IGP Mangu: Lugumi ilitekeleza mkataba wake na Jeshi la Polisi

Ni uzwazwa tu kuanza kujikosha leo wakati tayari timu ya kamati ya Bunge ipo kazini...subirini sindano iwaingie
 
Na wapi mtu huyo ana historia ya kazi kama hizo? Kilitafutwa kigezo cha ugaidi ili kuhalalisha uharaka wa kupeana ulaji. minyoo kasema inatafutwa skendo kutuondoa hapa.

Ninachoshangaa watuambuaji hapa wamekwama! Tunasikia ripoti za kwingine hapa ngoma muzito

Tulisema kuanzia awali, zile kimbia kimbia tupiana mpira n.k. ni mbinu tu za kuvuta muda mafaili yakae uzuri. Kwa bahati mbaya au nzuri taarifa zilishafikia vyombo vya habari na sasa wanabaki kubabaika tu

Hili la Lugumi lita define mapambano dhidi ya rushwa! likifunikwa basi tuendelee na utamaduni wetu wa kawaida. Washangiliaji wote mbio! hakuna anayekuja kujibu hoja
MsemajiUkweli tuambie ukweli. Simiyu Yetu hiliunalisemaje maana limenata na litaibuka kila asubuhi
Nguruvi3
Nilishakuambia mimi siwezi kuanza kujadili masuala ambayo sina uhakika nayo kwa sababu mimi siyo mwanaharakati ambaye moja ya tabia zao ni kuongea sana bila kuwa na balanced opinion and without concrete fact.

Hizi hoja za kusema suala la Lugumi lita-define mapambano ya Rais Magufuli dhidi ya rusha ni hisia zako tu kama ulivyo ujenzi wa hoja zako zenye msingi wa hisia.

Ni wewe toka siku ya kwanza ya Magufuli kuwa Rais wa Tanzania ulisema hana jipya lakini ninashangaa kwa sasa hoja zako unajenga mazingira kuwa hili suala ndiyo benchmark na litatoa mwerekeo wa Rais Magufuli. Hii inaonyesha huna hata msimamo kifikra kuhusu utawala wa Rais Magufuli au kwa maana nyingine, unahamisha magori ya kisiasa kila mara kulingana na mazingira na hisia zako.

Kila siku ninasema ukweli hauwezi kufichwa bali unaweza kucheleweshwa tu. Tunafahamu kwa sasa kuna Kamati ndogo ya bunge inatafuta ukweli kama umefichwa na baada ya wiki nne tutafahamu.

Kuanza kujadili na kutoa hukumu kwa suala ambalo tutapata ukweli baada ya wiki nne ni kupoteza muda au kufurahisha genge la Jamiiforums.

Lugumi au polisi kama watakuwa wameficha ukweli watastahili kuwajibishwa lakini pia tujiandae kuupokea ukweli kutoka kwenye kamati ndogo.

Ninafahamu kama ukweli utaletwa tofauti na jinsi baadhi ya watu walivyohukumu, kuna wengine wataanza kuukataa na kusema umepikwa.

Tuiache Kamati Ndogo ya Bunge ifanye kazi, Wiki nne siyo mbali.
 
Nguruvi3
Nilishakuambia mimi siwezi kuanza kujadili masuala ambayo sina uhakika nayo kwa sababu mimi siyo mwanaharakati ambaye moja ya tabia zao ni kuongea sana bila kuwa na balanced opinion and without concrete fact.

Hizi hoja za kusema suala la Lugumi lita-define mapambano ya Rais Magufuli dhidi ya rusha ni hisia zako tu kama ulivyo ujenzi wa hoja zako zenye msingi wa hisia.

Ni wewe toka siku ya kwanza ya Magufuli kuwa Rais wa Tanzania ulisema hana jipya lakini ninashangaa kwa sasa hoja zako unajenga mazingira kuwa hili suala ndiyo benchmark na litatoa mwerekeo wa Rais Magufuli. Hii inaonyesha huna hata msimamo kifikra kuhusu utawala wa Rais Magufuli au kwa maana nyingine, unahamisha magori ya kisiasa kila mara kulingana na mazingira na hisia zako.

Kila siku ninasema ukweli hauwezi kufichwa bali unaweza kucheleweshwa tu. Tunafahamu kwa sasa kuna Kamati ndogo ya bunge inatafuta ukweli kama umefichwa na baada ya wiki nne tutafahamu.

Kuanza kujadili na kutoa hukumu kwa suala ambalo tutapata ukweli baada ya wiki nne ni kupoteza muda au kufurahisha genge la Jamiiforums.

Lugumi au polisi kama watakuwa wameficha ukweli watastahili kuwajibishwa lakini pia tujiandae kuupokea ukweli kutoka kwenye kamati ndogo.

Ninafahamu kama ukweli utaletwa tofauti na jinsi baadhi ya watu walivyohukumu, kuna wengine wataanza kuukataa na kusema umepikwa.

Tuiache Kamati Ndogo ya Bunge ifanye kazi, Wiki nne siyo mbali.
Well, huenda nina hisia lakini kila mara hisia hizo hudhihirika kuwa kweli. Sijatoa hukumu kwa hili swala, naomba niweke rekodi sawa.

Nilichosema kuna kuficha ficha na kusita kulishughulikia.
Nadhani nimekuonyesha jinsi ambavyo ubabaishaji unavyoendelea na kujikanganya.

Hatuelewi nani mwenye dhamana na suala hili, mara tunasikia PCCB mara kamati ya bunge.
IGP anasema hakuna shida, kamati ya ulinzi na usalama inapokea nyaraka ambazo ilisema ni mkataba, bunge linasema ni maelezo ya kina.Hapo sina shaka na hisia zangu na nitasimama nazo

Kuhusu serikali hii, ni kweli kuanzia mwanzo nilisema hayo tena niongezee nilichosema '' Huwezi kupata kondoo mzuri kutoka genge la fisi' Ninasimama na hilo. CCM ni ile ile na watu wale wale katika mfumo ule ule na hapa tunaona wa kulindana

Kuna bandiko niliwahi kuandika katika uzi huu
Duru za Siasa: Awamu ya 5 - Uongozi na Yanayojiri... bandiko 83/106/107 na mengineyo ynayohusiana kama yale ya ZNZ na Umeya n.k.

Nikasema nia na dhamira ni vitu viwili tofauti.

Nia ni haja na matamanio, dhamira ni uthubutu wa kutenda yale ya nia.
Sidhani kama hisia hizo zilikuwa za uongo

Hii habari ya kusema tuachie muda fulani ni kukwepa ukweli.
Ukweli si tuhuma, ni kueleza kile kilicho cha kweli.

Nasema hili lita define utawala wake na mapambano ya rushwa kwasababu ikiwemo double standard basi kila kitu kitakuwa kwa mwendo huo.

Na washangiliaji kama ninyi mtashindwa mahala pa kusimama na kumwacha mzee mwenyewe.
Tutafeli kama Taifa
 
Lugumi kaiweka serikali na Bunge mfukoni kupitia kitwanga ambaye yupo Dodoma anahaha usiku na mchana kuwapoza wabunge wasimwandame akatumbuliwa.
 
Hela kubwa imeshapigwa hapa sasa wanahangaika kuficha dhambi zao kwa kukingiana vifua. Haiwezekani kabisa mkataba wa pesa nyingi kiasi hiki usainiwe ndani ya siku moja tu bila kuwepo wengine waliotuma maombi yao ya kuomba kupewa kazi hiyo. Wako busy kuhalalisha kwamba kazi imefanyika bila kujali je mkataba alipewa kihalali? Je, taratibu za mikataba ndani ya taasisi za Serikali zilifuatwa? Je, taratibu za malipo Serikalini zilifuatwa? Hiyo kazi ilifanywa katika viwango vinavyokubalika?
....

....Hela KUBWA
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mkuu siku nyingine Sterling haguswi maana huwa ni tajiri mkubwa sana nchini na akiguswa tu basi nchi itawaka moto au inaweza kabisa kupotea katika uso wa dunia. Nadhani unamkumbuka yule Sterling maarufu wa Eskrooo
ambaye baada ya kuchota mapesa yake chungu nzima na kugawa rushwa ya hali ya juu mpaka Bungeni hadi ndani ya Ikulu hakuna wa kumgusa wenyewe hupenda kumuita Tajri Ruge.

Hapo sterling ataishia ukonga tu
 
Rudi kasome tena IT. Mawasiliano ya Mwanza na kituo kikuu Dar yatafanyika kwa LAN?
Tatizo unataka kujikweza tu huna IT yoyote ulichosoma ni historia ya IT.



Kuchukua alama za vidole na vitu kama hivyo kama DNA haitaji any connectivity zaidi ya equipment za sehemu husika....analysis yake ndo inaweza kuhitaji connectivity na server ku fetch na compare na saved data.

Anyway kama hii ilikuwa ndio mradi ulivyotakiwa kuwa(Synchronized System) maana yake mradi haujakamilika na jamaa wamelipwa pesa yote. Ndio maana ni muhimu kujua mkataba ulikuwaje internet ilikuwa sehemu ya SOW au ni contractor mwingine alikuwa anafanya?
 
Well, huenda nina hisia lakini kila mara hisia hizo hudhihirika kuwa kweli. Sijatoa hukumu kwa hili swala, naomba niweke rekodi sawa.

Nilichosema kuna kuficha ficha na kusita kulishughulikia.
Nadhani nimekuonyesha jinsi ambavyo ubabaishaji unavyoendelea na kujikanganya.
Tofauti yangu na wewe kuhusu kwa hili suala ni moja. Wewe unajenga hoja kwa kutumia msingi wa nadharia, Mimi ninajenga hoja kwa kutumia msingi wa uharisia.

Ni nani unadhani anaficha ficha na kusita kulishughurikia wakati kwa sasa kuna Kamati Ndogo ya Bunge inalishughurikia. Au ulitaka PAC/Bunge wafanye kazi kulingana na matakwa yako?

Kwanza ieleweke kuwa, kama isingekuwa PAC, hata hisia zako zisingewepo kwa sababu usingefahamu kama kuna mkataba ambao unahitaji clarification kutoka polisi. Kwa msingi huu, siwezi pia kushangaa kama utakataa matokeo ya uchunguzi wa mkataba kutoka kwenye chombo kilichotaka majibu kuhusiana na mkataba ambacho ni PAC.

Nimesema na ninaendelea kusema, tuache Kamati Ndogo ya Bunge ifanye kazi zake labda kama hatuiamini.

Hatuelewi nani mwenye dhamana na suala hili, mara tunasikia PCCB mara kamati ya bunge.
IGP anasema hakuna shida, kamati ya ulinzi na usalama inapokea nyaraka ambazo ilisema ni mkataba, bunge linasema ni maelezo ya kina.Hapo sina shaka na hisia zangu na nitasimama nazo
Sasa kama huelewi mwenye dhamana na suala hili, kwa nini unasema kuna kuficha ficha.

Kwa kukusaidia kupitia tamko rasmi la Bunge ni kuwa, mwenye dhamana na suala hili ni Bunge kupitia kamati yake ya PAC. Bunge ni taasisi yenye vitengo rasmi vya mawasiliano. kuchukua maandishi kutoka kwenye Magazeti au mitandao na kuyafanya ni maelezo ya Bunge inakuwa ni kununua udaku.

Tumesikia matamko rasmi ya bunge kuhusiana na suala hili na katika matamko hayo ndiyo inapaswa tujenge hoja. Kinyume chake itakuwa tunajenga hoja kwa kutumia hisia. Ndiyo maana nimekuambia, wiki nne siyo mbali, tusubiri ukweli utufikie kutoka kwenye chombo kilichopewa kazi kisheria ambacho ni Kamati Ndogo ya Bunge.

Kuhusu serikali hii, ni kweli kuanzia mwanzo nilisema hayo tena niongezee nilichosema '' Huwezi kupata kondoo mzuri kutoka genge la fisi' Ninasimama na hilo. CCM ni ile ile na watu wale wale katika mfumo ule ule na hapa tunaona wa kulindana
Sasa kama ulishahitimisha fikra zako kuhusiana na utendaji wa Serikali, kwa nini unahangaika na masuala ambayo ulishayafahamu?

Mtu mwenye hekima na busara angekaa chini na kusubiri utawala mwingine baada ya 2020 kwa sababu anafahamu huu utawala hauna jipya. Watu kama mimi tungebaki na matumaini yetu kwa sababu tunaamini we are at war with the army we have (Rais Magufuli), not the army you might want or wish to have at your irrational thoughts and ideas!

Kuendelea kukosoa serikali uliyosema toka siku ya kwanza haina jipya huku umejificha katika vazi la uzalendo ni kuendeleza unafiki tu au kupoteza muda wako adhimu.

Hii habari ya kusema tuachie muda fulani ni kukwepa ukweli.
Ukweli si tuhuma, ni kueleza kile kilicho cha kweli.
Utakielezaje kilicho cha kweli bila ukweli? Ukweli wa Mkataba wanaofahamu ni polisi na Lugumu.

Kwa hiyo unataka kutuambia unafahamu yote kuhusiana na mkataba wa polisi na Lugumi?

Ndiyo maana nimekuambia, achana na hisia katika suala ambalo ukweli wake upo na baada ya wiki nne tutaupata.

Nasema hili lita define utawala wake na mapambano ya rushwa kwasababu ikiwemo double standard basi kila kitu kitakuwa kwa mwendo huo.

Na washangiliaji kama ninyi mtashindwa mahala pa kusimama na kumwacha mzee mwenyewe.
Tutafeli kama Taifa
Huu ni mtazamo wako ambao hauwezi kuwa ni sheria au mwanvuli kwa kila mwananchi.

Achana na hoja za ramli katika masuala ambayo kila mtu ana mtazamo wake. Eti tutashindwa mahala pa kusimama. Huoni kama kusema tutashindwa pa kusimama ina maana kuwa kwa sasa tuna mahali pa kusimama au kwa maana nyingine unasema, The President is doing fantastic job.

Kama mimi ni mshangiliaji, wewe ni nani?
 
Wewe Mangu tunakusubiri uingie kwenye 12 za Magufuli utupwe nje.
Kamanda mzima hujui hata kujenga hoja ya uongo ipendeze, unasema havifanyi kazi kwa sababu hakuna internet.

Kama internet haipo waliharibuje kodi yetu kuweka madhine hizo huku wakijua havitafanya kazi, njoo kanda ya kaskazini nikuonyeshe vituo vitatu vya wilaya vyenye internet lakini mimashine hiyo imeanza kuliwa kutu kabla ya kufanya kazi.
 
Mimi ni IT proffesional na sizdhani kama hizo biometric system ili zifanye kazi zinahitaji internet connection wala sio kweli Mangu anaongea mambo asiyo yajua. Only LOcal area network inahitajika kwenye hiyo system. Anajaribu kutetea uovu huyu Mangu
Si kwamba anaongea asiyoyajua, anajua kila kitu mwache aingize kitanzi shingoni.
 
"
MsemajiUkweli, post: 16008019, member: 91662"] Wewe unajenga hoja kwa kutumia msingi wa nadharia, Mimi ninajenga hoja kwa kutumia msingi wa uharisia.
Sidhani unatumia uhalisia, vinginevyo usingebabaika ukihamisha magoli kila asubuhi. Hujaeleza 'uhalisia' wa bunge kusema abcd, kamati zake efg, serikali hjk n.k.

utakumbuka ulisema 'hili suala lina utata sana, ndio uhalisia huo?
Ni nani unadhani anaficha ficha na kusita kulishughuliki, Kamati Ndogo ya Bunge inalishughurikia
Alaa, si ulisema ni la kamati ya ulinzi na usalama na mambo ya nje?

Hiyo ni baada ya kusema serikali inalishughulikia!
kama isingekuwa PAC,hisia zako zisingewepo,usingefahamu kuna mkataba unaohitaji clarification kutoka polisi.
PAC
.Kwakweli sikujua kama kuna mauza uza hayo, nadhani Watanzania wengi hawakaaujua ikiwemo PAC na PCCB. Wangalijua uchunguzi usingehitajika.

Kutojua ni sababu ya kutouliza? Niliwahi kusema katika uzi niliokupa, Tatizo la Watanzania ni watu wa kumeza, kuhoji ni 'uhalifu' na kukosa uzalendo kama CCM wanavyosema.

Kwamba, kukaa kimya ndio uzalendo uliotukuka, tena wakishangilia hata makosa!
Tuache Kamati Ndogo ya Bunge ifanye kazi zake labda kama hatuiamini
Ulisema tuache kamati ya ulinzi na usalama ifanye kazi zake
Sasa kama huelewi mwenye dhamana , kwa nini unasema kuna kuficha ficha.
Kwasababu kila mmoja anakimbia ! ndio msingi wa kusema hakuna anayechukua dhamana. Sidhani kama unaweza kunieleza
Kupitia tamko rasmi la Bunge mwenye dhamana ni Bunge kupitia PAC. Bunge ni taasisi mawasiliano.

kuchukua maandishi kutoka kwenye Magazeti au mitandao na kuyafanya ni maelezo ya Bunge inakuwa ni kununua udaku.
Ni kweli kabisa, lakini mawasiliano gani ikiwa hawakuweza kueleza tofauti ya mkataba na maelezo ya kina.

Kitu kinachoitwa maelezo ya kina kinasemwajwe kwa neno moja?

Mwasiliano yalikuwa wapi hadi kamati ya PAC ikaenda kudai mbele ya vyombo vya habari?
Nimekuambia, wiki nne siyo mbali, tusubiri ukweli utufikie kutoka kwenye chombo kilichopewa kazi kisheria ambacho ni Kamati Ndogo ya Bunge.
OK si kamati ya ulinzi , usalama na mambo ya nje? Si PCCB? Si serikali?
Sasa kama ulishahitimisha fikra zako kuhusiana na utendaji wa Serikali, kwa nini unahangaika na masuala ambayo ulishayafahamu?
Ili kukabiliana na washangiliaji wanaopotosha umma, wanaotaka umma uamini mambo safi, wanaosema uongo.

Ni kosa kukaa kimya umma ukibababishwa kwa mapambio ukweli ukifichwa
Mtu mwenye hekima na busara angesubiri baada ya 2020 kwa sababu anafahamu huu utawala hauna jipya.

Watu kama mimi tungebaki na matumaini yetu kwa sababu tunaamini we are at war with the army we have (Rais Magufuli), not the army you might want or wish to have at your irrational thoughts and ideas!
Nani kaukupoka matumaini mkuu? Endelea na matumaini wala usiahangaike na watu kama sisi. Jenga matumaini kwa nafsi na nafasi yako. Ni haki yako kikatiba na kibainadamu. Kuishi kwa matumaini hata kama ni mkate wa mawe! Hapa unatusingizia kufifisha matumaini yako! Si kweli. Kazi uzi mkuu

Well, 2005 walikuwa na matumaini kama wewe!
Mwaka jana wengine wakasema hali ya nchi ni njema kuelekea uchumi wa kati.

Mwaka huu wakasema hali ilifika pabaya sana
Wanaweza kusema hayo kwasababu wakipiga zumari wanaoitikia wengi hata kama hawajui wimbo wa zumari.

Wengine tunasema hapana, si suala la 'vita' tu, bali majemadari wa vita,nia , dhamira na mkakati. Vita haipiganwi kwa kubeba magobole na kwenda kichakani tu

Jeshi lililoshindwa miaka 20 na majemadari wale wale ni unlikely linaweza kuja na kitu kipya. Tatizo letu si vita, ni ni nia na dhamira ya vita, wapiganaji na mkakati

Jambo zuri ndani ya hekma zako huwezi kujibu hoja. Mimi nitasimama katika hoja nikiamini njia bora na matumizi sahihi ya ubongo ni kufikiri, kuhoji na kutaka kuelewa.
Kuendelea kukosoa serikali uliyosema toka siku ya kwanza haina jipya huku umejificha katika vazi la uzalendo ni kuendeleza unafiki tu au kupoteza muda wako adhimu.
Hapana suala la muda ni jambo binafsi na sioni linajibu vipi Lugumi.

Wengine tunasimama na Taifa kwanza kabla ya mtu au watu.

Kama kuhoji, kutoa maoni ni unafiki naafiki niwe hivyo na hakika najivunia hilo kuliko kujificha katika tumbo nikijua masilahi mapana ya Taifa yapo matatani
Ukweli wa Mkataba wanaofahamu ni polisi na Lugumu.
Hewalaa, ni mkataba wa umma, penye utata nini kinafichwa? Halafu una uhakika gani kama Polisi wanao?

Kwani kazi ilitolewa na nani? Nani mlipaji ? Mkataba ulisemaje kuhusu vifaa? tenda ilipatikanaje? Nani walishiriki?
Kwa hiyo unataka kutuambia unafahamu yote kuhusiana na mkataba wa polisi na Lugumi?
Sijui kabisa, ndio maana nashangaa kwanini mwezi mzima kuna kutupiana mpira, na baada ya wiki takribani tatu 'mwenye makataba' kwa mujibu wako anakuja na maswali badala ya majibu?

Unanunuaje kifaa eneo lisilo na internet?
Nani ali plan huu mradi? Nani aliidhinisha mradi huo? Wataalam gani walishiriki?
Kumbuka kama mlipa kodi na mwajiri wa serikali nina haki ya kuuliza
Huu

ni mtazamo wako ambao hauwezi kuwa ni sheria au mwanvuli kwa kila mwananchi.
Wapi mtazamo waangu nimeuita sharia au mwamvuli kwa wananchi?
Eti tutashindwa mahala pa kusimama. Huoni kama kusema tutashindwa pa kusimama ina maana kuwa kwa sasa tuna mahali pa kusimama au kwa maana nyingine unasema, The President is doing fantastic job.
Bandarini chereko, TRA chereko, Darajani kicheko, wafanyakazi hewa nderemo. Lugumi kimyaaa!

Lugumi imepelekwa ligi daraja la pili.
Ndio maana tunasema double std ni dalili njema za mbio kufikia ukingoni

Si kwa mujibu wa kauli zangu, bali wananchi wana akili za kupambanua
Kama mimi ni mshangiliaji, wewe ni nani?
Mimi jinga Fulani linalohoji mambo yasitokiwa. Nafiki Fulani lisilokubali kuimba wengine wakiserebuka.
Na puuzi Fulani lani tu linalotaka kudadisi dadisi kila kitu

Mkuu hoja zinajibiwa kwa hoja, nashangaa siku zote umekataa lugha tashtiti , mambo yakielemea unanyua silaha hiyo ambayo ni rahisi kuitumia. Haihitaji elimu au fikra

Huko siendi, lakini sitasita kutoa maoni hata kama yanachoma! au ungeshaurije mkuu!
 
Kuchukua alama za vidole na vitu kama hivyo kama DNA haitaji any connectivity zaidi ya equipment za sehemu husika....analysis yake ndo inaweza kuhitaji connectivity na server ku fetch na compare na saved data.

Anyway kama hii ilikuwa ndio mradi ulivyotakiwa kuwa(Synchronized System) maana yake mradi haujakamilika na jamaa wamelipwa pesa yote. Ndio maana ni muhimu kujua mkataba ulikuwaje internet ilikuwa sehemu ya SOW au ni contractor mwingine alikuwa anafanya?
Network inaonyesha Kama alishawahi ku commit crime kwengine etc.
 
Shida iliyopo katika suala la Lugumi ni kwamba Kuna wanasiasa wameligeuza kuwa driving force yao wakati ufafanuzi umekwisha wekwa wazi na wahusika
 
Kuchukua alama za vidole na vitu kama hivyo kama DNA haitaji any connectivity zaidi ya equipment za sehemu husika....analysis yake ndo inaweza kuhitaji connectivity na server ku fetch na compare na saved data.

Anyway kama hii ilikuwa ndio mradi ulivyotakiwa kuwa(Synchronized System) maana yake mradi haujakamilika na jamaa wamelipwa pesa yote. Ndio maana ni muhimu kujua mkataba ulikuwaje internet ilikuwa sehemu ya SOW au ni contractor mwingine alikuwa anafanya?
Ndio maana hawajamaliza kulipwa pia. Hakuna haja ya kuwa na kihelehele cha kushusha tuhuma nyingi wakati kamati itatujuza chamno ni nini kilichofanya swala hili kuchukua msukumo mkubwa kutoka kwa wanahabari.
Kuweni makini sana na wanahabari maana kuna mwaka walisababisha watu wengi kufa na wengine afya kuteteleka pale walipowashawishi watu kwenda Samunge
 
Back
Top Bottom