Wana Jf naleta hii kutoka Arusha, kuna Askari wa barabarani (trafic) mitaa ya mianzini anasimamisha kila hiece (daladala) na na kijana mmoja anamchukulia 1000 kwa kila gari, akisha simamisha wala yeye hafati gari ila kijana mmoja anafahamika kama "Sheikh" ndiye anayefuata gari na kuchukua hela, nikamuuliza dereva mbona unatoa hela na trafic hajakufuata akasema yeye haji ila kijana wake ndo anakuja. sasa ukipiga hesabu ya kila daladala anakula 1000 na usipotoa anakuwekea kinyongo huyu kweli anatufaa???