchi nao wanapaswa kufanya kazi kwa bidii kwa kuiga mfano wa kiongozi wao. Tunaposema kazi tunakusudia kazi yoyote aifanyayo mtu kama kulima, kujenga, kuongoza watu n.k na wala siyo kuajiriwa tu.
China na Japan zilipata maendeleo makubwa walipoamua kufanya kazi kwa bidii kwenye kilimo, viwanda, uvuvi na hata kwenye utumishi wa umma.
Ili tupate MABADILIKO ya kweli tunahitaji vitu viwili;
1. kiongozi mchapakazi atakayefanya kazi kubwa ya kupambana na MAFISADI wote nchi nzima
2. Raia wanaojituma kweli kweli
Hii ndiyo maana ya kaulimbiu ya #HapaKaziTu , kila mtu atafanya kazi kwa bidii popote alipo kuanzia wanafunzi shuleni, waliojiajiri kwenye miradi yao hadi watumishi wa umma ofisini.
Hakuna asiyehitaji MABADILIKO, lakini mabadiliko ya kweli yatakuja kwa kufanya kazi kwa bidii na kukomesha UFISADI.
Tumchague Dr. John Magufuli tupate MABADILIKO ya kweli kwa kufanya kazi na kujituma
#HapaKaziTu