Huyu si Lowassa ambaye UKAWA tulimtaka

Huyu si Lowassa ambaye UKAWA tulimtaka

Hatuitaji kutumia millions kulipia tvs wakati ushindi uko wazi kwa
Lowasa.Kumpat president sio voting peke yake...kuna maamuzi yanafanyika before and after voting.Rais anajulikana jamani msiumie sana waacheni ccm wajikamue wawezavo its too late
 
Kinyonga anabadilika kuakisi kile anachokiona/mazingira aliyeko....anaweza akawa wa blue kama yuko kwenye maeneo ya blue na anaweza kua mwekundu kama yupo kwenye eneo la rangi nyekundu, kipi ni kikgumu kinyonga kubadilika au mazingira kubadilika?

Upo sawa ni vigumu kwa mazingira kubadilika. je kinyonga anapobadilika rangi na kuwa wa blue kwa kufuata mazingira ya blue kunamfanya abadilike na tabia yake aliyokua nayo alipokuwa kwenye mazingira ya rangi nyekundu?
 
Unasikiliza Sera au unawasikiliza wasanii??? Wananchi tumechoka hatuhitaji wasanii tunahitaji mabadilikoo.
Kung'oa mizizi ya hii fisiemu sio rahisi dawa ni kwenda mapema kupiga kura na kuzilinda kura zetu.
😛eace:
 
Upo sawa ni vigumu kwa mazingira kubadilika. je kinyonga anapobadilika rangi na kuwa wa blue kwa kufuata mazingira ya blue kunamfanya abadilike na tabia yake aliyokua nayo alipokuwa kwenye mazingira ya rangi nyekundu?

Hapo nikuachie wewe ulieleta mfano wa kinyonga kwenye suala la rais. Mimi kazi yangu ilikua kujibu kwa mujibu wa bandiko lako.

Sasa hivi tunataka tupake rangi nyekundu kua ya blue, hatuhangaiki na kinyonga atafuata rangi ya mazingira aliyopo.
 
chema chajiuza, kibaya chajitembeza.... nafkiri umenielewa kamanda
 
Hapo nikuachie wewe ulieleta mfano wa kinyonga kwenye suala la rais. Mimi kazi yangu ilikua kujibu kwa mujibu wa bandiko lako.

Sasa hivi tunataka tupake rangi nyekundu kua ya blue, hatuhangaiki na kinyonga atafuata rangi ya mazingira aliyopo.

Aya mkuu tusubiri oktoba 25
 
Sasa wee ushakubali mikutano ya ukawa inajaa haswa bila wasanii...unawataka wa nini ilihali mikutano inajaa? Pili, sio mpango kuwaleta watu wafate wasanii. Watu wanatakiwa wavutwe na lengo kuu ambalo ni kusikiliza wagombea, sio wasanii
 
Sasa wee ushakubali mikutano ya ukawa inajaa haswa bila wasanii...unawataka wa nini ilihali mikutano inajaa? Pili, sio mpango kuwaleta watu wafate wasanii. Watu wanatakiwa wavutwe na lengo kuu ambalo ni kusikiliza wagombea, sio wasanii

Tunaoenda ktk mikutano, asilimia kubwa tumeshahamasika na kufanya maamuzi..
Ila tunawahitaji pia wale wa upande wa pili na ambao bado hawajafanya maamuzi.
Wasanii na kurusha mikutano live kunaweza kuongeza kura..
 
Aya mkuu tusubiri oktoba 25

Hapo umeongea ki utu uzima mkuu, tuko pamoja.

Hakuna haja ya watu kushupaliana ooh sijui Lowassa atashinda au Magufuli atashinda sijui nyomi leo funika, mara malori yamesomba watu....utaratibu uko wazi kabisa, unapiga kura mshindi anatangazwa na ndie anakua rais, awe Magufuli au Lowassa, maisha lazima yaendeleee!
 
Lowassa ambaye wengi wetu tulimtaka ahamie UKAWA, si huyu ambaye tunamshuhudia.
Kutaka kunielewa zaidi, hebu jaribu kukumbuka mkutano wake wakati wa kutangaza nia pale Arusha na ufananishe na mkutano wake wa leo Arusha.
Mkutano ule wa kwanza, ulionyesha kujiandaa.. Wasanii walijaa, vyombo karibu vyote vya habari vilikuwa live..
Tatizo sasa hivi liko wapi? Hana hela au ameishiwa? Bado sana kujihakikishia ushindi, tunahitaji kuongeza nguvu ktk medias, na pia kama inawezekana kuweka wasanii pia si vibaya kwani lengo ni kumpata kila mtu.
Hebu pata picha mikutano ya UKAWA inavyojaa leo bila wasanii wakubwa, je wangekuwepo ingekuwaje?
Wengine watabisha kwa hoja dhaifu ya kujitofautisha na fisiemu, bila kusahau lengo letu kubwa ni kuingia madarakani ndo maana tukamfanya Lowassa kuwa mgombea wetu.
Muda bado ungalipo, tubadilike.

Kwa hili niko upande wako ikiwa hakulipia matangazo za TV. Kama walilipia na wakahujumiwa itakuwa swala lingine.

Lakini kama hawakulipia kwa kweli ni kosa kubwa kwani Magufuli katoka juzi na propaganda kibao zilionyeshwa radioni na kwenye mitandao
Hivyo ilikuwa ni siku ya kuwajibu hata kama atarudi tena. Ukawa wajaribu kulipia matangazo Wanapofanya kampeni katika miji yote mikubwa iliyobaki kwani inawapa chachu hata miji yenye watu wachache kufuata mabadiliko inatusaidia hata sisi tulioko nje kusikiliza kwenye radio. Wamekosea tunaowaomba timu kampeni msirudie tena kosa
 
we Ni mrundi? hujui kuna
Hujuma rushwa, dhidi ya upinzani? uwanja wa mapamban hauko sawa
 
Magamba mwaka huu lazima Lowassa awatagishe ! Nami na sema na mtage tu . Lowassaaaaaaa !!!!!!!!!! Mabadilikooooooppppoooo !!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom