Ifahamu sumu kuvu (mycotoxins)

Asilimia kubwa ya wabongo wanaweza wasiwe exposed kwenye kiwango kikubwa cha aflatoxin na aina nyingine za sumu kuvu kutokana na kula ugali wa sembe, kukoboa mahindi kunapunguza sumu kuvu kwa kiwango kikubwa sana. Kwa wale wanaopenda dona, ni bora ukaandaa mahindi yako mwenyewe, ukaaondoa yale mahindi mabovu, ukaosha na kuanika kabla ya kwenda kusaga.

Kwa sababu karanga zinaweza kuwa na kiwango kikubwa cha aflatoxin, inafaa kuzichambua na kuondoa zile mbovu na zilizosinyaa. Kwa wale wanaoandaa unga kwa ajili ya watoto wawe makini zaidi kuchambua mahindi na karanga kwa ajili ya kusaga unga kwa ajili ya uji wa mtoto, nafikiri tumeelewana ndugu zanguni....
Karanga zinapendwa sana na kuvu...
 
Chanzo cha hii "sumu kuvu" (aflatoxin/mycotoxin) ni kutokana na kuhifadhi nafaka kama MAHINDI na KARANGA sehemu zenye UNYEVU-UNYEVU (Humid environment).. Kwasababu aina hii ya fungus na fungus wa aina zingine hupendelea sehemu zenye unyevu unyevu...
 
Inashauriwa nafaka hizi zikaushwe vizuri kabla ya kuhifadhiwa, na zihifadhiwe sehemu isiyo na unyevu unyevu au isiyoruhusu unyevu kuingia...
Pia mazao yakikauka yavunwe maramoja mfano mahindi, ili kuepuka mvua zile za mwisho (late season rainfall) kuja kulowanisha mazao shamban kwani ubichi huo utatengeneza mazingira mazuri kwa hawa fungus kutokea.
 
Karanga zinapendwa sana na kuvu...
Yaa, pamoja na mahindi, mfano, kule kenya milipuko ya watu kuugua na baadhi kufa kutokana na kula mahindi yenye kiwango kikubwa cha aflatoxin vimekua vikitokea mara kwa mara tokea mwaka 1981 na hivi karibuni mwaka 2004. Nilishangaa kusikia wanasema mahindi kutoka Tanzania yana aflatoxin jambo ambalo si kweli. Kutokana na kuwa na uhaba mkubwa wa mahindi huko kenya, watu wanaweza kuhifadhi hayo mahindi kwa muda mrefu kwenye mifuko ya sandarusi ambayo inaweza kupelekea kutengeneza uvundo na kuzalisha kiwango kikubwa cha aflatoxin, na kutokana na hali ya uhaba wa nafaka watu hasa wa kipato cha chini hawana namna ya kuacha kutumia mahindi hata kama kwa macho yataonekana hayafai kutumiwa kama chakula....
 
Karanga zinapendwa sana na kuvu...

Yaa, pamoja na mahindi, mfano, kule kenya milipuko ya watu kuugua na baadhi kufa kutokana na kula mahindi yenye kiwango kikubwa cha aflatoxin vimekua vikitokea mara kwa mara tokea mwaka 1981 na hivi karibuni mwaka 2004. Nilishangaa kusikia wanasema mahindi kutoka Tanzania yana aflatoxin jambo ambalo si kweli. Kutokana na kuwa na uhaba mkubwa wa mahindi huko kenya, watu wanaweza kuhifadhi hayo mahindi kwa muda mrefu kwenye mifuko ya sandarusi ambayo inaweza kupelekea kutengeneza uvundo na kuzalisha kiwango kikubwa cha aflatoxin, na kutokana na hali ya uhaba wa nafaka watu hasa wa kipato cha chini hawana namna ya kuacha kutumia mahindi hata kama kwa macho yataonekana hayafai kutumiwa kama chakula....
Inawezekana lakini wameshayashuku mahindi yetu hivyo ni vyema tuwe na hii elimu ya uhifadhi bora ili kugeuka hasara.
 

Attachments

  • Screenshot_20210307-220618_Chrome.jpg
    Screenshot_20210307-220618_Chrome.jpg
    62.9 KB · Views: 1
Wale wapenzi wa udaga au unga wa mihogo embu angalieni hii picha hapa chini huenda tukaona tunakoelekea au tukaamua kubadili uelekeo.

20210329_121342.jpg


20210329_121407.jpg


20210329_124647.jpg


20210329_124719.jpg


20210329_124834.jpg
 
Back
Top Bottom