Idara ya Usalama wa Taifa yakanusha tuhuma

Idara ya Usalama wa Taifa yakanusha tuhuma

Status
Not open for further replies.
Ukweli ni kwamba hawa TISS/UWT wamehusika na kuteka,kutesa na kujaribu kumwua Dr.Ulimboka. Hii ni piga ua wao ni watuhumiwa nambari wani!

Kitendo cha Polisi wenzao kutaka kuwasafisha kwa kisingizio cha Mkenya ni kuzidi kujidhalilisha! Maana bado moto utawawakia wao UWT na POLISI. Maana bado Watanzania tutauliza huyu Mkenya aliingiaingiaje nchini bila ya KUGUNDULIKA NA VYOMBO VYA USALAMA wakiwemo TISS na POLISI ambayo ndiyo kazi yao????

Maana kama hawahusika na kosa la utekaji wa Dr.Uli bado basi wana kosa la KUZEMBEA KWA KURUHUSU JASUSI,JAMBAZI AU ADUI TOKA NCHI JIRANI YA KENYA KUINGIA NCHINI TANZANIA NA KUFANYA UHALIFU WA KUMSHAMBULIA RAIA WA TANZANIA AMBAYE USALAMA WAKE UKO MIKONONI MWA WANA USALAMA uchwara!!!!

Kwa hiyo these guys(Police Force&TISS) hawana pa kutokea, bado moto utawawakia tu! Strategy yao ime-fail kwasababu waliipanga kijinga na katika hili wameonyesha kuwa hawafai kuwa wana usalama wa Taifa hili.Kwamba hawawezi kulinda usalama wa Raia,hawawezi kulinda mipaka ya nchi yetu na hawawezi kulinda Usalama wa Ikulu yetu. Adui yeyote toka popote anaweza kuingia Tanzania wakti wowote akashambulia na kutoweka bila ya kugundulika! Kwa hiyo waache kabisa kutudanganya kwa kusingizia mkenya wa watu ambaye tayari tumesha ambiwa ni KICHAA!

Sasa kichaa na kupanga mipango ya kumteka Dr. Ulimboka wapi na wapi????Nauliza tu!
 
Wauwaji wakubwa nyie, mlimuua Zongo na watuumiwa wakaachiwa kwa ujanja ujanja, kama kweli hamhusiki kwanini msimkamate aliyempigia simu ulimboka daklika za mwisho? wakati Dr Ulimboka kamtaja kuwa mara ya mwisho aliwahi kufanya nae mazungumzo Ikulu? Kwa kifupi sisi wananchi hatuna usalama wa taifa tena, hatuna Imani na nyie, tutajilinda wenyewe. Nyie ni usalama wa CCM na siyo taifa, kazi yenu nikulinda vitambi vya mafisadi
 
Sasa si waende mahakamani kama ni uongo ili wananchi tuamini?
Watoa tuhuma wapo na wanaendelea kutoa.
 
tuseme yote lakini ukweli unabaki pale pale kuwa magazeti yanaandika ili yauze,ndio kazi yao.

mwanahalisi limepika taarifa na halina ukweli wowote,linaacha maswali mengi ya kujiuliza katika taarifa yake.wanajifurahisha
 
kama hiyo idara inakanusha kwamba haihusiki na utekaji wa Dr. Ulimboka,,,kwa nini isilishitaki gazeti lililotoa taarifa hizo na kuzianika kwa jamii?watoaji wa taarifa hizo wanajiamini na wanajua wanachokifanya na wanaushahidi wa kutosha.
 
Hawana lolote hao, kwani toka lini wamekubali huo ushenzi wanaofanya kila siku? twiga wameibiwa yapo kimya tu hayatoi tamko, epa, richmond na madudu mengine hawatoi matamko kuwa tumekamata leo ndio unataka waseme tulimtesa ulimboka. Kwani hao polisi wanavyoua wanasemaje si ushenzi huo huo. Watanzania hakuna mjinga tena, waache wafanye tu ila ipo siku ambayo watajuta kwa nini walizaliwa. Mwisho wa ubaya ni aibu. UWT wa sasa ni vibaraka tu wa dhaifu na washkaji wake na ndio maana huko mtaani wanasema yale yote dhaifu anayowatuma wakafanye.
 
hawawezi kukubali hata siku moja.
Kinachoendelea humu jamvini ni wachangiaji wengi kutaka TISS wakanushe kwamba Rama siyo mtumishi wake,lakini kwa kawaida Rama kama kweli yupo ni sehemu ya taasisi? Na kama taasisi haihusiki, Rama atahusika vipi? Inavyoelekea watu wamejijengea tabia ya kuamini kwamba TISS inakanusha tu, lakini inahusika. Sasa kama watu hawawezi kuukubali ukweli mwingine ni bora kusubiri.
 
kama hiyo idara inakanusha kwamba haihusiki na utekaji wa Dr. Ulimboka,,,kwa nini isilishitaki gazeti lililotoa taarifa hizo na kuzianika kwa jamii?watoaji wa taarifa hizo wanajiamini na wanajua wanachokifanya na wanaushahidi wa kutosha.
Ushahidi wa kwenda kampuni ya simu na kuchukua details za mteja wao na kuzianika ndiyo ushahidi gani huo? Mimi naona Kampuni ya simu iliyotoa taarifa za mteja wao nao lao moja na Kubenea.
 
Hawana lolote hao, kwani toka lini wamekubali huo ushenzi wanaofanya kila siku? twiga wameibiwa yapo kimya tu hayatoi tamko, epa, richmond na madudu mengine hawatoi matamko kuwa tumekamata leo ndio unataka waseme tulimtesa ulimboka. Kwani hao polisi wanavyoua wanasemaje si ushenzi huo huo. Watanzania hakuna mjinga tena, waache wafanye tu ila ipo siku ambayo watajuta kwa nini walizaliwa. Mwisho wa ubaya ni aibu. UWT wa sasa ni vibaraka tu wa dhaifu na washkaji wake na ndio maana huko mtaani wanasema yale yote dhaifu anayowatuma wakafanye.

Wewe mbona unaongea kama umelala vile? Ninachokumbuka mimi ni kwamba TISS hawajawahi kutuhumiwa kutorosha Twiga na Hapa wametuhumiwa kumtesa Ulimboka, huwezi kuona tofauti hizo mbili.
 
Hawa usalama nao wamepitwa na wakati sana. Zamani serekali ikisema jambo watu wote walikuwa wanalikubali. Siku hizi hata waseme kwa kusisitiza vipi, wananchi wanaona kama ngonjera tu. Wajue kuwa wananchi wameshaamka kutoka usingizini. Upuuzi mtupu wametuandikia hapa ili waonekane wako ok, no way. Such serious allegations do not need such reactions. Kama sio ninyi na kwa vile nyie ndio usalama wa taifa, intelijensia yenyewe, bring the to us who did that
 
tusipo wakubali kwa kauli yao tutawakubali kwa lipi? cha msingi tuwaombe uchunguzi wa kina na majibu yake watuletee wao na director kova, ili wananchi wapate ukweli wa jambo lenyewe.
 
kama hiyo idara inakanusha kwamba haihusiki na utekaji wa Dr. Ulimboka,,,kwa nini isilishitaki gazeti lililotoa taarifa hizo na kuzianika kwa jamii?watoaji wa taarifa hizo wanajiamini na wanajua wanachokifanya na wanaushahidi wa kutosha.
Sidhani kama kila unapotuhumiwa lazima uende mahakamani. Mbona watu mbalimbali, vyama vya siasa , makampuni yameshatuhumiwa lakini si wote wanaokwenda mahakamani? Hapa naona kama tunakionea chombomhicho cha dola, Mbona mara kibao Polisi wametuhumiwa kwa mauaji na hawajawahi kwenda mahakamani? Mtu wenye matunda ndiyo unaopopolewa kwa mawe, Tusiwakatishe tamaa hawa jamaa kwa maneno ya kugushi na taarifa za waathirika. Huyu Kubenea bado ana kinyongo na Tindikali aliyomwagiwa sasa anafikiri ndiyo sehemu ya kulipiza kisasi na sijui kwa faida ya nani?
 
Ni vyema usalama wa taifa wakaja na majibu hata kama jeshi la polisi linachunguza watuambie aliyetajwa na namba yake kuanikwa hadharani,si mfanyakazi wao ,ni nani na anafanya kazi wapi ili akamatwe alisaidie jeshi la polisi kwani katika hali ya kawaida mtu yeyote akifa,au kuumizwa ktk mazingira kama hayo ya Ulimboka mtuhumiwa wa kwanza ni aliyekuwa nae mara ya mwisho na aliyekuwa nae ni aliyekuwa anawasiliana nae.Waje na majibu wasilete porojo hawa.
 
Wanaofanya kazi UWT ni Watanzania wenzetu tunaoishi nao huku mitaani na vijijini. Tunaishi kwa ujanjaujanja,michongo,fitina,majungu,nk. Kwa hiyo sishangai kusikia tuhuma hizo! Tumekuwa watu wa hovyo!
 
ukitaka kujua shilingi tazama pande zote yani kichwa na mwenge. Sasa wakikubali kuhusika hawataitwa usalama wa taifa bali usalama wa viongozi walioko madarakani.
 
Sidhani kama kila unapotuhumiwa lazima uende mahakamani. Mbona watu mbalimbali, vyama vya siasa , makampuni yameshatuhumiwa lakini si wote wanaokwenda mahakamani? Hapa naona kama tunakionea chombomhicho cha dola, Mbona mara kibao Polisi wametuhumiwa kwa mauaji na hawajawahi kwenda mahakamani? Mtu wenye matunda ndiyo unaopopolewa kwa mawe, Tusiwakatishe tamaa hawa jamaa kwa maneno ya kugushi na taarifa za waathirika. Huyu Kubenea bado ana kinyongo na Tindikali aliyomwagiwa sasa anafikiri ndiyo sehemu ya kulipiza kisasi na sijui kwa faida ya nani?
Mimi sioni sababu ya wao kukimbilia mahakamani watuambie namba ya simu imetajwa wamtafute ajulikane ni nani anafanya kazi gani kwa nini awe na Dr. Ulimboka mara ya mwisho na apotee katika mazingira ya kutatanisha na aokotwe ameumizwa.Alichukue hatua gani baada ya Dr Ulimboka kutekwa na kwa nini simu yake iliwekewa fedha nyingi kabla, nani aliweka fedha hizo kwenye simu yake,kwa sababu gani na so kawaida.Kwa nini simu yake haikuwa hewani baada ya tukio, na wale aliokuwa anawasiliana nao pia ni akina nani.Hayo ndo maelezo yanatakiwa na ndio kazi ya polisi na usalama wa taifa sio porojo za Kubenea na kumwagiwa tindikali brother.
 
tuseme yote lakini ukweli unabaki pale pale kuwa magazeti yanaandika ili yauze,ndio kazi yao.

mwanahalisi limepika taarifa na halina ukweli wowote,linaacha maswali mengi ya kujiuliza katika taarifa yake.wanajifurahisha
Turudi kwenye ukweli jeshi la polisi na usalama wa taifa ndio wanaotakiwa watujibie maswali hayo yasiyo na majibu yaliyotolewa na mwanahalisi huyo aliyekuwa anampigia simu ni nani kwani taarifa hizo za mwanahalisi ndio mwanzo mzuri wa kumpata mtekaji.Kwa nini taarifa hizo zisifanyiwe kazi? ni ushahidi gani tena zaidi unatakiwa ndugu yangu? Mbona iko wazi mno ?
 
Failed state............hata USSR wakati ukomunisiti unataka kuanguaka KGB behaved the same way ...............hata producers wa bongo movies wangelitengeneza vizuri kidogo...............ila kwa sababu maji yako shingoni hata akili za kitoto zimewaishia............2015 tuiondoe CCM madarakani na tubadilishe the whole broken intelligency and security system
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom