Idara ya serikali inayoongoza kwa ufisadi Tanzania

thread critic

Member
Jul 17, 2012
71
14
Sidhani kama hata ile idara ya procurement pale BOT wanaweza kuwashinda hawa Tanesco kwa ufisadi uliokithiri. TRA peke yake ndio itakuwa inawazidi Tanesco kwa rushwa Tanzania

Lakini mkitaka kujua ufisadi unavyofanya kazi tazameni:

1. Valuation team za hii tender board ina comprise akina nani

2. Muda gani wanakaa kufanya valuation

3. Appeals zilizopelekwa na watu waliochakachuliwa kwenda PPRA na PCCB na kwenye management ya Tanesco

4. Tazameni barua wanazopewa wanaokosa tenda pale TANESCO zinaandikwaje? na kwa nini haielezwi sababu ya kampuni kokosa kazi

5. Tender board wanapewa documents masaa mangapi na hii team ya valuation kabla hawajaamua nani apewe tender

6. Je Tenderboard ya TANESCO iko na akina nani.

7. Legal team ya TANESCO kwa nini wanapitisha haya madudu?

8. Mara ngapi TANESCO wamekiuka miiko na masharti ya PPA2004?

Baada ya hapo mtajua kwanini nimesema kuwa idara ya procurement na inaongoza kwa rushwa na ufisadi Tanzania.
 
hapa unaongelea idara zipi? za TANESCO, PCCB, BOT au TRA? sijakupata
 
Back
Top Bottom