Idadi ya mikoa irejeshwe kama zamani

Idadi ya mikoa irejeshwe kama zamani

Kama una watoto sita ni dhahiri huwezi kuishi chumba kimoja,lazima utafute nyumba kubwa.tanzania ya mwaka 1980 sio ya 2015,kuongeza mikoa kunasaidia kurahisisha huduma za kiutawala kwa wananchi.
kwa hiyo ukubwa wa tanzania umeongezeka?
 
Hili ni jipu hasa, kama kuna mkoa usio kuwa na jografia rafiki ni Mkoa wa Manyara jamani kha! Mtu anatoka mererani anahitaji huduma ya mkoa , anapita Arusha analala anaamka kesho kwenda Babati, kama una kesi inabidi uwe na hela ya kulala gesti, huduma angeweza pata Arumeru lakini lolh. Mkwere! Hata sahaulika.
Hapo Kikwete unamuonea, huu mkoa wa Manyara uliongezwa kipindi cha utawala wa Mzee Ben na si Kikwete.
 
gharama kubwa zimeongezeka kutokana na kuongezwa mikoa badala yake hizo pesa zingetumika kuboresha miundo mbinu haya ya kuongeza mikoa yaliamriwa kisiasa zaidi
 
Nasikia kuna mchakato unaendelea kuupiga panga Mkoa wa Morogoro. Yaani mpaka unakua mto Ruaha, Wilaya za Kilombero na Ulanga unakua Mkoa mpya.
 
Miaka ya themanini ilikuwa ukimuuliza mtu Tanzania bara ina mikoa mingapi atakwambia 20 na Zanzibar utajibiwa ni 5. Lakini miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mikoa kiasi kwamba hata leo ukiniuliza tuna mikoa mingapi sina jibu.
Kweli kabisa kaka.
 
Miaka ya themanini ilikuwa ukimuuliza mtu Tanzania bara ina mikoa mingapi atakwambia 20 na Zanzibar utajibiwa ni 5. Lakini miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mikoa kiasi kwamba hata leo ukiniuliza tuna mikoa mingapi sina jibu.
.. Uanzishaji wa mikoa kidogo kuna nafuu, shida ipo kwenye wilaya. Dhana ya kufikisha huduma karibu inatatiza. Nenda Tabora, ili mtu wa Tutuo afike ISIKIZYA makao makuu ya UYUI inambidi apite Tabora mjini.
 
Last edited:
Miaka ya themanini ilikuwa ukimuuliza mtu Tanzania bara ina mikoa mingapi atakwambia 20 na Zanzibar utajibiwa ni 5. Lakini miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mikoa kiasi kwamba hata leo ukiniuliza tuna mikoa mingapi sina jibu.
Tusaidiane kuitaja hapa mkuu;
1. Dar
2. Pwani
3. Morogoro
4. Tanga
5. Kilimanjaro
6. Arusha
7. Manyara
8. Singida
9. Tabora
10. Shinyanga
11. Simiyu
12. Mara
13. Mwanza
14. Geita
15. Kagera
16. Kigoma
17. Rukwa
18. Katavi
19. Mbeya
20. Iringa
21. Njombe
22. Ruvuma
23. Mtwara
24. Lindi
25. Dodoma
26. Songwe (is coming soon)

Nafikri nimejitahidi wadau kama kuna mkoa umesahaulika naomba mnikumbushe. Kwa Zanzibar nafikri Shein hakuongeza mikoa, bado ni ile ile 5.
 
Miaka ya themanini ilikuwa ukimuuliza mtu Tanzania bara ina mikoa mingapi atakwambia 20 na Zanzibar utajibiwa ni 5. Lakini miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mikoa kiasi kwamba hata leo ukiniuliza tuna mikoa mingapi sina jibu.

Nadhani issue si mikoa tu, inatakiwa iende zaidi ya hapo- ukubwa wa serikali. Wakati tukifikiri kupunguza wizara, mikoa, wilaya, tarafa na kata na agencies kama bodi ya korosho, maziwa, pareto, tukaongezewa idadi ya makatibu wakuu. Nasikia wizara zingine sasa zinao wanne!!! Mbona watu wawili waliongoza vizuri hapa juzi tu. Shida labda wangepata katika kujibu maswali bungeni na sura zao zingetuchosha (monotony). Wote hawa wa nini? Jamani tuweni serious vinginevyo makusanyo ya kodi yataishia mifukoni mwa hawa vingunge na gharama kubwa za uendeshaji, kwani Kuongeza idadi ya watendaji siyo kuwa ni ufanisi bali gharama. Wakati mwingine huwa nafikiri , hivi watu wanaoongoza mataifa makubwa kama China, Japan na India wanahitaji mikoa, wizara na wilaya ngapi. Au kuendesha kampuni kama Cocacola kunahitaji milolongo hii ya urasimu?! Kumbe ni suala la kuweka miundombinu na proper system of governance. Mwenye sikio na asikie.
 
Nadhani issue si mikoa tu, inatakiwa iende zaidi ya hapo- ukubwa wa serikali. Wakati tukifikiri kupunguza wizara, mikoa, wilaya, tarafa na kata na agencies kama bodi ya korosho, maziwa, pareto, tukaongezewa idadi ya makatibu wakuu. Nasikia wizara zingine sasa zinao wanne!!! Mbona watu wawili waliongoza vizuri hapa juzi tu. Shida labda wangepata katika kujibu maswali bungeni na sura zao zingetuchosha (monotony). Wote hawa wa nini? Jamani tuweni serious vinginevyo makusanyo ya kodi yataishia mifukoni mwa hawa vingunge na gharama kubwa za uendeshaji, kwani Kuongeza idadi ya watendaji siyo kuwa ni ufanisi bali gharama. Wakati mwingine huwa nafikiri , hivi watu wanaoongoza mataifa makubwa kama China, Japan na India wanahitaji mikoa, wizara na wilaya ngapi. Au kuendesha kampuni kama Cocacola kunahitaji milolongo hii ya urasimu?! Kumbe ni suala la kuweka miundombinu na proper system of governance. Mwenye sikio na asikie.
 
Back
Top Bottom