Nyakijooga
Senior Member
- Dec 9, 2018
- 123
- 202
Moja ya Sheria ya Jeshi la Polisi ni kuwa ikibainika Askari Polisi ametembea au ameingilia uhusiano wa mke wa mtu iwe ni Askari mwenzake au raia na uthibitisho ukapatikana bila kupepesa macho ajira yake ndio inakuwa imeishia hapohapo.
Kuna kesi kadhaa nyingi ambazo zimetokea siku za nyuma na hatua kali zikachukuliwa, nasema hayo kwa kuwa ninajua ninachokisema kwa sababu ni mmoja wa washiriki katika Idara hiyo ya Ulinzi (nadhani utakuwa umenielewa).
Kuna huyu bwana ni Mkuu wa Kituo cha Polisi – Tegeta ndani ya Dar es Salaam.
Kwa muda mrefu amekuwa ni mmoja wa watu ambao wamekuwa wasumbufu katika majukumu yao, ananyanyasa Watumishi walio chini yake kwa kutumia cheo chake.
Amekuwa akitumia vibaya madaraka yake, mfano amekuwa akiwatuma Askari wake kwa lazima kwenda kwenye mambo yake binafsi, wakikataa anaanza kuwafanyia figisu au anakuja juu.
Askari hawapendi na hawafurahishwi na kinachofanywa na bosi wao lakini kwa kuwa Sheria ya Jeshi ni kutii amri, hawana jinsi.
Kibaya zaidi ambacho kinatuuma ni tabia yake ya kutengeneza mazingira ya kutongoza na kuwa na uhusiano na wake za watu, hili linaweza kuonekana ni jambo binafsi au majungu lakini kwa kuwa lipo kinyume na Maadili ya kazi yake nimeamua kulisema.
Namuomba Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Camillius Wambura atumie watu wake au mbinu zake amchunguze huyu Mkuu wa Kituo, ili kama haya ninayoandika hapa ni majungu basi ayapotezee na kama ni kweli hatua zichukuliwe.
Kuna mengi ambayo anayafanya huyu Afande na yapo kinyume kabisa na suala la Utawala Bora.
Kama hatua hazitachukuliwa dhidi ya Kiongozi huyu nitarejea na kuweka picha na jina lake wazi ili Watanzania wamjue, japo najua kwa wasifu huo nilioutaja tayari mamlaka zitakuwa zimeshamjua ni nani.
Lengo langu si kumchafua bali ni kutaka Mamlaka zichukue hatua ili kuwa na utawala bora na uwajibikaji kwenye Jeshi letu la Polisi, sio kama huyu bwana anavyofanya, nimeamua kumstahi japo kidogo kuhusu kuweka wazi sura na jina lake.
Kuna kesi kadhaa nyingi ambazo zimetokea siku za nyuma na hatua kali zikachukuliwa, nasema hayo kwa kuwa ninajua ninachokisema kwa sababu ni mmoja wa washiriki katika Idara hiyo ya Ulinzi (nadhani utakuwa umenielewa).
Kuna huyu bwana ni Mkuu wa Kituo cha Polisi – Tegeta ndani ya Dar es Salaam.
Kwa muda mrefu amekuwa ni mmoja wa watu ambao wamekuwa wasumbufu katika majukumu yao, ananyanyasa Watumishi walio chini yake kwa kutumia cheo chake.
Amekuwa akitumia vibaya madaraka yake, mfano amekuwa akiwatuma Askari wake kwa lazima kwenda kwenye mambo yake binafsi, wakikataa anaanza kuwafanyia figisu au anakuja juu.
Askari hawapendi na hawafurahishwi na kinachofanywa na bosi wao lakini kwa kuwa Sheria ya Jeshi ni kutii amri, hawana jinsi.
Kibaya zaidi ambacho kinatuuma ni tabia yake ya kutengeneza mazingira ya kutongoza na kuwa na uhusiano na wake za watu, hili linaweza kuonekana ni jambo binafsi au majungu lakini kwa kuwa lipo kinyume na Maadili ya kazi yake nimeamua kulisema.
Namuomba Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Camillius Wambura atumie watu wake au mbinu zake amchunguze huyu Mkuu wa Kituo, ili kama haya ninayoandika hapa ni majungu basi ayapotezee na kama ni kweli hatua zichukuliwe.
Kuna mengi ambayo anayafanya huyu Afande na yapo kinyume kabisa na suala la Utawala Bora.
Kama hatua hazitachukuliwa dhidi ya Kiongozi huyu nitarejea na kuweka picha na jina lake wazi ili Watanzania wamjue, japo najua kwa wasifu huo nilioutaja tayari mamlaka zitakuwa zimeshamjua ni nani.
Lengo langu si kumchafua bali ni kutaka Mamlaka zichukue hatua ili kuwa na utawala bora na uwajibikaji kwenye Jeshi letu la Polisi, sio kama huyu bwana anavyofanya, nimeamua kumstahi japo kidogo kuhusu kuweka wazi sura na jina lake.