Huyu nabii George Kairuki ni nani?

Huyu nabii George Kairuki ni nani?

Huyo jamaa nimeshawahi kumsikia hadi redioni. Nilimsikia kwa mara ya kwanza kipindi kile Kanumba amefariki. Anaeleza ushuhuda kwamba yeye pia alikua freemason ila alifanikiwa kuacha uanachama bila kudhurika. Anasema ameokoka yupo imara.. Freemason wanataka wamuue wanashindwa. Kama ni George huyo basi hizo ndio dondoo zake kwa ufupi.... Lakini nikuulize, Bahi kuna eneo linaitwa Singidani?
Ni mojawapo ya manabii waongo na hatari sana
 
Kwa pini iliyopo.... Mbona manabii wataibuka wengi tuu.... [emoji38][emoji38][emoji38]
 
Kuna nabii kaagiza twende na kufuli jumapili sijui ni ya nini
 
Ni vigumu sn kwa kipindi hichi kuwaamini baadhi ya hawa watu wanaojiita mitume, manabii, maana imeandikwa nao watatupwa jehanam na watasema"bwana bwana sikutoa mapepo kwa jina lako? Yesu atawajibu siwatambui" kwa ufupi tumia akili yako katika kila ufanyalo, kwani mungu amekupa akili ili ikisaidie kutafakari. Usiganye vitu kwa kufuata mkumbo bila kuishughulisha akili
 
huyo ni mjanja tu wa mjini anayeweza kucheza na akili za watu na kujipatia hela nyingi sana. mara ya kwanza jamaa kuingia dar alikuwa anaonekana sana maeneo ya posta na kariakoo akijifanya alikuwa freemason then akaacha na alikuja akiwa anatembelea miguu na kwa muda mfupi tu akaanza kutembelea matako baada ya kuwatepeli wabongo wasiokuwa na akili yaani vi*la*a. naona kaamua kuwafuata vijana wa JF walioko vijijini atawakomba mpaka mshindwe kunua ch*p* zenu za VIP
 
Biblia imesema Siku za mwisho (ambazo ndio hizi tulimo) watatokea manabii wengi wa uongo na watawadanganya wengi....... Usikubali kabisa kujipaka mafuta ya mtu kama huyo. Yamenuiziwa kiganga. Ukijipaka tu, unakuta hela zako karibu zo-o-te unampelekea yeye kama sadaka kwa mtumishi (wa Bwana) kumbe yeye bwana wake ni shetani sio Bwana Mungu
 
Mjasiliamali anayelitumia vibaya jina la yesu, hivi na yule aliyesema, wale waandishi waliomwandika vibaya hawataumaliza mwezi wa tatu, vipi wale waandishi washaanza kufa manake imebaki siku moja mwezi kuisha. Nataka ni muuzie mapipa ya kupikia gongo, kwani alisema wasipokufa atarudi kwao kijijini na kuacha kazi ya uchungaji akapike gongo.
 
Huyu Tapeli niliishwahi kumkuta Mnazi Mmoja na Kariakoo kwa Siku tofauti, huyu Tapeli kama matapeli wengine wanaotumia Kanisa kuwatapeli Watu!
 
Leo hii jamaa yupo hapa Mkiu pande za Mkuranga anahubiri alivyojitoa freemanson na kuuza mafuta ya mzaituni.
Kweli pesa inatafutwa jamani
 
Muda huu anaendelea kuhubiri hapa mtaani kwetu kuhusu Kanumba na Diamond kuwa ni ma 'freemason, tena anasema ana mafuta matakatifu kutoka kwa mungu ambayo atayatumia kuangamiza dunia anasema aliyaonyesha dah! Mji mzima ulipatwa na taharuki na kusema yeye ni nabii.

Ni kijana tu, amenyoa kiduku, t shirt lina mistari, ana suruali modo nyeupe amekuja na kagari kadogo ka 'kirikou' samahanini kwa kuandika bila mpangilio maana nipo kwenye msongamano wa watu.

Naomba mwenye taarifa za huyu mtu anipe

Chanzo: Mimi mhudhuriaji

Eneo: Dodoma, Bahi mission, eneo la Singidani
Kapicha tafadhali
 
Back
Top Bottom