Hydroponic fodder, Mkombozi pekee wa wafugaji wa ng'ombe, kuku, nguruwe, mbuzi na kadhalika

K

Trei zipo, Tshs. 7,000/= kama unahitaji tuwasiliane. Mi niko Mwanza city. Nutrients sio lazima ila ni muhimu kwa sababu ndo hizo zinazotumika pia kuboresha afya ya mifugo. Ndiyo maana unashauriwa kutumia zenye NPK, hizi ni muhimu sana kwenye ukuaji wa mmea na mifugo pia.
Ninachokisubiria ni namna zinavyoweza kuwakuza haraka vifaranga tofauti na mashes za kawaida. Natarajia kuwa na vifaranga tarehe 12 Feb. 2017; hivyo kila hatua nitakayokuwa nafikia nitawajulisheni waungwana.
NPK si ni mbolea au ni kitu kingine kabisa? Ngoja nifuatilie hii elimu ya Hydroponics humu then nitakuuliza maswali mengi maana haipo sana kichwani. Lakini kwa kuanza tu, mnasema gharama yake ni ndogo, mfano kg moja ya hiyo mbegu ya shayiri ni sh.ngapi na ng'ombe mmoja kwa siku anaweza kutumia kiasi gani ya hiyo kg? Na mfugo unaweza kumpa hiyo hydroponics tu bila ya chakula kingine?
 
NPK si ni mbolea au ni kitu kingine kabisa? Ngoja nifuatilie hii elimu ya Hydroponics humu then nitakuuliza maswali mengi maana haipo sana kichwani. Lakini kwa kuanza tu, mnasema gharama yake ni ndogo, mfano kg moja ya hiyo mbegu ya shayiri ni sh.ngapi na ng'ombe mmoja kwa siku anaweza kutumia kiasi gani ya hiyo kg? Na mfugo unaweza kumpa hiyo hydroponics tu bila ya chakula kingine?
1. KIlo moja ya mtama / ngano ni Tshs 2,000/= kwa hapa Mwanza, na hiyo ni bei ya rejareja. Ina maana ukinunua kwa jumla utakuwa chini.
2. Kuhusu kiasi cha kulisha ng'ombe mmoja binafsi sijafatilia - mi nafuga kuku, kumu mia wanatumia kilo nne za H.Fooder
 
1. KIlo moja ya mtama / ngano ni Tshs 2,000/= kwa hapa Mwanza, na hiyo ni bei ya rejareja. Ina maana ukinunua kwa jumla utakuwa chini.
2. Kuhusu kiasi cha kulisha ng'ombe mmoja binafsi sijafatilia - mi nafuga kuku, kumu mia wanatumia kilo nne za H.Fooder
Nashukuru kwa majibu yako. Ila hapo kwenye bei sio kwamba hiyo H. Fodder ndo gharama zaidi nikiwa na maana kama kuku wako 100 wanatumia sh.8000 /day kiasi kwamba hiyo fedha kwa chakula cha kununua isingefika huko. Mimi kuku wangu ni wa kienyeji na nawalisha pumba tu za kawaida hivyo nataka nijifunze hii kitu kama sio gharama sana.
 
Nashukuru kwa majibu yako. Ila hapo kwenye bei sio kwamba hiyo H. Fodder ndo gharama zaidi nikiwa na maana kama kuku wako 100 wanatumia sh.8000 /day kiasi kwamba hiyo fedha kwa chakula cha kununua isingefika huko. Mimi kuku wangu ni wa kienyeji na nawalisha pumba tu za kawaida hivyo nataka nijifunze hii kitu kama sio gharama sana.
Umechanganya ndugu,
kilo nne za H. Fooder sio elfu nane - hiyo ni bei ya mbefu. H. Fooder ni majani pamoja na mizizi na kilo moja ya mbegu ndo inaweza kukupatia kilo 10 za H fooder. Naomba nieleweke kwenye hilo.
 
Ndugu zangu msinione mshamba kwa hili,yan nmesoma post zenu ata nijue hyo H Fooder ni nn kiukwel cjaelewa naona kila mmoja anasifia pia maelezo yanaonyesha faida nyingi kwenye hyo kitu,daah nisaidieni nielewe hyo kitu ni nini na inatumika kwa mifugo aina ipi?
 
Ndugu zangu msinione mshamba kwa hili,yan nmesoma post zenu ata nijue hyo H Fooder ni nn kiukwel cjaelewa naona kila mmoja anasifia pia maelezo yanaonyesha faida nyingi kwenye hyo kitu,daah nisaidieni nielewe hyo kitu ni nini na inatumika kwa mifugo aina ipi?
Hydroponics Fooder ni nini?
Ni utaratibu wa kuotesha mazao aina ya mtama, ngano, shayiri, ulezi n.k bila kutumia udongo. Ina maana utakachokiotesha kinatumika chote kama chakula kuanzia mizizi hadi majani. Unaotesha kwenye trai na unatumia virutubisho vyenye wingi wa NPK, kwa sasa mimi natumia DI Grow green pamoja na EM na mbegu zinaota vizuri.
Kama wewe ni mfugaji na una shida na uzalishaji wa chakula tuwasiliane ili nikuelekeze.
Trei zipo
Mbegu ziko sokoni
Maji yapo hapo ulipo
Nutrients unaagiza popote
SOP's ndo muhimu na utaelekezwa ...
Uliza jingine
 
Hydroponics Fooder ni nini?
Ni utaratibu wa kuotesha mazao aina ya mtama, ngano, shayiri, ulezi n.k bila kutumia udongo. Ina maana utakachokiotesha kinatumika chote kama chakula kuanzia mizizi hadi majani. Unaotesha kwenye trai na unatumia virutubisho vyenye wingi wa NPK, kwa sasa mimi natumia DI Grow green pamoja na EM na mbegu zinaota vizuri.
Kama wewe ni mfugaji na una shida na uzalishaji wa chakula tuwasiliane ili nikuelekeze.
Trei zipo
Mbegu ziko sokoni
Maji yapo hapo ulipo
Nutrients unaagiza popote
SOP's ndo muhimu na utaelekezwa ...
Uliza jingine
Nashukuru sana mkuu kwa maelezo yako pia nmeipenda hyo njia inayotumika,ila mkuu mimi ni mfugaji wa kuku na cfugi wanyama pia kwenye huo ufugaji wenyewe hunipa changamoto ad nashindwa kuelewa faida yake inavyopatikana,vp hyo h food c kwa ajili ya wanyama pekee au ata kwa hawa ndege?
 
Nashukuru sana mkuu kwa maelezo yako pia nmeipenda hyo njia inayotumika,ila mkuu mimi ni mfugaji wa kuku na cfugi wanyama pia kwenye huo ufugaji wenyewe hunipa changamoto ad nashindwa kuelewa faida yake inavyopatikana,vp hyo h food c kwa ajili ya wanyama pekee au ata kwa hawa ndege?
Kuku wakipatiwa hiyo chakula wanakula sana tena sana. Inasaidia kwa sababu huangaiki tena kuwatafutia majani.
upload_2017-2-13_15-37-51.jpeg
 
Wala sio kitu cha kusema ni complicated system .. mi huwa nafanya kwa vifaa nilivyonavyo ili mradi nifate maelekezo ya kitaalam. Kwanza mpaka sasa naoteshea ndani kwa sababu sijajenga sehemu maalum kwa ajili ya shughuli hiyo.
Niko Mwanza city - Karibu sana!
Haya ndo mambo vijana tunatakiwa kushirikishana, sio ya kijingajinga na ndoto za alinacha. Mkuu hongera sana, na utabarikiwa sana. Binafsi ntaangalia uwezekano wa kukuona, niko Simiyu. Na ukame, uhaba wa maeneo ya malisho ni shida sana kwa wafugaji wetu.

Naamini nikielimika ktk hili ntawaokoa wengi sana. Kwanza nitajaribu kuwashirikisha wataalamu wa huku, tukishindwa nitakufuata Mkuu.

Nadhani huu utamaduni ukiendelezwa wa kushirikishana tutafika mbali sana, Tanzania yetu iko mikononi mwetu Mkuu.
 
Haya ndo mambo vijana tunatakiwa kushirikishana, sio ya kijingajinga na ndoto za alinacha. Mkuu hongera sana, na utabarikiwa sana. Binafsi ntaangalia uwezekano wa kukuona, niko Simiyu. Na ukame, uhaba wa maeneo ya malisho ni shida sana kwa wafugaji wetu.

Naamini nikielimika ktk hili ntawaokoa wengi sana. Kwanza nitajaribu kuwashirikisha wataalamu wa huku, tukishindwa nitakufuata Mkuu.

Nadhani huu utamaduni ukiendelezwa wa kushirikishana tutafika mbali sana, Tanzania yetu iko mikononi mwetu Mkuu.
WE ANDAA TREI, MBEGU NA NUTRIENTS
 
Waungwana naamini hamjambo!
Nitangulize shukrani za dhati kwenu wote mnaoutumia mda wenu vyema katika kuhakikisha yale mnayoyaelewa mnawaelekeza wengine.
Leo nataka niwajuze kile nilichokiona baada ya kupata maelezo mazuri kuhusu Hydroponic Fooder.

Kuna mjasiriamali mmoja alitoa maelekezo mazuri kuhusu namna ya kutengeneza chakula bora na kingi kwa mifugo kwa njia ya kisasa. Kweli nilinunua mahitaji na nikajaribu kutengeneza karibia mara mbili, nikawa nakwama.

Baadaye akajitokeza mjasiriamali mwingine akaelezea kwa kina na nashukuru sana kwa sababu alinilenga mimi binafsi kwa kunitumia PM. Nilipojaribu mara hii nilifanikiwa ila changamoto ikaja kwenye nutrients.

Nilifanikiwa kutafuta nutrients na bahati nzuri nikakutana na mtaalam ambaye kweli yeye aliwahi kutengeneza na ana uzoefu; tatizo kwake ni kwamba hana muda wa kufanya kazi hizo kwa sababu ametingwa na ajira. Alinipatia nutrients aina ya ID-Grow Green.

Bwana huyo pamoja na kwamba sikufahamiana naye kabla, alionesha nia ya kutaka kunifundisha na namshukuru Mungu yale aliyonifundisha niliyaelewa vyema.

Leo ni siku ya tatu tangu nimestawisha na naona maendeleo ni mazuri sana. Kwa kila hatua nitakayopitia nitawajuza ili wale wenye nia ya kuyafanyia kazi waweze kufanya huko waliko.

Angalizo: Kuna nutrients ambazo ukizitumia zinaweza zikasababisha madhara makubwa kwa mifugo yako na walaji pia.
Baada ya siku 9 nitakuja na full habari kuhusiana na kile nitakachokuwa nimekizalisha. Wenye nia msikose kuniuliza ili twende wote sambamba kwenye zoezi hili.
Shukran sana kiongozi
 
Kwanza nutrients ulo tumia inaitwa DI grow green na sio ID grow.

Zingatia tu hali ya hewa na joto ya mahali unapozalishia ndo jambo la msingi Sio lazima hutumie hyo unaweza tumia booster yoyote ya majan itasaidia kuyakimbiza yakue vyema mimi nastawisha na hata situmii hzo nutrients kutumia nutrients ni kujarbu kuzikimbiza tu ziwah kukua ndan ya muda mfupi ziwe kubwa.
Safi na hongera sana
Mkuu hii booster ya majani unachanganya na chakula cha kuku au?

Shukran
 
Kiukweli ukikutana na mtaalam wala hautatumia muda mwingi kuelewa kinachoendelea. Mimi atakayehitaji maelezo namkaribisha - tena hatua kwa hatua. Kikubwa ni kuandaa muda wa kupeana maelekezo. Ukifanikiwa wewe unakuwa umesaidia jamii.
Mkuu unapatikana wapi na unaweza kunisaidiaje step by step?

Ikiwezekana nije kwajili ya shamba darasa
 
Back
Top Bottom