Ifikie mahali Serikali ipige marufuku askari trafiki kusimamisha gari ili kutafuta kosa, huo ni unyanyasaji

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Labda ni Tanzania pekee ambako kila siku askari wanasimamisha gari ili watafute kosa kuhusu wewe dereva au gari. Ni kwamba askari anapoamua kusimamisha gari, dereva unakuwa huna kosa aliloona, bali utakaposimama ndio ataanza kutafuta kosa ambalo atakuambia ulilipie faini. Naendesha gari, nafuata kila sheria, gari yangi nzima, halafu unanisimamisha ili unitafutie kosa, kwa nini? Una chuki gani na mimi?

Huu ni uratibu mbaya na haufai, na unakuwa mbaya zaidi pale ambapo unafanywa kama jambo la kawaida la kila siku. Ikiwa huu utaratibu wa kusimamisha gari ili kutafuta kosa ungefanywa wiki ya "Nenda kwa Usalama" wala tusingeona shida. Lakini sasa, kwa nini jeshi la polisi limeamua kwamba haya ndiyo yatakuwa maisha ya kila siku ya wanaoendesha magari?

Je lengo ni nini hasa? NI kwamba serikali imefulia au kufilisika kabisa kiasi kwamba Raisi ametoa agizo kwamba askari watafute hela kwa kuwasumbua wananchi kiasi hiki? Je Raisi au mawaziri hawaoni hii ni kero kwa wananchi kwa kuwa wao hawaguswi na kadhia hii? Ni sawa na Ni sawa na kutembelea Ofisi za TRA na kuwauliza wafanyakazi kama wamepokea rushwa ili uwachukulie hatua!

Kwa nini lakini Raisi Magufuli anaifanya Tanzania kuwa nchi yenye kero na usumbufu usio na msingi? Ana hasira ya kuchaguliwa kuwa Raisi?

Basi sisi kama wananchi tuna ujumbe kwa Raisi Magufuli. Tunaelewa kwamba usalama barabarani ni jambo muhimu, lakini huu usumbufu sio wa lazima ni kero ambayo tusingependa kuwa nayo katika nchi yetu huru. Kama askari wa trafiki wanataka kukaa barabarani basi wasimamishe gari ambazo zinakuwa zimefanya kosa fulani. Sio kunisimamisha ili uanze kutafuta kwa kila namna kosa la kunipigia faini. Huu ni ukandamizaji na unyanyasaji (opression and harassment) ndani ya nchi yetu wenyewe unaopaswa kupingwa kwa nguvu zote na wananchi huru wa Tanzania.
 
Wanafanya ukaguzi,ni muhimu wawepo. Mimi Nashauri kwa pawe na clearance stika ya Siku kwa ubora wa gari tairi nk. Wakibakie kukagua makosa dereva uendeshaji,kupunguza vituo ukaguzi. Inachosha wilaya moja ukaguzi bima,leseni vituo zaidi ya 4.
 
Niltaka kufungua uzi kma huu. Ila kuzungumzia hasa upande wa busi. Yan ni kero. Busi inakingamuzi, imetoka stend imekaguliwa kila kitu, ila kila kituo chenye trafik inasimamishwa. Najiuliza wanasimamisha kukagua nini tena? Yan usafir wa mikoan sasa hiv unatumia muda mrefu sababu ya hwa trafic. Safar ilyokuwa ya siku 1 siku hiz ni siku mbili.
 
Wanafanya ukaguzi,ni muhimu wawepo. Mimi Nashauri kwa pawe na clearance stika ya Siku kwa ubora wa gari tairi nk. Wakibakie kukagua makosa dereva uendeshashaji,
Kukaguliwa ili upewe stika kila siku bado ni kero. Ndio maana nikasema, ikiwa nakaguliwa wiki ya nenda kwa usalama na kupewa stika, kwa nini unisumbue tena barabarani kutafuta makosa ya gari?

Kumbuka naweza kupewa stika ya Wiki ya Nenda kwa Usaama leo, kesho trafiki ananisimamisha kukagua gari yangu atafute kosa. Huu ni ujinga. Wao wasimaishe gari zinazofanya makosa, sio kila gari.
 
Ni muhimu wakague kuna madereva huwa wanasimama njiani kulewa pombe au kubeba bidhaa haramu, au gari limeharibika njiani lakini kwa sababu ameishakaguliwa anaendelea na safari hivyohivyo
 
Kwa kweli wanachofanya polisi wa barabarani ni unyanyasaji na kupotezeana muda pale wanapo kaa wenyewe wanaita kijiwe yani kila gali inayopita lazima isimamishwe na kuanza kupekua pekuwa gali sijajua na nchi nyingine km wanafanya hivi yani sasa imefika point kutembea na gali ni km unatembea na kaa la moto
 
Jana nilikuwa natoka posta naenda mbagala
Kufika raund about gerezani nimesimamishwa
Polisi ufundi nimesimamishwa tens
Kufika raund about mtongani tena nimesimamishwa
Sasa mambo gani haya wakati kagali kadogo saloon
 
Ni muhimu wakague kuna madereva huwa wanasimama njiani kulewa pombe au kubeba bidhaa haramu, au gari limeharibika njiani lakini kwa sababu ameishakaguliwa anaendelea na safari hivyohivyo
Ndio maana nikauliza, kuna maofisa wa TRA wanachukua rushwa. MBina hatuoni Polisi au TAKUKURU kwenda kila siku ofisni kwao kuwakagua?

Au fikiria hili. Kuna raia nchini wanatembea na silaha mitaani kwenda kufanya ujambazi au kutafuta fursa ya kufanya ujambazi. Je suluhisho ni kusimamisha raia kila siku na kuwakagua kama wana silaha? Ni mwendawazimu ndio anaweza kuja na mbinu kama hizo za kushughulikia tatizo, mtu mwenye akili ndogo mamlaka makubwa.
 
Tunataka pesa zenu ili tuweze kuendesha nchi

Serikali yetu tukufu imenuia kukusanya kodi ya barabara kwa namna ambayo bado wananchi hawajaeleweshwa,,,, tutaanza kutoa elimu namna tulivyojipanga kukusanya kodi hii.

Tunaomba wananchi muwe wazalendo maana serikali inajitahidi kuwa bega kwa bega na nyie
 
Labda ni Tanzania pekee ambako kila siku askari wanasimamisha gari ili watafute kosa kuhusu wewe dereva au gari. Ni kwamba askari anapoamua kusimamisha gari, dereva unakuwa huna kosa aliloona, bali utakaposimama ndio ataanza kutafuta kosa ambalo atakuambia ulilipie faini. Naendesha gari, nafuata kila sheria, gari yangi nzima, halafu unanisimamisha ili unitafutie kosa, kwa nini? Una chuki gani na mimi?

Huu ni uratibu mbaya na haufai, na unakuwa mbaya zaidi pale ambapo unafanywa kama jambo la kawaida la kila siku. Ikiwa huu utaratibu wa kusimamisha gari ili kutafuta kosa ungefanywa wiki ya "Nenda kwa Usalama" wala tusingeona shida. Lakini sasa, kwa nini jeshi la polisi limeamua kwamba haya ndiyo yatakuwa maisha ya kila siku ya wanaoendesha magari?

Je lengo ni nini hasa? NI kwamba serikali imefulia au kufilisika kabisa kiasi kwamba Raisi ametoa agizo kwamba askari watafute hela kwa kuwasumbua wananchi kiasi hiki? Je Raisi au mawaziri hawaoni hii ni kero kwa wananchi kwa kuwa wao hawaguswi na kadhia hii? Ni sawa na Ni sawa na kutembelea Ofisi za TRA na kuwauliza wafanyakazi kama wamepokea rushwa ili uwachukulie hatua!

Kwa nini lakini Raisi Magufuli anaifanya Tanzania kuwa nchi yenye kero na usumbufu usio na msingi? Ana hasira ya kuchaguliwa kuwa Raisi?

Basi sisi kama wananchi tuna ujumbe kwa Raisi Magufuli. Tunaelewa kwamba usalama barabarani ni jambo muhimu, lakini huu usumbufu sio wa lazima ni kero ambayo tusingependa kuwa nayo katika nchi yetu huru. Kama askari wa trafiki wanataka kukaa barabarani basi wasimamishe gari ambazo zinakuwa zimefanya kosa fulani. Sio kunisimamisha ili uanze kutafuta kwa kila namna kosa la kunipigia faini. Huu ni ukandamizaji na unyanyasaji (opression and harassment) ndani ya nchi yetu wenyewe unaopaswa kupingwa kwa nguvu zote na wananchi huru wa Tanzania.
Trafiki wanatafuta fursa ya mapato ya serikali vinginevyo tusijelalamika tukiwekewa kodi ya mswaki ambapo kila kwenye mswaki atatakiwa kuulipia.
 
Ndio maana nikauliza, kuna maofisa wa TRA wanachukua rushwa. MBina hatuoni Polisi au TAKUKURU kwenda kila siku ofisni kwao kuwakagua?

Au fikiria hili. Kuna raia nchini wanatembea na silaha mitaani kwenda kufanya ujambazi au kutafuta fursa ya kufanya ujambazi. Je suluhisho ni kusimamisha raia kila siku na kuwakagua kama wana silaha? Ni mwendawazimu ndio anaweza kuja na mbinu kama hizo za kushughulikia tatizo, mtu mwenye akili ndogo mamlaka makubwa.
Toa ufumbuzi sasa, usiniambie waajiri trafiki zaidi au Polisi zaidi
 
Ni muhimu wakague kuna madereva huwa wanasimama njiani kulewa pombe au kubeba bidhaa haramu, au gari limeharibika njiani lakini kwa sababu ameishakaguliwa anaendelea na safari hivyohivyo
Naungana na mleta uzi. Ni muhimu wawepo lakini wasimamishe hari pale wanapoona, kwa mfano, gari linaendeshwa vista kiasi cha kuweza kuleteleza ajali. Si vizuri kabisa kusimamisha gari halafu ndo uanze kutafuta makosa.
 
Hili la traffic kuacha kusimamisha magari na kutafuta makosa,litamalizwa maratu ambapo madereva na wamiliki wa magari watakapokuwa wazalendo wa kusimama wenyewe wanapomkuta askari traffic na kueleza makosa ya magari yao na kujipeleka wenyewe vituo vya polisi kuripoti makosa yao.
 
Ni muhimu wakague kuna madereva huwa wanasimama njiani kulewa pombe au kubeba bidhaa haramu, au gari limeharibika njiani lakini kwa sababu ameishakaguliwa anaendelea na safari hivyohivyo
Kwa sababu ya hawa wachache tusumbue watu wengi?
Hebu fikiria,asubuhi unawasha gari lako kwenda ofisini KM 8 mfano, unaendesha KM 3 unasimamishwa na Traffic na viPOS vyao, anazunguka gari mara mbili, anaomba driving licence yako, anaomba kadi ya gari then anakurudishia vitu vyote anakuambia uko sawa nenda. Unatoka hapo karibia unafika ofisini unakutana na Traffic wengine na zoezi ni hilo hilo.....Mimi huwa najiuliza nakosa jibu na kama mtu anafikiri uongo iko hivi
Unatoka zako Mkolani Mwanza kuelekea mjini unafika Maeneo ya Stendi kuu (Nyegezi) unapigwa mkono unakaguliwa(Tuseme wanatafuta makosa) wanakuruhusu kuondoka, unafika relini unakutana nao unasimama tena na ukifika mjini maeneo ya SITTA Supermarket unawakuta wamepanga magari pale na unasimama!!!!
Halafu sehemu zote tatu hata haukutwi na kosa ni upuuzi tu na hii safari ni kilomita kumi tu.
Kwa kweli hawa jamaa wamekuwa wasumbufu mno na wasipoona kosa wanakukalisha muda mrefu mno wakitafuta kosa hadi expiry date za matairi watatafuta.
Mi siku moja niliambiwa kosa la kutoandika anuani ya gari ubavuni na nilikuwa na kicorona!!!
Siku nyingine sina First Aid Kit yaani ni shida mno. Mara Fog light moja haiwaki na hizo zote wanakula 30,000 si upuuzi jamani. Hivi hiyo ajari ya kusababishwa na kutoandika anuani ubavuni ni ipi? au unayosababishwa na kutokuwa na First Aid kit ni ajari ipi?
Anywa, siku hizi wanasoma ripoti ya makusanyo kwa hiyo wanajitahidi sana kukusanya.
Hapa kazi tu.
 
Kila nikisimamishwa huwa nawauliza askari,
mnasimamisha kila gari au mnasimamisha gari lenye kosa?

Hawajawahi nipa jibu mahususi zaidi ya kusema unatupangia.
Nawaambia,Chukua namba ya gari na leseni,
niandikie kosa then niite mahakamani.
.
.
Sijawahi itwa mahakamani wala kulipa,polisi wa bongo wababaishaji tu.
 
Umeandika upuuzi mtupu
Traffic watajuaje kama dereva amelewa kama hawatasimamisha gari?
Watajuaje gari ni mbovu wasipokusimamisha?
Watajuaje idadi ya abiria imezidi wasipokusimamisha?
Watajuaje umebeba haramu wasipokusimamisha?
USHAHIDI
1.Tumeshuhudia madereva walevi wakikamatwa barabarani baada ya kusimamishwa.
2.Tumeshuhudia magari yenye hitilafu kubwa kama vile kufeli kwa breki yakikamatwa kila siku baada ya traffic kuyasimamisha.
3.Tumeshuhudia madawa ya kulevya,silaha na wahamiaji haramu wakikamatwa baada ya magari kusimamishwa na traffic.
Yaani kwa akili timamu unataka gari itoke Arusha hadi Dar bila kusimamishwa kisa kuna stika ya nenda kwa usalama? Hii ni akili au matope?
Halafu kumlaumu Magufuli kwa jambo hili ni upumbavu mkubwa na yawezekena unaendeshwa na chuki, Kabla ya Magufuli matrafiki hawakuwepo? hawakusimamisha magari? hawakutoza faini?
Tumia akili kijana sio unaleta mada kwa chuki za kipumbavu.
Sitaki majibu yako maana utajibu upuuzi as usual.
Sir Khan
 
Back
Top Bottom