Hysteria ya uongo!

Hysteria ya uongo!

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,094
Reaction score
136,678
Howdy!?

Naona kuna kakundi ka watu wachache humu JF na kwenye mitandao mingine ya kijamii wanaotengeneza hysteria ya uongo kwa kukuza mambo.

Lengo lao ni moja tu, nadhani. Ni kumchafua rais aliyepo madarakani sasa.

Awali mtu ungeweza kusema labda pia hawa watu wanaichukia CCM. Lakini mimi nimehitimisha kuwa wanamchukia zaidi Rais Magufuli kuliko wanavyoichukia CCM.

Na ndo maana wanakuwa wanakuza kuza tu mambo.

Wakiona kijimakala kilichochapishwa kwenye jarida sijui la wapi wapi huko wanakimbilia kuchekelea, kusherehekea, na kupagawa utadhani ni ujio wa pili wa Yesu au kiama.

Oh sijui mpaka wazungu wameandika...sijui wazungu nini nini....who cares what wazungus say?

Mara sijui watu siku hizi wanapigwa risasi! Kwani zamani watu walikuwa hawapigwi risasi?

Mnashangaza sana nyie watu. Mko too hysterical kiasi hata kumbukumbu zenu zimeathirika.

Kikwete aliponunua yale magari ya kupulizia upupu mlilia lia humu na mkamlaani. Leo hii kaja Ngosha Mashine mnajifanya kumkumbuka Kikwete. Ina maana mmesahau kuwa alileta magari 700 na ushee ya kuwapulizia upupu na akawaambia ole wenu mkileta vurugu kwenye uchaguzi?

Mna matatizo sana nyie watu!

Si ajabu mshasahau kuwa Dkt. Ulimboka naye alitekwa na watu wasiojulikana akajikuta yuko Mabwepande huko akiwa hajielewi wakati Kikwete akiwa rais.

Hata yule Kibanda naye si alipigwa na hao hao wasiojulikana kipindi cha Kikwete...

Lakini mnavyopiga mayowe sasa hivi utadhani haya mambo yameanza baada ya Ngosha Mashine kushika hatamu za madaraka.

Acheni kukuza mambo nyie makamanda.

Mliikuza ile njaa weee hadi mkaishia kuumbuka tu mwishowe. Tena hayo matumbo yenu makubwa ndo yaliwaumbua zaidi maana kila nilipokuwa nawauliza kama mmeshinda njaa mlikuwa mnakosa majibu.

Mtaishia kuwa wafa maji tu na huko kutapatapa kwenu.
 
Silichukii jiwe, kuna mambo yapo sawa na mengine yameenda mrama..

Tatizo kuna watu wamebobea kwenye tasnia ya ukosoaji na kulaumu kila kitu. Mbaya zaidi unakuta huyo anaetaka mambo yaende sawa, familia inamshinda kuiongoza.

Mwisho, hata kama kuna uvundo ulifanyika tawala zilizopita, ugiligili wowote utakaofanywa sasa na baadae hautanyamaziwa.
 
Nyani Ngabu pepo mchafu wa kumkejeli Rais aliyekuingia 2015 ni dhahiri ameshindwa katika jina la Yesu na sasa umekuwa " mtoto" mzuri. Ubarikiwe na hao wazungu wanaokutumikisha kwa kuwalea huko ughaibuni washindwe na walegee!!......karibu Tanzania tujenge taifa letu utumwa ni dhambi NN!
 
Back
Top Bottom