666 chata
JF-Expert Member
- Mar 14, 2013
- 1,710
- 4,044
Ukiwa unauingia uwanja huu wa kisasa na mkubwa kuliko ata viwanja vingi barani ulaya na Africa, unakutana na bango kubwa mbele yake linaloutambulisha uwanja huo kwa majina ya 'Tanzania National Main Stadium' kwa tafsiri isiyo rasmi sana 'uwanja mkuu wa Taifa', na hili ndio jina lake, jina lilobuniwa na watu ambao uenda ni wasomi kabisa na wana exposure kubwa tu ya kuzunguka huku na huko.
Asee kituko iki kinachekesha sanaa maana ni sawa na kumtaja mnyama kwa wajihi wake, na kusema tu huyu ni mbwa, sasa nani asiejua kua uyo ni mbwa? Wewe sema Jina lake nani?
Duniani kote kila nchi ina uwanja wa taifa lakini vyote vina majina yake na yenye kuleta maana tu, majina yapo mengi sana ambayo yangekua kama utambulisho wa taifa kwa namna yake, sasa uwanja mzuri kama huu wetu wa taifa si ungeitwa tu ata 'Mwalimu Nyerere Stadium' au 'the Serengeti Arena' au ata Tanzanite Stadium na majina mengi tu yenye maana kubwa hapa nchini.
Sasa et uwanja unaitwa Tanzania National Main stadium? Sasa si kituko hiki au? Ni hatujui kiingereza au tunajua national main stadium ni bonge la jina la kimataifa? Tunatia aibu bhana hasa nyie TFF, acheni zenu uwanja upewe jina ilo, kama uko vijijini tu Ng'ombe wanapewa majina mazuri tu na hawaitwi 'Cow' kama nyie mlivyofanya, sasa mnashindwa wapi nyie? Muuite ata Chief Mkwawa Stadium.
Asee kituko iki kinachekesha sanaa maana ni sawa na kumtaja mnyama kwa wajihi wake, na kusema tu huyu ni mbwa, sasa nani asiejua kua uyo ni mbwa? Wewe sema Jina lake nani?
Duniani kote kila nchi ina uwanja wa taifa lakini vyote vina majina yake na yenye kuleta maana tu, majina yapo mengi sana ambayo yangekua kama utambulisho wa taifa kwa namna yake, sasa uwanja mzuri kama huu wetu wa taifa si ungeitwa tu ata 'Mwalimu Nyerere Stadium' au 'the Serengeti Arena' au ata Tanzanite Stadium na majina mengi tu yenye maana kubwa hapa nchini.
Sasa et uwanja unaitwa Tanzania National Main stadium? Sasa si kituko hiki au? Ni hatujui kiingereza au tunajua national main stadium ni bonge la jina la kimataifa? Tunatia aibu bhana hasa nyie TFF, acheni zenu uwanja upewe jina ilo, kama uko vijijini tu Ng'ombe wanapewa majina mazuri tu na hawaitwi 'Cow' kama nyie mlivyofanya, sasa mnashindwa wapi nyie? Muuite ata Chief Mkwawa Stadium.