Idadi ya mikoa irejeshwe kama zamani

Idadi ya mikoa irejeshwe kama zamani

TANZANNIA

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2015
Posts
1,047
Reaction score
385
Miaka ya themanini ilikuwa ukimuuliza mtu Tanzania bara ina mikoa mingapi atakwambia 20 na Zanzibar utajibiwa ni 5. Lakini miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mikoa kiasi kwamba hata leo ukiniuliza tuna mikoa mingapi sina jibu.
 
Hili ni jipu jengine ambalo niko na mashaka makubwa kama JPM ataligusa...., vinginevyo so far so good
 
Kwakweli hilo La mikoa hata mimi siku hizi sina jibu kamili.
 
Upo sahihi miaka mingi viongozi Nguri tumewasikia wakizungumzia kuungana ili kuleta nguvu ya uchumi na mambo mengine na si kutenganisha kama hapa kwetu tunavyofanya..
 
100% , badala ya kuongeza ufanisi wa kazi wanaongeza watendaji ambao wengi ni wabadhilifu.
Rudisha mikoa 25, iliyozidi idadi ya watu boresha miundo mbinu weka hadhi ya manispaa, jiji.
 
100% , badala ya kuongeza ufanisi wa kazi wanaongeza watendaji ambao wengi ni wabadhilifu.
Rudisha mikoa 25, iliyozidi idadi ya watu boresha miundo mbinu weka hadhi ya manispaa, jiji.

naunga mkono hojaa.nahc kama gharama za uendeshaji zinaongezeka badala ya kupungua.
 
Naunga mkono hoja, idadi kubwa ya mikoa haina tija yyt kwa taifa zaidi ya watu kujitafutia ulaji tu!
 
Miaka ya themanini ilikuwa ukimuuliza mtu Tanzania bara ina mikoa mingapi atakwambia 20 na Zanzibar utajibiwa ni 5. Lakini miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mikoa kiasi kwamba hata leo ukiniuliza tuna mikoa mingapi sina jibu.

zamani mikoa ilikuwa minane unaongelea zamani ipi?
 
Nikichangia hoja hii nasema irudi kama zamani au kama zamani sana. Zamani sana ni katika mfumo wa mwanzo kabisa wa Tanganyika yaani Majimbo. Hii haimaanishi ni kuunga mkono UKAWA au chama chochote. Ni jambo ambalo lilikuwepo huko nyuma. Hata hivyo ikishindikana, mikoa ibaki ile ile 20 huku Bara na 5 Znz. Mipaka inaweza kufanyiwe re-demarcation/relocation ili kubalance ukubwa wa mikoa. Kwa mfano, mkoa wa Dar es Salaam, Kilimanjaro na Mtwara ni midogo sana, lakini ina watu wengi kwa maana Population Density(People per km) ni kubwa! Dar inaweza kumegewa maeneo ya Mkuranga, Kisarawe na Bagamoyo, wakati Mtwara inaweza kumegewa Tunduru na eneo la Lindi Vijijini. Kilimanjaro inaweza kumegewa baadhi ya maeneo ya mkoa wa Tanga na Manyara!
 
Miaka ya themanini ilikuwa ukimuuliza mtu Tanzania bara ina mikoa mingapi atakwambia 20 na Zanzibar utajibiwa ni 5. Lakini miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mikoa kiasi kwamba hata leo ukiniuliza tuna mikoa mingapi sina jibu.



Si unakumbuka kuna mtoto wa mnene alikuwa anawatafutia mashost nafasi za uongozi?
 
Hili ni jipu hasa, kama kuna mkoa usio kuwa na jografia rafiki ni Mkoa wa Manyara jamani kha! Mtu anatoka mererani anahitaji huduma ya mkoa , anapita Arusha analala anaamka kesho kwenda Babati, kama una kesi inabidi uwe na hela ya kulala gesti, huduma angeweza pata Arumeru lakini lolh. Mkwere! Hata sahaulika.
 
Naunga mkono hoja. Mikoa ni mingi sana, idadi ya wilaya ni kubwa mno, na baraza la mawaziri ni kubwa sana. Gharama za uendeshaji ni balaa hasa katika ununuzi na kuhudumia mashangingi, makazi na mishahara. Uongezaji na uendelezwaji wa vitu hivi ni kwa ajili ya kulipa fadhira za maswahiba na hazina tija yeyote. Kuboresha ufanisi siyo kuziongeza, cha mhimu ni kuwa na miundombinu, hususani barabara, mawasiliano na hali bora za watumishi. Kodi ichochee maendeleo ya wananchi na siyo kugharimia LISERIKALI
 
Mkoa mwingine ni Katavi,yaani huu bado kabisa kuwa Mkoa sema siasa za Pinda ndio zimefanya ukawa Mkoa.
 
Na kila wilaya iwe ndiyo jimbo la uchaguzi kama zamani. Idadi kubwa ya wabunge haiongezi ufanisi bungeni. Inaongeza gharama ya kuendesha bunge.

Viti maalum vifutwe kabisa. Ukiondoa wabunge wa majimbo (kila wilaya mmoja), wabunge wa ziada wawe ni AG kwa nafasi yake na wale wa kuteuliwa na Rais wasizidi watano.
 
Haya ndiyo mambo ya kutajwa katika katiba, lazima ieleweke nchi imegawanyika kwa utaratibu upi, wizara ngapi, siyo Kila kiongozi ajaye anakipa kijijini chake hadhi ya Mkoa au idadi ya wizara kutegemea idadi ya mashwahiba.
 
Back
Top Bottom