Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 10,884
- 18,824
Nasoma soma historia ya Wazaramo. Nimekutana na hiki kisa.
Basi baada ya Vita Kuu ya Pili Serikali iliongeza kujenga skuli za vijijini katika sehemu kadha za Uzaramo.
Lakini sehemu nyingine migogoro ilitokea kati ya wazazi na walimu, kwa mfano Mwalimu Barnabas Mwinyiwaziri aliyekuwa akiendesha Skuli ya Mkamba mnamo 1948, alikamatwa na kuuawa shambani kwake na watu wasiojulikana.
Baadaye wenyeji wa Mkamba walipinga na kuikataa Skuli hiyo isiwemo katika nchi yao. Basi Skuli ile ikafungwa na majengo yake yakateketezwa.
Wenyeji wa Mkamba hawakupata skuli tena mpaka miaka hii ya karibuni baada ya nchi hii kujipatia uhuru, mnamo mwaka 1962.
Basi baada ya Vita Kuu ya Pili Serikali iliongeza kujenga skuli za vijijini katika sehemu kadha za Uzaramo.
Lakini sehemu nyingine migogoro ilitokea kati ya wazazi na walimu, kwa mfano Mwalimu Barnabas Mwinyiwaziri aliyekuwa akiendesha Skuli ya Mkamba mnamo 1948, alikamatwa na kuuawa shambani kwake na watu wasiojulikana.
Baadaye wenyeji wa Mkamba walipinga na kuikataa Skuli hiyo isiwemo katika nchi yao. Basi Skuli ile ikafungwa na majengo yake yakateketezwa.
Wenyeji wa Mkamba hawakupata skuli tena mpaka miaka hii ya karibuni baada ya nchi hii kujipatia uhuru, mnamo mwaka 1962.