Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Ameandika Hilda Newton
Majina yake anaitwa Aidan Francis Msuya wengi humwita Danny, ni mtoto wa Mzee Msuya ambaye alikuwa mtumishi wa kawaida UDSM siyo Profesa.
Msuya amesoma shule ya Msingi Mlimani (UDSM), Secondary amesoma Tambaza na baadae akamalizia Mikoani.
Soma > Wanaodaiwa kuwa Watanzania wakamatwa nchini Kenya wakijaribu kumteka Mwanaharakati Mshabaha Hamza
Amezaliwa na kukulia Ubungo Msewe kwa Baba na mama yake na hapo hapo kwao kwanyuma ndiyo amejenga ghorofa lake japo kwasasa Wazazi wake wanaishi Kibaha-Mkoa wa Pwani.
Msuya anawatoto wa kike wote wapo watano na Mke wake muhaya maarufu kama Mama Ivana.
Msuya alishawahi kufanya kazi Airtel ila akafukuzwa bada ya kufukuzwa Airtel akawa mfanyabiashara wa kawaida.
Msuya aliingia CHADEMA 2014 akagombea Uenyekiti wa Serikali ya mtaa Ubungo Msewe akashinda kwa kumuondoa Jaffary Nyegesha (ambaye huyu jaffary ndiyo Diwani wa Ubungo leo hii)
Mwaka 2019 Msuya aligombea Uenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa kichama Ubungo na akashinda japo aliondolewa June 2020 na Katibu Mkuu, John Mnyika baada ya kuthibitika kwamba alishirikiana na Serikali ya ya Magufuli kumuondoa Meya wa Ubungo wakati huo Boniface Jacob.
Baada ya kuvuliwa Uongozi ndani ya CHADEMA, Msuya alikimbilia ACT ambako hadi sasa ni Mwanachama wao.
Kwasasa Msuya ameoa Mke mwingine Mzungu Raia wa Uswiss anaitwa Sandra, Sandra anamiliki Duka kubwa la Dawa maeneo ya Kisutu na amepanga Appartment Masaki wakaoishi kwa siri yeye pamoja na Aidan bila Mke wa Aidan (Danny) kujua.
MAISHA YA MASHAKA.
Msuya amekuwa na kesi nyingi za Ujambazi za kuvunja magodauni ya watu lakini huwa hafungwi.
Mwaka 2024 alikamatwa kwa kesi ya wizi wa mitandao ambapo yeye na wenzake waliiba Shilingi za kitanzania Bilioni 5 lakini aliachiwa katika mazingira ambayo ni tatanishi.
Machi 2025 alikamatwa kwa kesi nyingine ya wizi wa mtandao ambapo yeye na wenzake wengine waliiba bilioni 2 za kitanzania lakini Disemba 2025 yeye ambaye ni mtuhumiwa namba moja aliachiwa kwa NOLE ya DPP wenzake wote mpaka leo bado wako jela katika.
DPP alimfutia kesi Msuya kwasababu Msuya ni mtu wao ambaye TISS, Abdul na akina Mafwele huwa wanamtumia kwenye mambo yao meusi ikiwemo kuteka na kupoteza watu hasa wapinzani na Wanaharakati ambao wanaikosoa Serikali.
Ikumbukwe kuwa Dada yake Aidan Msuya ni Boss Mkubwa TISS (HR) ambapo mwaka 2016 Magufuli alimfukuza Dada yake Msuya pamoja Suleiman Mombo kwenye hiyo nafasi.
Dada yake Msuya akapelekewa India Ubalozini na Mombo akapelekwa ubalozini Brazil.
Dada yake Aidan alirejea Tanzania mwaka 2021 baada ya Samia kuingia madarakani na aliporudi tu nchini alimteuwa kuwa Naibu katibu mkuu wa Wizara baadae alimtoa Wizarani na kumrudisha Ikulu.
Februari 22, 2025 yaani Jumapili iliyopita Msuya akiwa na wenzake watatu nchini Kenya walifanya jaribio la kumteka Mwanaharakati Hamza Mshabaha bahati nzuri watekaji watatu walikamatwa na Jeshi la Polisi nchini Kenya ila Msuya alifanikiwa kukimbia na kurudi nchi mara baada jaribio lao kufeli.
Nimejulishwa kwamba Serikali ya Samia kupitia vyombo vya usalama wamempa Msuya na wenzake tenda ya kuhakikisha mie Hilda Newton, Maria Sarungi na Sativa tunauawa mahali popote ambapo watabahatika kumuona yeyote kati yetu na endapo watafanikisha hili watapewa mpunga mrefu sana ndiyo maana kasi ya kutuwinda imekuwa kubwa maana watekaji wanatuona sie fursa.
So mkimuona huyu kaka huko mtaani basi mjue huyu ni moja ya watu ambao wanaunda Genge la Kuteka, kupoteza na kuuwa watu.
Kama kuna mtu yeyote ambae anataarifa ya ziada kuhusu mtu huyu ikiwemo picha za Familia yake yaani mke wake wa kwanza na yule mzungu, fullname ya mzungu na jina la duka lake la dawa lakini pia kama unajua jina na picha ya Dada ake ambae ni afisa TISS zitatusaidia sana kwenye kufanikisha kumpata huyu muuaji
Mwisho kabisa namshukuru sana Mungu wetu kwa kuendelea kutupigania mpaka hapa tulipofika leo japo Vita ni kubwa, mapambano ni makali ila tutashinda kwasababu Mungu yupo upande wetu.🙏