Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Akizungumza leo Agosti 11, 2025, katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa maafisa waandamizi wa Jeshi la Polisi uliofanyika katika shule ya Polisi Moshi, Inspekta Jenerali wa Polisi, Camillus Wambura ameeleza kuwa hali ya usalama ni shwari na Jeshi hilo linajiandaa na uchaguzi kwa kuweka mikakati.
"Shughuli yoyote kubwa na muhimu ni lazima iwe na mipango mahususi, lazima iwe na mipango iliyopangiliwa kwajili ya kwenda kutimiza shughuli hiyo kwa umakini mkubwa, kwa kawaida hakuna vita inayopiganwa kwenye uwanja wa mapambano," alieleza IGP Wambura katika shughuli hiyo ambayo Makamu wa Rais Philip Mpango alikuwa mgeni rasmi.
"Vita yote hupiganwa mezani na pale mezani ndipo mikakati hupangwa na pale mezani miongoni mwa mikakati inayopangwa ni kubaini nguvu ya adui ,kubaini vifaa anavyotumia adui, iliujue Je? wewe unahitajika Kwenda na AK-47 au unahitajika Kwenda na mizinga au kwenda na aina gani ya silaha lakini ni vizuri kujua idadi ya askari alionao adui na utakapofika vitani ni utekelezaji wa mikakati ulikwisha kujiwekea," anendelea kufafanua IGP Wambura.
"Hatuendi vitani lakini tunakwenda kusimamia usalama, amani, utulivu wa taifa letu kabla, wakati na baada ya uchaguzi," alisisitiza Wambura.
"Shughuli yoyote kubwa na muhimu ni lazima iwe na mipango mahususi, lazima iwe na mipango iliyopangiliwa kwajili ya kwenda kutimiza shughuli hiyo kwa umakini mkubwa, kwa kawaida hakuna vita inayopiganwa kwenye uwanja wa mapambano," alieleza IGP Wambura katika shughuli hiyo ambayo Makamu wa Rais Philip Mpango alikuwa mgeni rasmi.
"Vita yote hupiganwa mezani na pale mezani ndipo mikakati hupangwa na pale mezani miongoni mwa mikakati inayopangwa ni kubaini nguvu ya adui ,kubaini vifaa anavyotumia adui, iliujue Je? wewe unahitajika Kwenda na AK-47 au unahitajika Kwenda na mizinga au kwenda na aina gani ya silaha lakini ni vizuri kujua idadi ya askari alionao adui na utakapofika vitani ni utekelezaji wa mikakati ulikwisha kujiwekea," anendelea kufafanua IGP Wambura.
"Hatuendi vitani lakini tunakwenda kusimamia usalama, amani, utulivu wa taifa letu kabla, wakati na baada ya uchaguzi," alisisitiza Wambura.