kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 200
WanaJF,
Kuibiwa kwa upanga wa dhahabu aliokuwa amekabidhiwa IGP Mwema kuashiria uongozi wake wa muda,ambao ni mali ya shirikisho la wakuu wa majeshi ya polisi wa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO),kumelifedhehesha na kuliaibisha Taifa!
Kutokana na uzembe uliosababisha kuibiwa kwa upanga huo wenye thamani kubwa inayokadiriwa kufikia shilingi milioni 600 za kitanzania,IGP Mwema hana budi kuwajibika kwa kung'atuka madarakani bila shuruti yoyote!
Yeye kama kamanda mkuu anastahili kuoyesha mfano katika kukabiliana na adui ambaye ni uzembe,rushwa na wizi uliokithiri katika jeshi la polisi nchini na kuwapa changamoto wanaobaki nyuma yake kwani cheo ni dhamana!
Swali:Ni nani anayeweza kuingia ofisini kwa IGP Mwema akaiba Laptop yenye mambo nyeti au upanga wa dhahabu unaotakiwa kulindwa masaa 24 na kutoka bila kukamatwa?
Kuibiwa kwa upanga wa dhahabu aliokuwa amekabidhiwa IGP Mwema kuashiria uongozi wake wa muda,ambao ni mali ya shirikisho la wakuu wa majeshi ya polisi wa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO),kumelifedhehesha na kuliaibisha Taifa!
Kutokana na uzembe uliosababisha kuibiwa kwa upanga huo wenye thamani kubwa inayokadiriwa kufikia shilingi milioni 600 za kitanzania,IGP Mwema hana budi kuwajibika kwa kung'atuka madarakani bila shuruti yoyote!
Yeye kama kamanda mkuu anastahili kuoyesha mfano katika kukabiliana na adui ambaye ni uzembe,rushwa na wizi uliokithiri katika jeshi la polisi nchini na kuwapa changamoto wanaobaki nyuma yake kwani cheo ni dhamana!
Swali:Ni nani anayeweza kuingia ofisini kwa IGP Mwema akaiba Laptop yenye mambo nyeti au upanga wa dhahabu unaotakiwa kulindwa masaa 24 na kutoka bila kukamatwa?